Vitabu

  • Neno Laonekana katika Mwili

    Kuonekana na Kazi ya Mungu

    Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, ambaye Ameonekana kufanya kazi Yake, anaonyesha ukweli wote ambao huwatakasa na kuwaokoa wanadamu, na wote umejumuishwa katika Neno Laonekana katika Mwili. Hili limetimiza kile kilichoandikwa katika Biblia: “Mwanzoni kulikuwa na Neno, na Neno alikuwa na Mungu, na Neno alikuwa Mungu(Yohana 1:1). Na kuhusu Neno Laonekana katika Mwili, hiyo pia ilikuwa mara ya kwanza Alipozungumza mengi hivyo, na kwa muda mrefu sana, kwa wanadamu wote. Ilikuwa ya kipekee kabisa. Na zaidi, matamshi haya yalikuwa maneno halisi ya kwanza yaliyoonyeshwa na Mungu miongoni mwa wanadamu ambapo Aliwafichua watu, akawaongoza, akawahukumu, na kuzungumza nao wazi wazi na kwa hiyo, pia, yalikuwa matamshi ya kwanza ambayo kwayo Mungu aliwaruhusu watu wajue nyayo Zake, mahali Anapokaa, tabia ya Mungu, kile Mungu anacho na alicho, mawazo ya Mungu, na sikitiko Lake kwa wanadamu. Inaweza kusemwa kwamba haya yalikuwa matamshi ya kwanza ambayo Mungu alikuwa amezungumza kwa wanadamu kutoka mbingu ya tatu tangu uumbaji, na mara ya kwanza ambapo Mungu alikuwa ametumia utambulisho Wake wa asili kuonekana na kuonyesha sauti Yake kwa wanadamu katikati ya maneno. Neno Laonekana katika Mwili (linalofupishwa kama Neno), kilichoonenwa na Kristo wa Siku za Mwisho, Mwenyezi Mungu, kwa sasa kina buku sita: Buku la Kwanza, Kuonekana na Kazi ya Mungu; Buku la Pili, Kuhusu Kumjua Mungu; Buku la Tatu, Mihadhara ya Kristo wa Siku za Mwisho; Buku la Nne, Kuwafichua Wapinga Kristo; Buku la Tano, Majukumu ya Viongozi na Wafanyakazi; na Buku la Sita, Kuhusu Ufuatiliaji wa Ukweli.
  • Kuhusu Kumjua Mungu

    Kuhusu Kumjua Mungu, buku la pili la Neno Laonekana katika Mwili, lina matamko ya Kristo wa siku, Mwenyezi Mungu, za mwisho kwa binadamu wote, yakija baada ya yale ya yaliyo katika Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu anafafanua juu ya ukweli mbalimbali kama vile kazi ambayo Amefanya tangu aumbe ulimwengu, mapenzi Yake na matarajio Yake kwa wanadamu yaliyomo humo ndani, na mbubujiko wa kila kitu ambacho Mungu anacho na alicho kutokana na kazi Yake, na vile vile haki Yake, mamlaka Yake, utakatifu Wake na ukweli kwamba Yeye ndiye chanzo cha uzima wa vitu vyote. Baada ya kukisoma kitabu hiki, wale wanaomwamini Mungu kwa kweli wataweza kuthibitisha kwamba Yule anayeweza kufanya kazi hii na kumimina tabia hizi ndiye Mkuu juu ya vitu vyote, na pia wanaweza kujua kwa kweli kuhusu utambulisho wa Mungu, hadhi Yake na kiini Chake, na hivyo kuthibitisha kwamba Kristo wa siku za mwisho, Mwenyezi Mungu, ni Mungu Mwenyewe, wa kipekee.
  • Hukumu Yaanza na Nyumba ya Mungu

    Hukumu Yaanza na Nyumba ya Mungu

    Chaguzi zilizo katika kitabu hiki zote ni maneno yaliyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu kwa ajili ya kazi Yake ya hukumu katika siku za mwisho, zilizochukuliwa hasa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili, Vol 1, Kuonekana na Kazi ya Mungu. Ni ukweli ambao kila mtu anayetafuta na kuchunguza kazi ya Mungu katika siku za mwisho anahitaji kupata kwa haraka sana. Maonyesho ya Mungu katika kitabu hiki ni yale ambayo Roho Mtakatifu anayanena kwa makanisa kama ilivyotabiriwa katika Kitabu cha Ufunuo. Maneno haya ya sasa ya Mungu ni ushuhuda bora wa kuonekana Kwake na kazi Yake, na vile vile ushuhuda bora wa ukweli kwamba Kristo ndiye ukweli, njia na uzima. Kitabu hiki kinanuiwa kuwawezesha wale wote wanaotamani kuonekana kwa Mungu waisikie sauti Yake haraka iwezekanavyo. Tunatumaini kwamba wote wanaosubiri kuja kwa Bwana na wanaotazamia kuonekana kwa Mungu na kazi Yake wataweza kusoma kitabu hiki.
  • Maneno Yaliyo Bora Kabisa Kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Kristo wa Siku za Mwisho

    Maneno Yaliyo Bora Kabisa Kutoka kwa Mwenyezi Mungu, Kristo wa Siku za Mwisho

    Kitabu hiki kina dondoo kutoka katika maneno yaliyo bora kabisa yaliyoonyeshwa na Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, katika Neno Laonekana katika Mwili. Maneno haya yaliyo bora kabisa yanafafanua ukweli moja kwa moja, na yanaweza kuwawezesha watu waelewe mapenzi ya Mungu moja kwa moja, waje kuijua kazi Yake, na wapate maarifa kuhusu tabia Yake na kile Anacho na alicho. Maneno haya ni mwongozo ambao kwao wale wote wanaotamani sana kuonekana kwa Mungu wanaweza kutafuta nyayo Zake. Yanaweza kukuongoza upate mlango wa kuingia katika ufalme wa mbinguni.
  • Maneno ya Mungu ya Kila Siku

    Maneno ya Mungu ya Kila Siku

    Kitabu hiki kina vifungu vilivyoteuliwa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili. Ili kwamba wateule wa Mungu waweze kupata ukweli na riziki ya kila siku ya uzima kutoka katika maneno Yake, maneno haya yaliyo bora kabisa ya Mwenyezi Mungu, ambayo yanaadilisha sana kwa kuingia kwa watu katika uzima, hapa yameteuliwa kwa njia maalumu ili watu wafurahie, na hivyo kuwaruhusu wale wanaopenda ukweli waweze kuuelewa, waweze kuishi mbele za Mungu, na kuokolewa na kukamilishwa na Mungu. Maneno haya yaliyo bora kabisa ya Mungu ni maonyesho ya ukweli; aidha, haya ndiyo kanuni zilizo bora kabisa zaidi za maisha, na hakuna maneno yanayowaadilisha na kuwanufaisha watu zaidi ya haya. Ukiweza kweli kufurahia kifungu kimoja cha maneno haya kila siku, basi hii ndiyo neema yako kubwa kabisa, na umebarikiwa na Mungu.
  • Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

    Kitabu hiki cha nyimbo za dini kimegawanywa katika sehemu mbili kuu: Ya kwanza inajumuisha nyimbo za dini za maneno ya Mungu, ambazo zinajumuisha matamko yaliyo bora kabisa kutoka kwa Mwenyezi Mungu, na ya pili inajumuisha nyimbo za dini za maisha ya kanisa, ambazo ni ushuhuda halisi wa wateule wa Mungu uliotolewa baada ya kupitia hukumu Yake na ugumu na dhiki wakiwa wanamfuata. Nyimbo hizi za dini ni za faida kubwa kwa watu katika kufanya ibada zao za kiroho, kumkaribia Mungu, kutafakari maneno Yake, na kuelewa ukweli. Ni za faida kubwa hata zaidi kwa watu wanaopitia maneno ya Mungu na kuingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu.
  • Kondoo wa Mungu Huisikia Sauti ya Mungu (Mambo Muhimu ya Muumini Mpya)

    Kondoo wa Mungu Huisikia Sauti ya Mungu

    Kitabu hiki ni mkusanyiko wa ukweli wa maono kama vile hatua tatu za kazi ya Mungu, majina Yake, siri ya kupata mwili Kwake, na jinsi ya kutofautisha kati ya njia ya kweli na njia za uwongo. Kinaweza kusomwa na kutumiwa kujiandaa na wale ambao wameikubali kazi ya Mungu ya siku za mwisho hivi karibuni, ili waweze kuelewa ukweli wa maono wa kazi ya Mungu na kuweka misingi haraka iwezekanavyo kwenye njia ya kweli.
  • Sikiliza Sauti ya Mungu      Tazama Kuonekana kwa Mungu

    Mabikira wenye busara wataitambua sauti ya Mungu na kuiona sura Yake kutoka katika matamko Yake, na wakaribishe kurudi kwa Bwana. Kitabu hiki ni mkusanyiko wa ukweli unaohusiana na kupata mwili kwa Mungu na hatua Zake tatu za kazi ya wokovu. Ukweli huu unashuhudia kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho: Mwenyezi Mungu ndiye Bwana Yesu aliyerudi, na Ameonyesha ukweli na Anafanya kazi ya “hukumu kuanzia katika nyumba ya Mungu” katika siku za mwisho, na hivyo kuwaongoza wanadamu kugeuka na kurudi kuelekea kiti cha enzi cha Mungu.
  • Ushuhuda wa Uzoefu Mbele ya Kiti cha Hukumu cha Kristo

    Hukumu mbele ya kiti kikuu cheupe cha enzi ya siku za mwisho imeanza! Mwenyezi Mungu, Kristo wa siku za mwisho, Ameonyesha ukweli ili kutekeleza kazi Yake ya kuwahukumu na kuwatakasa wanadamu. Kupitia ufunuo na hukumu ya maneno ya Mungu, wateule Wake wanajua ukweli wa upotovu wao wa kishetani polepole na kupata njia ya kuutoroka ushawishi wa Shetani na kupata wokovu, na polepole wanaona mabadiliko katika tabia zao za maisha. Matukio haya halisi yanashuhudia kwamba kazi ya hukumu inayotekelezwa na Mwenyezi Mungu ni kazi ya kuwatakasa na kuwaokoa wanadamu kikamilifu.
  • Jinsi Nilivyomgeukia Mwenyezi Mungu Tena

    Kila mtu anayemwamini Mungu ana hadithi maalumu kuhusu safari yake binafsi ya kurejea Kwake. Kitabu hiki kinashiriki mambo halisi waliyopitia wateule wa Mungu katika kupokea mwongozo kutoka kwa maneno ya Mwenyezi Mungu, wakiwa na uhakika kuhusu njia ya kweli, na kurudi mbele ya kiti Chake cha enzi. Wengine walijinasua kutokana na minyororo na shutuma za mawazo yao ya kidini, wengine walitoroka kuvurugika na kuteswa na nguvu za wapinga Kristo katika jamii za kidini na nguvu za uovu za Chama cha Kikomunisti cha China, na bado wengine walipata utambuzi kuhusu mienendo miovu ya ulimwengu. Mwishowe, wote walirudi mbele za Mungu.

    Wasiliana nasi kupitia WhatsApp