01Unabii wa kurudi kwa Bwana umetimia kimsingi, ukipiga king’ora cha siku za mwisho

Upotovu na uovu wa wanadamu sasa umefikia kilele, na unabii wa Biblia kuhusu kurudi kwa Bwana kwa kweli umetimia. Maafa yanazidi kuwa mabaya zaidi ulimwenguni kote: Matetemeko ya ardhi, tauni, njaa, na vita vimekuwa matukio ya mara kwa mara, na matukio yasiyo ya kawaida yameonekana angani. Siku za kurudi kwa Bwana zimefika, na Wakristo wengi wacha Mungu wanahisi kwamba tayari Amerudi …

Aya za Biblia za Kurejelea

“Na jinsi ilivyokuwa katika siku za Nuhu, hivyo ndivyo itakavyokuwa pia katika siku za Mwana wa Adamu. Walikula, walikunywa, walioa, waliolewa, mpaka siku ambayo Nuhu aliingia ndani ya safina, na gharika ikaja, na kuwaangamiza wote. Vile vile pia ilivyokuwa siku za Loti: walikula, wakanywa, walinunua, waliuza, walipanda, walijenga; Lakini siku iyo hiyo ambayo Loti alitoka Sodoma kulinyesha moto na kiberiti kutoka mbinguni, na kuwaangamiza wote. Hivyo ndivyo itakavyokuwa katika siku ambapo Mwanadamu atafunuliwa” (Luka 17:26–30).

“Kwani taifa litainuka dhidi ya taifa, na ufalme dhidi ya ufalme: na kutakuweko na njaa, na ndwele, na ardhi kutetemeka katika sehemu mbalimbali. Yote haya ndiyo asili ya huzun” (Mathayo 24: 7–8).

“Na nitaonyesha maajabu mbinguni na duniani, damu, na moto, na miimo ya moshi. Jua litageuzwa kuwa giza, na mwezi kuwa damu, kabla ya kuja kwa siku kuu na ya kutisha ya Yehova” (Yoeli 2:30-31).

“Na nikaona wakati ambapo alikuwa ameufungua muhuri wa sita, na, tazama, kulikuwa na tetemeko kubwa la ardhi; na jua likageuka kuwa jeusi kama gunia la nywele, na mwezi ukageuka kuwa kama damu; Na nyota za angani zikaanguka duniani, jinsi vile mtini unavyopukuta matini yake kwa wakati usiofaa unapotikiswa na upepo mkali” (Ufunuo 6:12-13).

02Njia mbili ambazo Bwana Yesu atarudi

Unabii wa Biblia kuhusu kurudi kwa Bwana haujumuishi tu Yeye kuja waziwazi juu ya mawingu, lakini pia unajumuisha Yeye kuja kwa siri, kama mwizi. Kwa hivyo basi, unabii wa kuja sirini na hadharani utatimizwaje? Tukimsubiri tu Bwana aje juu ya mawingu, lakini tusitilie maanani unabii wa kuja Kwake kama mwizi, je, tutaweza kukaribisha kuwasili kwa Bwana?

Aya za Biblia za Kurejelea

“Na ninyi pia muwe tayari: maana katika saa kama hii msiyofikiria kuwa Mwana wa Adamu atakuja” (Luka 12:40).

“Tazama, mimi nakuja kama mwizi” (Ufunuo 16:15).

“Tazama, nimesimama mlangoni, na kupiga hodi: mtu yeyote akisikia sauti yangu, na aufungue mlango, Mimi nitaingia kwake, na nitakula na yeye, na yeye na Mimi” (Ufunuo 3:20).

“Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha” (Mathayo 25:6).

“Kwani kama umeme, unavyomulika chini ya mbingu kutoka sehemu moja, huangaza hadi sehemu nyingine chini ya mbingu; vivyo ndivyo Mwana wa Adamu atakuwa katika siku yake. Bali kwanza lazima apitie mambo mengi, na akataliwe na kizazi hiki” (Luka 17:24-25).

“Tazama, anakuja na mawingu; nalo kila jicho litamwona yeye, na pia wale waliomdunga: na makabila yote ya ulimwengu yatalia kwa huzuni kwa sababu ya yeye. Hata hivyo, Amina” (Ufunuo 1:7).

“Na kisha itatokea ishara yake Mwana wa Adamu huko mbinguni: na kisha makabila yote ya dunia yataomboleza, na wao watamwona yule Mwana wa Adamu akifika kwa mawingu ya mbinguni akiwa na nguvu na utukufu mkubwa” (Mathayo 24:30).

03Mwokozi tayari amewasili kwa siri ili kuonyesha ukweli na kutekeleza kazi ya hukumu Akianzia katika nyumba ya Mungu

Miaka elfu mbili iliyopita, Bwana Yesu alitabiri kurudi Kwake, na sasa unabii wa kurudi kwa Bwana kimsingi umetimia. Bwana Yesu, Mwokozi wetu aliyesubiriwa kwa muda mrefu, Amekuja sirini, na Yeye ndiye Kristo wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu. Mwenyezi Mungu amefanya kazi ya hukumu akianza na nyumba ya Mungu, Amefichua siri za mpango wa Mungu wa usimamizi wa miaka elfu sita, na Ameonyesha ukweli wote ili kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu; Ametufichulia, sisi wanadamu, kiini kitakatifu na cha haki cha Mungu, na vile vile tabia Yake adhimu na yenye ghadhabu ambayo haitavumilia kosa lolote. Amefanya hivi ili kuwaokoa kabisa wanadamu kutoka kwa tabia zao potovu, kuwasaidia kuondokana na ushawishi wa Shetani, kufanyiza kundi la washindi kabla ya maafa, na kuleta wanadamu mwishowe kwenye hatima yao nzuri.

Aya za Biblia za Kurejelea

“Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, atawaongoza hadi kwenye ukweli wote” (Yohana 16:12-13).

“Yeye ambaye ana sikio, na asikie yale ambayo Roho alisema kwa makanisa; Yeye ambaye atashinda hataumizwa na kifo cha pili” (Ufunuo 2:29).

“Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa mimi, na hayakubali maneno yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho” (Yohana 12:47-48).

“Kwa maana muda umekuja ambao lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu” (1 Petro 4:17).

“Na nikamwona malaika mwingine akiruka katikati ya mbingu, akiwa na injili ya daima kuwahubiria hao wanaoishi katika ulimwengu, na kwa kila taifa, na ukoo, na lugha, na watu, Akisema kwa sauti kuu, Mwogopeni Mungu, na kumpa utukufu; kwa kuwa saa ya hukumu yake imekuja: na mumsujudie yule aliyeziumba mbingu, na ulimwengu, na bahari, na chemchemi za maji” (Ufunuo 14:6–7).

04Bwana anabisha mlangoni—kuwa mwanamwali mwenye busara na ukaribishe kurudi Kwake

Bwana Yesu alisema, “Tazama, nimesimama mlangoni, na kupiga hodi: mtu yeyote akisikia sauti yangu, na aufungue mlango, Mimi nitaingia kwake, na nitakula na yeye, na yeye na Mimi” (Ufunuo 3:20). “Kondoo wangu huisikia sauti yangu, na mimi Ninawajua, nao hunifuata” (Yohana 10:27). Ni wazi kwamba katika siku za mwisho, Mungu anabisha mlangoni pa wanadamu na kutafuta kondoo Wake kwa njia ya kunena maneno. Wale wanawali werevu ambao wanamwamini Mungu kweli na wanaotamani ukweli wanaweza kutafuta na kuchunguza kuonekana kwa Mungu wa siku za mwisho na kazi Yake wakiwa tayari kusikia maoni mapya, pasipo kuzuiwa na nguvu yoyote, na kwa hivyo wamesikia sauti ya Mungu na kumkaribisha Bwana. Hawa pekee ndio wana haki ya kuinuliwa mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kushiriki katika karamu kuu pamoja na Bwana.

Aya za Biblia za Kurejelea

“Hapo ndipo ufalme wa mbinguni utakapofananishwa na mabikira kumi, waliochukua taa zao, wakaondoka kwenda kumkaribisha bwana arusi. Na watano kati yao walikuwa wenye busara, na watano walikuwa wapumbavu. Wale wapumbavu walizichukua taa zao, na hawakubeba mafuta nao: Lakini wenye busara walibeba mafuta katika vyombo vyao walipochukua taa zao. Bwana harusi alipochelewa, wote walisinzia na kulala. Na kukawa na kelele saa sita ya usiku, Tazama, anakuja bwana arusi; ondokeni nje ili kumkaribisha. Kisha hao mabikira wote wakaamka na kutayarisha taa zao. Nao wapumbavu wakawaambia wale wenye busara, Tugawieni mafuta yenu kiasi; kwani taa zetu zimezimika. Lakini wenye busara wakajibu, wakisema, Hatuwezi; yasije yakakosa kututosha sisi na ninyi: lakini ni heri muende kwa wale wanaouza na mkajinunulie. Na wakati walienda kununua, bwana harusi alikuja; na wale waliokuwa tayari wakaingia ndani na yeye kwa harusi: nao mlango ukafungwa” (Mathayo 25:1-10).

“Tazama, nimesimama mlangoni, na kupiga hodi: mtu yeyote akisikia sauti yangu, na aufungue mlango, Mimi nitaingia kwake, na nitakula na yeye, na yeye na Mimi” (Ufunuo 3:20).

“Yeye ambaye ana sikio, na asikie yale ambayo Roho alisema kwa makanisa; Yeye ambaye atashinda hataumizwa na kifo cha pili” (Ufunuo 2:29).

“Kondoo wangu huisikia sauti yangu, na mimi Ninawajua, nao hunifuata” (Yohana 10:27).

“Ombeni, na mtapatiwa; tafuteni, na mtapata; pigeni hodi, na mtafunguliwa: Kwa sababu kila anayeomba hupata; na yeye ambaye hutafuta hupata; na apigaye hodi atafunguliwa” (Mathayo 7:7-8).

Makala ya Marejeo

Utabiri wa Nyakati za Mwisho Umetimia: Jinsi ya Kukaribisha Ujio wa Pili wa Bwana

Utabiri wa Nyakati za Mwisho Umetimia: Jinsi ya Kukaribisha Ujio wa Pili wa Bwana

Ishara za Nyakati za Mwisho Zimeonekana na Bwana Yesu Atarudije?

Ishara za Nyakati za Mwisho Zimeonekana na Bwana Yesu Atarudije?

Kufichua Siri ya “Lakini juu ya hiyo siku na saa hiyo hakuna mtu anayejua” katika Mathayo 24:36

Kufichua Siri ya “Lakini juu ya hiyo siku na saa hiyo hakuna mtu anayejua” katika Mathayo 24:36

Video za Marejeo

Mada Zaidi

Hukumu ya Kiti Kikuu Cheupe cha Enzi Ilianza Zamani
Hukumu ya Kiti Kikuu Cheupe cha Enzi Ilianza Zamani
Bwana Alisharudi Kitambo Akiwa Katika Mwili ili Aonekane na Kufanya Kazi
Bwana Alisharudi Kitambo Akiwa Katika Mwili ili Aonekane na Kufanya Kazi
Jinsi ya Kunyakuliwa Kabla ya Dhiki
Jinsi ya Kunyakuliwa Kabla ya Dhiki
Bwana Anavyoonekana Wakati wa Kurudi Kwake
Bwana Anavyoonekana Wakati wa Kurudi Kwake