Kuhusu Majina na Utambulisho (Sehemu ya Kwanza)

Iwapo unataka kufaa kwa ajili ya matumizi na Mungu, lazima uijue kazi ya Mungu; lazima uijue kazi Aliyofanya awali (katika Agano Jipya na la Kale), na, zaidi ya hayo, lazima uijue kazi Yake ya leo. Ndiyo kusema, ni lazima uzitambue hatua tatu za kazi ya Mungu ya zaidi ya miaka 6,000. Ukiulizwa ueneze injili, basi hutaweza kufanya hivyo bila kuijua kazi ya Mungu. Watu watakuuliza yote kuhusu Biblia, na Agano la Kale, na nini Yesu alisema na kufanya wakati huo. Watasema, “Mungu wenu hajawaeleza haya yote? Kama Yeye (Mungu) hawezi kuwaeleza ni nini hasa yanayoendelea kwa Biblia, basi Yeye si Mungu; kama Anaweza, basi tumeamini.” Mwanzoni, Yesu alizungumzia sana Agano la Kale na wanafunzi Wake. Kila kitu walichosoma kilitoka Agano la Kale; Agano Jipya liliandikwa tu miongo kadhaa baada ya kusulubiwa kwa Yesu. Kueneza injili, mnapaswa hasa kufahamu ukweli wa ndani wa Biblia, na kazi ya Mungu katika Israeli, ndiyo kusema kazi Aliyoifanya Yehova. Na pia mnapaswa kuelewa kazi aliyoifanya Yesu. Haya ndiyo sanasana maswala ambayo watu wote wana wasiwasi nayo, na hawana ufahamu wa[a] hizi hatua mbili za kazi. Wakati wa kueneza injili, kwanza weka kando majadiliano juu ya kazi ya Roho Mtakatifu leo. Hii hatua ya kazi hawawezi kufikia, kwa sababu mnachotafuta ni kile kilicho juu kuliko zote: maarifa ya Mungu, na maarifa ya kazi ya Roho Mtakatifu, na hakuna kilichopandishwa cheo zaidi ya hizi mbili. Ukizungumzia kwanza kilicho juu, itakuwa ni kubwa mno kwao, kwani hakuna hata mmoja wao aliye na uzoefu wa kazi hiyo ya Roho Mtakatifu; haina historia, na si rahisi kwa mwanadamu kukubali. Uzoefu wao ni mambo ya kale kutoka zamani, pamoja na baadhi ya kazi ya Roho Mtakatifu. Wanayopitia si kazi ya leo ya Roho Mtakatifu, ama mapenzi ya Mungu leo. Bado wanatenda kulingana na mazoea ya kale, bila mwangaza mpya wala mambo mapya.

Katika enzi ya Yesu, Roho Mtakatifu hasa alifanya kazi Yake ndani ya Yesu, wakati wale waliomtumikia Bwana wakivaa mavazi ya kuhani hekaluni walifanya hivyo wa uaminifu uliodumu. Wao pia walikuwa na kazi ya Roho Mtakatifu, lakini hawakuweza kuhisi mapenzi ya sasa ya Mungu, na wakabakia tu waaminifu kwa Yehova kulingana na mazoea ya kale, bila uongozi mpya. Yesu alikuja na kuleta kazi mpya. Wale watu hekaluni hawakuwa na uongozi mpya wala hawakuwa na kazi mpya. Wakihudumu hekaluni wangeweza tu kutetea mazoea ya kale; bila kuondoka hekaluni, hawangeweza kuwa na kuingia kupya. Kazi mpya ililetwa na Yesu, na Yesu hakuingia hekaluni kufanya kazi Yake. Alifanya kazi yake nje ya hekalu pekee, kwani wigo wa kazi ya Mungu ulikuwa umebadilika kitambo sana. Hakufanya kazi ndani ya hekalu, na mwanadamu alipomtumikia hapo ingeweza tu kuweka mambo yalivyokuwa, na haingeleta kazi yoyote mpya. Vivyo hivyo, watu wa dini bado huabudu Biblia leo. Ukieneza injili kwao, basi watabishana nawe kuhusu Biblia; na iwapo, wakiongea juu ya Biblia, utakosa maneno, ukose la kusema, basi watafikiria wewe ni mjinga katika imani yenu, ya kwamba hujui hata Biblia, Neno la Mungu, na unawezaje sema unamwamini Mungu? Kisha watakudharau, na kusema, “Sababu mnayemwamini ni Mungu, mbona Asiwaeleze yote kuhusu Agano la Kale na Jipya? Sababu Ameleta utukufu Wake kutoka Israeli hadi upande wa Mashariki, mbona hajui kazi iliyofanywa Israeli? Mbona hajui kazi ya Yesu? Kama hamjui, basi inathibitisha kwamba hamjaelezwa; sababu Yeye ndiye kupata mwili kwa Yesu kwa mara ya pili, ingewezekanaje kuwa hajui mambo haya? Yesu alijua kazi aliyoifanya Yehova; Angekosaje?” Wakati utakapofika, wote watakuuliza maswali kama haya. Vichwa vyao vimejaa mambo kama haya; watakosaje kuuliza? Wale walio katika mkondo huu hawazingatii Biblia, kwa vile mmetazama hatua kwa hatua kazi aliyoifanya Mungu leo, mmeshuhudia hii kazi ya hatua kwa hatua kwa macho yenu, mmeona wazi hatua tatu za kazi, na kwa hivyo imewabidi kuweka chini Biblia na kukoma kuitafiti. Lakini hawawezi kukosa kuitafiti, kwani hawana ujuzi wa hii kazi ya hatua kwa hatua. Watu wengine watauliza, “Nini tofauti kati ya kazi aliyoifanya Mungu wa mwili na ile ya manabii na mitume wa zamani?” Daudi pia aliitwa Bwana, na hivyo pia akawa Yesu; ingawa kazi waliyoifanya ilikuwa tofauti, waliitwa kitu kimoja. Mbona, unauliza, hawakuwa na utambulisho mmoja? Kile Yohana alichoshuhudia kilikuwa maono, moja iliyotoka pia kwa Roho Mtakatifu, na aliweza kuyasema maneno ambayo Roho Mtakatifu alikusudia kuyasema; kwa nini utambulisho wa Yohana ni tofauti na ule wa Yesu? Maneno aliyoyasema Yesu yaliweza kumwakilisha Mungu kikamilifu, na kuwakilisha kikamilifu kazi ya Mungu. Kile alichokiona Yohana kilikuwa maono, na hakuweza kuwakilisha kikamilifu kazi ya Mungu. Ni kwa nini Yohana, Petro na Paulo walizungumza maneno mengi—kama alivyofanya Yesu—lakini bado hawakuwa na utambulisho sawa na Yesu? Ni hasa kwa sababu kazi waliyoifanya ilikuwa tofauti. Yesu aliwakilisha Roho wa Mungu, na Alikuwa Roho wa Mungu Akifanya kazi moja kwa moja. Alifanya kazi ya enzi mpya, kazi ambayo hakuna aliyekuwa amefanya mbeleni. Yeye Alifungua njia mpya, Alimwakilisha Yehova, na Alimwakilisha Mungu Mwenyewe. Ilhali kwa Petro, Paulo na Daudi, bila kujali walichoitwa, waliwakilisha tu utambulisho wa kiumbe wa Mungu, ama walitumwa na Yesu na Yehova. Kwa hivyo bila kujali kiasi cha kazi walichofanya, bila kujali jinsi walivyofanya miujiza kubwa, walikuwa bado tu viumbe wa Mungu, na hawakuweza kuwakilisha Roho Mtakatifu. Walifanya kazi kwa jina la Mungu ama baada ya kutumwa na Mungu; zaidi ya hayo, walifanya kazi katika enzi iliyoanzishwa na Yesu ama Yehova, na kazi waliyoifanya haikutengwa. Walikuwa, hatimaye, viumbe wa Mungu tu. Katika Agano la Kale, manabii wengi walizungumza utabiri, ama kuandika vitabu vya unabii. Hakuna aliyesema kuwa yeye ni Mungu, lakini punde tu Yesu Alipojitokeza, kabla yeye kutamka neno lolote, Roho wa Mungu Alimshuhudia kuwa Yeye ni Mungu. Mbona hivyo? Kwa sasa, unapaswa kujua tayari! Awali, mitume na manabii waliandika nyaraka mbalimbali, na kufanya unabii mwingi. Baadaye, watu walichagua baadhi zao kuweka katika Biblia, na baadhi zikapotea. Kwa vile kuna watu wanaosema kuwa vitu vyote wanavyozungumza vimetoka kwa Roho Mtakatifu, mbona baadhi yavyo vinachukuliwa kuwa nzuri, na baadhi yavyo vinachukuliwa kuwa mbaya? Na mbona baadhi vilichaguliwa, na sio vingine? Kama kweli yalikuwa maneno Aliyoyasema Roho Mtakatifu, ingekuwa lazima kwa watu kuyachagua? Kwa nini akaunti ya maneno yaliyosemwa na Yesu na kazi Aliyoifanya ni tofauti katika kila moja ya Injili Nne? Makosa sio ya waliyoyarekodi? Watu wengine watauliza, “Sababu nyaraka zilizoandikwa na Paulo na waandishi wengine wa Agano Jipya na kazi walizozifanya zilitokana kidogo na matakwa ya mwanadamu, na zilichanganywa na dhana za mwanadamu, basi hakuna uchafu wa binadamu katika maneno ambayo Wewe (Mungu) unazungumza leo? Je, kweli hayana dhana hata moja za mwanadamu?” Hii hatua ya kazi aliyoifanya Mungu ni tofauti kabisa na zile walizozifanya Paulo na wengi wa mitume na manabii. Sio tu kwamba kuna tofauti na utambulisho, lakini, hasa, kuna tofauti kati ya kazi inayofanywa. Baada ya Paulo kupigwa chini na kuanguka mbele ya Bwana, aliongozwa na Roho Mtakatifu kufanya kazi, na akawa mtume. Na hivyo akaandikia makanisa nyaraka, na hizi nyaraka zote zilifuata mafundisho ya Yesu. Paulo alitumwa na Bwana kufanya kazi kwa jina la Bwana Yesu, lakini Mungu Mwenyewe alipokuja, Hakufanya kazi kwa jina lolote na Hakuwakilisha yeyote isipokuwa Roho wa Mungu katika kazi Yake. Mungu alikuja kufanya kazi Yake moja kwa moja: Hakukamilishwa na mwanadamu, na kazi Yake haikufanywa juu ya mafundisho ya mwanadamu yeyote. Katika hatua hii ya kazi Mungu haongozi kwa kuzungumza juu ya uzoefu Wake binafsi, ila Hufanya kazi Yake moja kwa moja, kulingana na Alicho nacho. Kwa mfano, Anafanya kazi ya watoa huduma, wa nyakati za kuadibu, kazi ya kifo, ya kumpenda Mungu…. Hii yote ni kazi ambayo haijawahi kufanywa mbeleni, na ni kazi ya enzi ya sasa, badala ya uzoefu wa binadamu. Kwa maneno Nimesema, ni yapi mazoefu ya mwanadamu? Je, yote hayatoki moja kwa moja kwa Roho Mtakatifu, na hayatolewi nje na Roho Mtakatifu? Ni vile tu aina yako ni maskini sana hadi huwezi kuona kupitia ukweli! Maisha ya vitendo Ninayozungumzia ni ya kuongoza njia, na hayajawahi zungumziwa na yeyote mbeleni, wala hakuna aliye na uzoefu wa njia hii, wala kujua ukweli huu. Kabla Niliyatamka maneno haya, hakuna aliyewahi kuyasema. Hakuna aliyezungumzia mazoefu haya, wala hakuna aliyewahi kusema maelezo hayo, na, zaidi ya hayo, hakuna aliyewahi kuonyesha hali kama hizo kufichua mambo haya. Hakuna aliyewahi kuongoza njia Ninayoongoza leo, na kama ingeongozwa na mwanadamu, basi isingekuwa njia mpya. Chukua Paulo na Petro, kwa mfano. Hawakuwa na mazoefu yao binafsi kabla ya kutembelea[b] njia iliyoongozwa na Yesu. Ilikuwa tu baada ya Yesu kuongoza njia ndipo walipopata uzoefu wa maneno aliyoyasema Yesu, na njia aliyoiongoza; kutoka hapa walipata mazoefu mengi, na kuziandika nyaraka, Na hivyo, uzoefu wa mwanadamu sio sawa na kazi Ya Mungu, na kazi ya Mungu sio sawa na maarifa yalivyoelezwa na dhana na uzoefu wa mwanadamu. Nimesema, tena na tena, kuwa leo Ninaongoza njia mpya, na kufanya kazi mpya, na kazi na matamshi Yangu ni tofauti na yale ya Yohana na wale manabii wengine wote. Kamwe, Sijawahi pata uzoefu kwanza, na kisha kuyazungumzia kwenu—hiyo sio ukweli hata kidogo. Kama ingekuwa hivyo, haingewachelewesha kitambo sana? Zamani, maarifa waliyoyazungumzia wengi yalipandishwa cheo pia, lakini maneno yao yote yalisemwa tu kulingana na hayo ya wanaoitwa takwimu wa kiroho. Hawakuiongoza njia, lakini walitoka kwa uzoefu wao, walitoka kwa walichokiona, na kwa maarifa yao. Zingine zilikuwa dhana zao, na mengine yalikuwa mazoefu waliyofupisha. Leo, asili ya kazi Yangu ni tofauti kabisa na yao. Sijapata uzoefu wa kuongozwa na wengine, wala Sijakubali kukamilishwa na wengine. Zaidi ya hayo, yote Nimesema na kushiriki ni tofauti na yale ya wengine, na hayajawahi kuzungumzwa na mwengine yeyote. Leo, bila kujali ninyi ni nani, kazi yenu inafanywa kulingana na maneno Nisemayo. Bila haya matamshi na kazi, nani angeweza kupata uzoefu wa mambo haya (majaribu ya[c] watendaji huduma, nyakati za kuadibu…), na nani ataweza kuzungumzia maarifa kama haya? Kweli huna uwezo wa kuona haya? Bila kujali hatua ya kazi, punde tu maneno Yangu yasemwapo, mnaanza kushiriki kulingana na maneno Yangu, na kufanya kazi kulingana nayo, na sio njia ambayo yeyote kati yenu amefikiria. Baada ya kuja mbali hivi, huna uwezo wa kuona swali wazi na rahisi hivi? Sio njia iliyowazwa na yeyote, wala haijalinganishwa na mtu yeyote wa kiroho. Ni njia mpya, na hata maneno mengi yaliyosemwa mara kwanza na Yesu hayatumiki tena. Ninachozungumza ni kazi ya kufungua enzi mpya, na ni kazi inayosimama peke yake; kazi Nifanyayo, na maneno Nizungumzayo, yote ni mapya. Si hii ndiyo kazi mpya ya leo? Kazi ya Yesu pia ilikuwa hivi. Kazi Yake pia ilikuwa tofauti na hizo za watu wengine hekaluni, na pia ilitofautiana na kazi za Mafarisayo, na wala haikufanana na zilizofanywa na watu wote wa Israeli. Baada ya kuishuhudia, watu walishindwa kuamua: Kweli ilifanywa na Mungu? Yesu hakuzingatia sheria ya Yehova; Alipokuja kumfunza mwanadamu, yote Aliyoyanena yalikuwa mapya na tofauti na yale yaliyosemwa na watakatifu wa zamani na manabii wa Agano la Kale, na kwa sababu hii, watu walisalia bila uhakika. Hii ndiyo humfanya mwanadamu kuwa mgumu sana kushughulika naye. Kabla ya kukubali hii hatua mpya ya kazi, njia ambayo wengi wenu walitembelea ilikuwa ya kutenda na kuingia katika msingi wa watu hao wa kiroho. Lakini leo, kazi Ninayoifanya ni tofauti sana, na hivyo hamna uwezo wa kuamua kama ni sawa ama sio. Sijalishwi na njia uliyopitia mbeleni, wala Sijali ulikula chakula cha nani, ama uliyemchukua kama “babako.” Sababu Nimekuja na kuleta kazi mpya ya kumwongoza mwanadamu, wote wanaonifuata lazima watende kulingana na Ninachosema. Bila kujali jinsi ulivyotoka “familia” ya nguvu, lazima unifuate, hupaswi kutenda kulingana na mazoea yako ya awali, “Baba wa kambo” wako anapaswa kushuka nawe unapaswa kuja mbele ya Mungu wako kupata mgao wako halali. Uzima wako wote umo mikononi Mwangu, nawe hupaswi kuwa na imani kipofu nyingi kwa baba wako wa kambo, hawezi kukutawala kabisa. Kazi ya leo inasimama peke yake. Yote Nisemayo leo ni wazi hayajalinganishwa na msingi wa zamani; ni mwanzo mpya, na ukisema kuwa umetengenezwa na mkono wa mwanadamu, basi wewe ni mmoja wa wale ambao hawawezi tibiwa upofu wao!

Isaya, Ezekieli, Musa, Daudi, Ibrahimu na Danieli walikuwa viongozi ama manabii kati ya wateule wa Israeli. Mbona hawakuitwa Mungu? Mbona Roho Mtakatifu hakuwashuhudia? Mbona Roho Mtakatifu alimshuhudia Yesu punde tu Alipoanza kazi yake na kuanza kuzungumza maneno Yake? Na mbona Roho Mtakatifu hakuwashuhudia wengine? Wao, wanadamu waliokuwa na mwili, wote waliitwa “Bwana.” Bila kujali waliyoitwa, kazi yao inawakilisha utu wao na kiini chao, na utu wao na kiini chao kinawakilisha utambulisho wao. Kiini chao hakina uhusiano na majina yao, inawakilishwa na waliyoonyesha, na waliyoishi kwa kudhihirisha. Kwa Agano la Kale, hakuwa na chochote tofauti na kuitwa Bwana, na mtu angeitwa kwa njia yoyote, lakini kiini na utambulisho wake wa asili ulikuwa haubadiliki. Kati ya hao Kristo wa uwongo, manabii waongo na wadanganyifu, hakuna wanaoitwa Mungu pia? Na mbona hao sio Mungu? Kwa sababu hawana uwezo wa kufanya kazi ya Mungu. Mizizini, wao ni wanadamu, wanaowadanganya watu, sio Mungu, na hivyo hawana utambulisho wa Mungu. Daudi pia hakuitwa Bwana miongoni mwa makabila kumi na mawili? Yesu pia aliitwa Bwana: mbona ni Yesu pekee aliyeitwa Mungu wa mwili? Yeremia pia hakujulikana kama Mwana wa Adamu? Na Yesu pia hakujulikana kama Mwana wa Adamu? Mbona Yesu alisulubiwa kwa niaba ya Mungu? Si kwa sababu kiini chake kilikuwa tofauti? Si kwa sababu kazi aliyoifanya ilikuwa tofauti? Je, jina lina umuhimu? Ingawa Yesu pia aliitwa Mwana wa Adamu, Alikuwa kupata mwili kwa Mungu kwa mara ya kwanza. Alikuwa amekuja kuchukua mamlaka, na kukamilisha kazi ya ukombozi. Hii inathibitisha kuwa utambulisho na kiini cha Yesu kilikuwa tofauti na kile cha wengine walioitwa pia wana wa wanadamu. Leo, nani kati yenu anathubutu kusema kwamba maneno yote yaliyotamkwa na wale waliotumiwa na Roho Mtakatifu yalitoka kwa Roho Mtakatifu? Kuna anayethubutu kusema mambo kama haya? Ukisema mambo kama haya, basi mbona kitabu cha Ezra cha unabii kiliondolewa, na mbona jambo hilo pia likafanyiwa vitabu vya watakatifu na manabii wa kale? Kama yote yalitoka kwa Roho Mtakatifu, basi mbona mnathubutu kufanya maamuzi ambayo yanabadilika kama haya? Umehitimu kuchagua kazi ya Roho Mtakatifu? Hadithi nyingi kutoka Israeli pia zilitolewa. Na ukiamini kwamba maandishi haya yote ya kale yalitoka Roho Mtakatifu, basi mbona baadhi ya vitabu vilitolewa? Kama yote yalitoka kwa Roho Mtakatifu, yote yanapaswa kuwekwa, na kutumwa kwa ndugu na dada wa makanisa kuyasoma. Hayapaswi kuchaguliwa na kutolewa kwa matakwa ya mwanadamu; ni makosa kufanya hivyo. Kusema kwamba mazoefu ya Paulo na Yohana yalichanganywa na waliyoyaona binafsi hakumaanishi kwamba uzoefu na umaarifa wao ulitoka kwa Shetani, ila tu walikuwa na mambo yaliyotoka kwa mazoefu na waliyoyaona wao binafsi. Maarifa yao yalilingana na asili ya mazoefu halisi ya wakati huo, na ni nani anayeweza kusema kwa ujasiri kwamba yote yalitoka kwa Roho Mtakatifu? Kama Injili Nne zote zilitoka kwa Roho Mtakatifu, basi ilikuwaje kwamba Mathayo, Marko, Luka na Yohana kila mmoja alisema jambo tofauti kuhusu kazi ya Yesu? Msipoamini haya, basi angalia akaunti tofauti kwa Biblia ya jinsi Petro alivyomkana Yesu mara tatu: Yote ni tofauti, na kila moja ina sifa yake yenyewe. Wengi walio wajinga husema, Mungu wa mwili pia Alikuwa mwanadamu, kwa hivyo maneno Aliyoyazungumza yangeweza kutoka kikamilifu kwa Roho Mtakatifu? Kama maneno ya Paulo na Yohana yalichanganywa na matakwa ya mwanadamu, basi maneno Aliyoyasema yalikuwa kweli hayajachanganywa na matakwa ya mwanadamu? Watu wanaosema mambo kama haya ni vipofu na wajinga! Soma Injili Nne kwa kina; soma iliyorekodi kuhusu alichofanya Yesu, na maneno Aliyoyasema. Kila akaunti ilikuwa, kwa urahisi, tofauti, na kila ilikuwa na mtazamo wake. Kama vilivyoandikwa na waandishi wa vitabu hivi vyote vilitoka kwa Roho Mtakatifu, basi yote yanapaswa kuwa sawa na thabiti. Basi mbona kuna tofauti? Si mwanadamu ni mjinga sana, kutoweza kuona haya? Ukiulizwa kutoa ushuhuda kwa Mungu, ni ushuhuda upi unaoweza kutoa? Njia hii ya kumjua Mungu inaweza kumshuhudia? Wengine wakikuuliza, “Kama rekodi ya Yohana na Luka yalichanganywa na matakwa ya mwanadamu, basi maneno yanayosemwa na Mungu wenu hayajachanganywa na matakwa ya mwanadamu?” utaweza kupeana jibu wazi? Baada ya Luka na Mathayo kuyasikia maneno ya Yesu, na kuona kazi ya Yesu, walizungumzia maarifa yao, kwa namna ya kumbukumbu walisema kwa kina baadhi ya mambo aliyoyafanya Yesu. Unaweza kusema kwamba maarifa yao yalifichuliwa kabisa na Roho Mtakatifu? Nje ya Biblia, kulikuwa na watu wengi wa kiroho wa maarifa ya juu kuwaliko; mbona maneno yao hayajachukuliwa na vizazi vya baadaye? Wao hawakutumika pia na Roho Mtakatifu? Jua kwamba kwa kazi ya leo, Sizungumzii juu ya kuona kwangu kunaolingana na msingi wa kazi ya Yesu, wala Sizungumzi juu ya maarifa Yangu dhidi ya usuli wa kazi ya Yesu. Ni kazi ipi Aliyofanya Yesu wakati huo? Na ni kazi ipi Ninayofanya leo? Ninachofanya na kusema hayana historia. Njia Nitembeleayo leo haijawahi kukanyagiwa mbeleni, haikuwahi tembelewa na watu wa enzi na vizazi vya kale. Leo, imefunguliwa, na hii sio kazi ya Roho? Hata kama ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu, viongozi wote wa kale walifanya kazi yao juu ya msingi wa wengine. Lakini kazi ya Mungu Mwenyewe ni tofauti, ilivyokuwa tu kazi ya hatua ya Yesu: Aliifungua njia mpya. Alipokuja Alihubiri injili ya ufalme wa mbinguni, na kusema kwamba mwanadamu anapaswa kutubu, na kukiri. Baada ya Yesu kukamilisha kazi yake, Petro na Paulo na wengineo walianza kuendeleza kazi ya Yesu. Baada ya Yesu kusulubiwa na kupaa mbinguni, walitumwa na Roho Mtakatifu kueneza njia ya msalaba. Ingawa maneno ya Paulo yalipandishwa cheo, pia yalilingana na msingi uliolazwa na Yesu, kama uvumilivu, upendo, mateso, kufunika kichwa, ubatizo, ama mafundisho mengine yakufuatwa. Haya yote yalikuwa juu ya msingi wa maneno ya Yesu. Hawakuwa na uwezo wa kufungua njia mpya, kwani wote walikuwa wanadamu waliotumiwa na Mungu.

Matamshi na kazi ya Yesu wakati huo hayakushikilia mafundisho, na hakufanya kazi Yake kulingana na kazi ya sheria ya Agano la Kale. Yalilingana na kazi iliyopaswa kufanywa kwa Enzi ya Neema. Alitenda kulingana na kazi Aliyokuwa ameleta mbele, kulingana na mipango Yake, na kulingana na huduma Yake; Hakufanya kazi kulingana na sheria ya Agano la Kale. Hakuna Alichofanya kilicholingana na Agano la Kale, na Hakuja kufanya kazi ili kutimiza maneno ya manabii. Kila hatua ya kazi ya Mungu haikuwa wazi ili kutimiza utabiri wa manabii wa zamani, na Hakuja kuyafuata mafundisho au kutambua makusudi utabiri wa manabii wa kale. Bado vitendo Vyake havikuvuruga utabiri wa manabii wa kale, wala havikuvuruga kazi Aliyokuwa amefanya awali. Hatua muhimu ya kazi Yake haikuwa kufuata mafundisho yoyote, na kufanya kazi ambayo Yeye Mwenyewe anapaswa kufanya. Yeye hakuwa nabii wala mwaguzi, ila mtendaji, aliyekuja kufanya hiyo kazi Aliyopaswa kufanya, na aliyekuja kufungua enzi Yake mpya na kufanya kazi Yake mpya. Bila shaka, Yesu alipokuja kufanya kazi Yake, pia Alitimiza maneno mengi yaliyosemwa na manabii wa zamani kwa Agano la Kale. Hivyo pia kazi ya leo imetimiza utabiri wa manabii wa zamani wa Agano la Kale. Ni vile tu Sishikilii hiyo “kalenda njano ya zamani,” hayo tu. Kwani kuna kazi zaidi ambayo lazima Nifanye, kuna maneno zaidi ambayo lazima Niwazungumzie, na kazi hii na maneno haya ni ya umuhimu mkubwa kuliko kueleza vifungu kutoka Biblia, kwa sababu kazi kama hiyo haina maana ama thamani kubwa kwenu, na haiwezi kuwasaidia, au kuwabadilisha. Ninanuia kufanya kazi mpya sio kwa ajili ya kutimiza kifungu chochote kutoka Biblia. Ikiwa Mungu alikuja duniani tu kutimiza maneno ya manabii wa Biblia, basi ni nani aliye mkuu, Mungu wa mwili ama hao manabii wa zamani. Na hata hivyo, hao manabii ni wasimamizi wa Mungu, ama Mungu ni msimamizi wa manabii? Unaweza kueleza haya maneno jinsi gani?

Tanbihi:

a. Nakala ya awali imeacha “ufahamu wa.”

b. Nakala ya awali imeacha “kutembea juu ya.”

c. Nakala ya awali imeacha “majaribu ya.”

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp