Ushuhuda wa Mkristo: Jinsi Alivyoshinda Majaribu ya Kuwa na Mpenzi wa Siri (Sehemu ya 2)
Jingru akashusha pumzi kwa hisia, na kuwaza: “Isingekuwa kwa ajili ya Mungu kuniokoa na kunilinda kupitia maneno Yake, ningekuwa nimeharibika zamani sana na kuwa mtu bila mfano wa binadamu, na ningekuwa nimefanya mambo bila uadilifu au heshima, kama wale watu ambao wana uhusiano nje ya ndoa, ambao huwa wapenzi wa watu waliooa, na ambao huwa yule mwanamke mwingine. Pia ningetwishwa mzigo na jina baya la mvunja familia, na ningeishi maisha yaliyoshushwa hadhi, nikipitia shutuma ya dhamiri yangu mwenyewe.” Kwa dhati, Jingru alitoa shukrani na sifa kwa Mungu! Leo, maisha yake yamepata tena utulivu wake wa awali, kwa furaha yeye hutekeleza wajibu wake kanisani, hukubali hukumu na utakaso wa maneno ya Mungu, na anapiga hatua kwelekea kwenye maisha ya furaha ya kweli. Utukufu wote uwe kwa Mungu!