01Ni nini hasa maana ya kuokolewa? Na kupata wokovu kamili kunamaanisha nini?

Watu wengi huamini kwamba kwa kumwamini Bwana dhambi zao zimesamehewa, kwamba kuokolewa mara moja ni kuokolewa milele na kwamba, Bwana atakapokuja tena, wanaweza kunyakuliwa mara moja na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Hata hivyo, ingawa dhambi za mwanadamu zimesamehewa, bado wamefungwa na asili yao ya dhambi, na wanaishi katika mzunguko wa kutenda dhambi na kukiri, bila uwezo wa kujiweka huru wenyewe. Asili ya dhambi ya mwanadamu haijatakaswa. Biblia inasema, “Utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana” (Waebrania 12:14). Hivyo je, wale ambao bado hawajatakaswa asili zao za dhambi ndiyo wale ambao wamepata wokovu kamili? Je, wanaweza kunyakuliwa moja kwa moja hadi katika ufalme wa mbinguni? Nini maana hasa ya kuokoka? Na kupata wokovu kamili kunamaanisha nini?

Aya za Biblia za Kurejelea

“Kwa kuwa Mungu hakumtuma Mwana wake duniani ili kuishutumu dunia; ila ili dunia iweze kuokolewa kupitia yeye” (Yohana 3:17).

“Yule ambaye anaamini na kubatizwa ataokolewa; lakini yule ambaye haamini atahukumiwa0” (Marko 16:16).

“Kwa kuwa hii ni damu yangu ya agano jipya, ambayo inamwagwa kwa ajiki ya msamaha wa dhambi” (Mathayo 26: 28).

“Utakatifu, bila huu hakuna mwanadamu atakayemwona Bwana” (Waebrania 12:14).

“Siye kila mmoja ambaye aliniambia, Bwana, Bwana, ataingia ufalme wa mbinguni, ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni” (Mathayo 7:21).

“Hao ndio wale wanaomfuata Mwanakondoo popote aendapo. Hawa walikombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu, wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na Mwanakondoo. Na vinywani mwao hakukuwa na hila: kwani hawana hatia mbele ya Kiti cha Mungu cha enzi” (Ufunuo 14:4-5).

02Ni kazi tu ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho inayoweza kuwawezesha watu kuachana na asili zao za dhambi, kutakaswa na kupata wokovu kamili

Watu wengine hufikiri kwamba katika imani ya mtu katika Bwana kubadilika kunamaanisha kutenda kwa mujibu wa maneno ya Bwana mambo kama vile unyenyekevu na uvumilivu, kujibebea msalaba, mtu kupenda adui zake na mtu kuhini mwili wake, pamoja na kuacha vitu vya dunia na kumfanyia Bwana kazi na kuhubiri kwa niaba ya Bwana. Wanauliza, kama yote wanayopaswa kufanya ni kufuatilia kwa njia hii ili waweze kupata wokovu wa Mungu, kwa nini basi wanahitaji kukubali kazi ya Mungu ya hukumu katika siku za mwisho?

Aya za Biblia za Kurejelea

“Hakika nawaambieni, Yeyote ambaye hutenda dhambi ni mtumishi wa dhambi. Na mtumishi haishi katika nyumba milele: lakini Mwana huishi milele” (Yohana 8:34-35).

“Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote” (Yohana 16:12-13).

“Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho” (Yohana 12:47-48).

“Kwa hiyo Kristo alitolewa mara moja kuzichukua dhambi za wengi; na kwa wale wamtazamiao ataonekana mara ya pili bila dhambi kwa wokovu” (Waebrania 9:28).

03Ahadi na baraka za Mungu kwa wale wanaotakaswa na wanaopata wokovu kamili

Aya za Biblia za Kurejelea

“Tazama, hema takatifu la Mungu liko pamoja nao watu, na yeye atakaa pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Na yeye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao, na kuwa Mungu wao. Na Mungu atayafuta machozi yote kutoka kwa macho yao, na hakutakuwa na kifo tena, wala huzuni, wala kilio, wala hakutakuwa na uchungu tena; maana yale mambo ya kale yamepita” (Ufunuo 21:3-4).

“Yeye aliye na sikio, na alisikie neno ambalo Roho aliyaambia makanisa. Kwa yule ambaye anashinda, nitampa matunda ya mti wa uzima ale, ambao uko katikati ya bustani ya Mungu” (Ufunuo 2:7).

“Yeye ambaye ana sikio, na asikie yale ambayo Roho alisema kwa makanisa; Yeye ambaye atashinda hataumizwa na kifo cha pili” (Ufunuo 2:11).

“Wamebarikiwa wale wanaofanya amri zake, ili wawe na haki ya mti wa uzima, na waweze kuingia mjini humo kupitia malango yake” (Ufunuo 22:14).

“Hawa ndio waliotoka katika taabu kubwa, na wameosha mavazi yao, na kuyageuza kuwa meupe katika damu ya Mwanakondoo. Kwa hiyo wao wako mbele ya kiti cha Mungu cha enzi, na wanamhudumia mchana na usiku hekaluni mwake: na Yeye anayeketi katika kiti hicho cha enzi ataishi kati yao. Hawahisi njaa tena, wala kuwa na kiu tena; wala jua kuwachoma, au joto yoyote. Kwa kuwa Mwanakondoo huyo ambaye yuko katikati ya kiti cha enzi atawalisha, na yeye atawaongoza hadi kwa chemchemi za maji ya uhai: naye Mungu atafuta machozi yote kutoka machoni mwao” (Ufunuo 7:14-17).

Kuokolewa dhidi ya Kupata Wokovu Kamili

Tovuti Rasmi