01Ni mtu wa aina gani anayeweza kuingia katika ufalme wa mbinguni

Watu wengi hufikiri kwamba kwa kumwamini Bwana na kusamehewa dhambi zao, tayari wameokolewa kwa neema. Wanadhani kwamba kwa kumfanyia Bwana kazi kwa bidii, kwa kujitolea na kujitumia, kwamba hata ingawa hawajaondokana na utumwa wa dhambi, Bwana atakapokuja watanyakuliwa kwenda katika ufalme wa mbinguni.Mungu anasema, “Kwa hivyo mtakuwa watakatifu, kwa sababu mimi ni mtakatifu” (Walawi 11:45). Mungu ni mwenye haki na mtakatifu, kwa hivyo Anawezaje kuwaruhusu watu ambao wanatenda dhambi daima waingie katika ufalme Wake? Ni mtu wa aina gani anayeweza kuingia katika ufalme wa mbinguni kwa kweli?

Aya za Biblia za Kurejelea

“Hakika nawaambieni, Yeyote ambaye hutenda dhambi ni mtumishi wa dhambi. Na mtumishi haishi katika nyumba milele: lakini Mwana huishi milele” (Yohana 8:34-35).

“Siye kila mmoja ambaye aliniambia, Bwana, Bwana, ataingia ufalme wa mbinguni, ila yeye atendaye mapenzi ya Baba yangu ambaye yuko mbinguni. Wengi watasema kwangu siku hiyo, Bwana, Bwana, hatujatabiri kupitia jina lako? Na kutoa mapepo kupitia jina lako? Na kutenda miujiza mingi kupitia jina lako? Na hapo ndipo nitasema wazi kwao, Sikuwahi kuwajua: tokeni kwangu, ninyi ambao hutenda udhalimu” (Mathayo 7:21-23).

“Kwa maana mimi ni Yehova Mungu wenu: kwa hivyo mtajitakasa, na mtakuwa watakatifu; kwani mimi ni mtakatifu” (Walawi 11:44).

“Kweli nawaambia, Ila msipobadilishwa, na kugeuka kuwa kama wana wadogo, hamtaingia ndani ya ufalme wa mbinguni” (Mathayo 18:3).

“Hao ndio wale hawakunajisiwa na wanawake; kwani wao ni bikira. Hao ndio wale wanaomfuata Mwanakondoo popote aendapo. Hawa walikombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu, wakiwa matunda ya kwanza kwa Mungu na Mwanakondoo” (Ufunuo 14:4).

“Wamebarikiwa wale wanaofanya amri zake, ili wawe na haki ya mti wa uzima, na waweze kuingia mjini humo kupitia malango yake” (Ufunuo 22:14).

02Njia pekee ya kuingia katika ufalme wa mbinguni

Kazi ya Bwana Yesu ya ukombozi ilisamehe tu dhambi za mwanadamu, lakini haikutatua tabia potovu za wanadamu. Asili ya dhambi ya binadamu bado imekita mizizi, na ingawa tunaweza kuomba mara kwa mara na kukiri kwa Bwana, na kufanya kazi kwa bidii ili kumtumikia Bwana, hatuwezi kuondokana na utumwa wa dhambi, na hatuwezi kutakaswa na kuingia katika ufalme wa mbinguni. Kwa hivyo, Bwana anaporudi katika siku za mwisho, Anaonyesha ukweli na kufanya kazi ya hukumu kuanza na nyumba ya Mungu ili kusuluhisha kabisa asili ya dhambi ya wanadamu na tabia zao potovu, ili watu waondokane na dhambi na kutakaswa. Bila shaka, kukubali na kupata hukumu na kuadibu kwa maneno ya Mungu ndiyo njia pekee ya kupata wokovu kamili na kuingia ufalme wa mbinguni.

Aya za Biblia za Kurejelea

“Ninyi mnaohifadhiwa na nguvu zake Mungu kupitia imani hadi kwa wokovu ambao uko tayari kufichuliwa katika muda wa mwisho” (1 Petro 1:5).

“Siombi kwamba uwatoe ulimwenguni, bali uwalinde dhidi ya maovu. … Watakase kupitia kwa ukweli wako: neno lako ni ukweli. … Na kwa ajili yao najitakasa ili wao pia waweze kutakaswa kupitia kwa ukweli” ( Yohana 17:15-19).

“Bado ningali nayo mengi ya kuwaambieni, lakini hivi sasa hamwezi kuyavumilia. Hata hivyo, wakati Yeye, Roho wa ukweli, atakapokuja, Atawaongoza hadi kwenye ukweli wote: kwa maana Hatazungumza juu Yake Mwenyewe; bali chochote Atakachosikia, Atakinena: na Atawaonyesha mambo yajayo” (Yohana 16:12-13).

“Na iwapo mtu yeyote atayasikia maneno Yangu, na asiyaamini, Mimi sitamhukumu: kwa kuwa mimi sikuja ili niihukumu dunia, bali kuiokoa dunia. Yeye ambaye ananikataa Mimi, na hayakubali maneno Yangu, ana yule ambaye anamhukumu: neno hilo ambalo nimelisema, ndilo hilo ambalo litamhukumu katika siku ya mwisho” (Yohana 12:47-48).

“Kwa maana muda umekuja ambao lazima hukumu ianze katika nyumba ya Mungu” (1 Petro 4:17).

“Yule aliye dhalimu, basi aendelee kuwa dhalimu; na yeye aliye mtakatifu, na awe mtakatifu bado; na yeye aliye mwenye haki, awe mwenye haki bado: na yeye aliye mtakatifu, awe mtakatifu bado. Tazama, Naja upesi; na Nina thawabu Yangu, kumpa kila mwanadamu kulingana na vile matendo yake yatakuwa” (Ufunuo 22:11-12).

Makala ya Marejeo

Njia ya Utakaso

Njia ya Utakaso

Nimepata Njia ya Kuingia Katika Ufalme wa Mbinguni

Nimepata Njia ya Kuingia Katika Ufalme wa Mbinguni

Ukungu Waondoka na Napata Njia ya Ufalme wa Mbinguni

Ukungu Waondoka na Napata Njia ya Ufalme wa Mbinguni

Wakristo Wanawezaje Kuacha Kutenda Dhambi? Jibu Liko Hapa!

Wakristo Wanawezaje Kuacha Kutenda Dhambi? Jibu Liko Hapa!

Video za Marejeo

Mada Zaidi

Je, Umeisikia Sauti ya Mungu?
Je, Umeisikia Sauti ya Mungu?
Jinsi Mwanadamu Anaweza Kutakaswa Upotovu
Jinsi Mwanadamu Anaweza Kutakaswa Upotovu
Hukumu ya Kiti Kikuu Cheupe cha Enzi Ilianza Zamani
Hukumu ya Kiti Kikuu Cheupe cha Enzi Ilianza Zamani
Bwana Alisharudi Kitambo Akiwa Katika Mwili ili Aonekane na Kufanya Kazi
Bwana Alisharudi Kitambo Akiwa Katika Mwili ili Aonekane na Kufanya Kazi