Kupata Mwili kwa Mungu Hukumu ya Siku za Mwisho Hatua Tatu za Kazi ya Mungu Kuhusiana na Majina ya Mungu Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme Wokovu na Wokovu Kamili Njia ya Uzima wa Milele Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu Kumjua Kristo Kumjua Mungu Biblia na Mungu Kuijua Sauti ya Mungu Maana ya Kweli ya Unyakuo Mungu Ameshuka Nchini China Kanisa la Mungu na Dini Kuwatambua Mafarisayo Njia ya Kweli Imekuwa Ikiteswa Daima Ufafanuzi wa Utatu Ukweli na Mafundisho ya Dini Kufanya Mapenzi ya Mungu
  • Aina 20 za Ukweli wa Injili
    • Kupata Mwili kwa Mungu
    • Hukumu ya Siku za Mwisho
    • Hatua Tatu za Kazi ya Mungu
    • Kuhusiana na Majina ya Mungu
    • Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme
    • Wokovu na Wokovu Kamili
    • Njia ya Uzima wa Milele
    • Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu
    • Kumjua Kristo
    • Kumjua Mungu
    • Biblia na Mungu
    • Kuijua Sauti ya Mungu
    • Maana ya Kweli ya Unyakuo
    • Mungu Ameshuka Nchini China
    • Kanisa la Mungu na Dini
    • Kuwatambua Mafarisayo
    • Njia ya Kweli Imekuwa Ikiteswa Daima
    • Ufafanuzi wa Utatu
    • Ukweli na Mafundisho ya Dini
    • Kufanya Mapenzi ya Mungu
Kuhusiana na Majina ya Mungu

Uhusiano gani kati ya kila hatua ya kazi ya Mungu na jina Lake

Ingawa Yehova, Yesu, na Masihi yote yanawakilisha Roho Wangu, majina haya yanaashiria tu enzi tofauti katika mpango Wangu wa usimamizi, nayo hayaniwakilishi katika ukamilifu Wangu. Majina wanayoniita watu duniani hayawezi kueleza kwa ufasaha tabia Yangu nzima na yote Niliyo. Ni majina tofauti tu ambayo Ninaitwa katika enzi tofauti.

Jina la Mungu linaweza kubadilika, lakini asili Yake haitabadilika kamwe

Kuna wale ambao wanasema kuwa Mungu habadiliki. Hiyo ni sahihi, lakini inaashiria mabadiliko ya tabia ya Mungu na pia kiini chake. Mabadiliko ya jina lake na kazi hayathibitishi ya kuwa kiini chake kimebadilika; kwa maneno mengine, Mungu siku zote Atakuwa Mungu, na hii kamwe haitabadilika. Iwapo utasema kuwa kazi ya Mungu daima inabaki vile vile, basi Angekuwa na uwezo wa kumaliza mpango wake wa usimamizi wa miaka elfu sita?

Sura ya tatizo la mtu asiyejua umuhimu wa jina la Mungu na asiyelikubali jina jipya la Mungu ni ipi?

Katika kila kipindi cha wakati, Mungu ataanza kazi mpya, na katika kila kipindi, patakuwepo na mwanzo mpya kwa mwanadamu. Laiti mwanadamu ashikilie tu ukweli kwamba “Yehova ni Mungu” na “Yesu ni Kristo,” ambao ni ukweli unaozingatiwa katika enzi moja tu, basi mwanadamu hatawahi kwenda sambamba na kazi ya Roho Mtakatifu, na daima hataweza kupokea kazi ya Roho Mtakatifu. Bila kujali jinsi Mungu anavyofanya, mwanadamu anafaa kufuata bila shaka lolote, na afuate kwa ukaribu. Kwa jinsi hii basi itakuwaje mwanadamu aondolewe na Roho Mtakatifu? Bila kujali kile anachofanya Mungu, kama mwanadamu ana uhakika ni kazi ya Roho Mtakatifu, na kushirikiana katika kazi ya Roho Mtakatifu bila mashaka yoyote, na kujaribu kufikia mahitaji ya Mungu, basi ataadhibiwaje? Kazi ya Mungu kamwe haijasimama, hatua Zake hazijakwama na kabla kukamilisha kazi Yake ya usimamizi, siku zote Mungu amekuwa mwenye kazi nyingi, na kamwe hajasimama.

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp