Wimbo wa Injili | Wanaomwacha Kristo wa Siku za Mwisho Wataadhibiwa Milele

04/04/2020

Watu wengi wanaweza kukosa kujali kuhusu kile Mungu anachosema,

lakini bado Mungu anataka kumwambia kila anayedaiwa

kuwa mtakatifu wa Mungu anayemfuata Yesu kwamba,

mtakapoona Yesu Akishuka kutoka juu mbinguni juu ya wingu jeupe

kwa macho yenu wenyewe,

huu ndio utakuwa mwonekano wa umma wa Jua la haki.

Pengine huo utakuwa wakati wa furaha kubwa kwako,

ilhali lazima ujue

kuwa wakati utakaposhuhudia Yesu Akishuka kutoka mbinguni

ndio pia wakati ambapo utaenda chini kuzimu kuadhibiwa.

Utaashiria mwisho wa mpango wa Mungu wa usimamizi,

na utakuwa wakati ambapo Mungu atawatunukia wazuri na kuwaadhibu waovu.

Kwani hukumu ya Mungu

itakuwa imeisha kabla ya mwanadamu kuona ishara,

wakati kuna onyesho la ukweli tu.

Wale wanaokubali ukweli na hawatafuti ishara, na hivyo wametakaswa,

watakuwa wamerudi mbele za kiti cha enzi cha Mungu

na kuingia katika kumbatio la Muumba.

Ni wale tu ambao wanashikilia imani kwamba

“Yesu Asiyeshuka juu ya wingu jeupe ni Kristo wa uongo”

Ni wale tu ambao wanashikilia imani kwamba

“Yesu Asiyeshuka juu ya wingu jeupe ni Kristo wa uongo”

watakabiliwa na adhabu ya milele,

kwani wanaamini tu katika Yesu ambaye Anaonyesha ishara,

lakini hawamkubali Yesu Anayetangaza hukumu kali na Anatoa njia ya kweli ya uzima.

Na hivyo itakuwa tu kuwa Yesu Atawashughulikia

tu Atakaporejea wazi wazi juu ya wingu jeupe.

kwani wanaamini tu katika Yesu ambaye Anaonyesha ishara,

lakini hawamkubali Yesu Anayetangaza hukumu kali na Anatoa njia ya kweli ya uzima.

Na hivyo itakuwa tu kuwa Yesu Atawashughulikia

tu Atakaporejea wazi wazi juu ya wingu jeupe.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp