Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 29

Mungu aliwaumba wanadamu; licha ya kama wamepotoka au kama wanamfuata Yeye, Mungu hushughulikia binadamu kama wapendwa Wake—au kama vile binadamu wangesema, watu walio wapenzi Wake sana—na wala si makaragosi Yake. Ingawaje Mungu anasema Yeye ndiye muumba na kwamba binadamu ni uumbaji Wake, hali ambayo inaweza kuonekana ni kana kwamba kuna tofauti kiasi katika mpangilio wa cheo, uhalisia ni kwamba kila kitu ambacho Mungu amefanya kwa mwanadamu kinazidi kabisa uhusiano wa asili hii. Mungu anampenda mwanadamu, anamtunza mwanadamu, na anaonyesha kwamba anamjali mwanadamu, pamoja na kumkimu mwanadamu bila kuacha na bila ya kusita. Kamwe hahisi katika moyo Wake kwamba hii ni kazi ya ziada au ni kitu kinachostahili sifa nyingi. Wala Hahisi kwamba kuokoa binadamu, kuwatosheleza, na kuwapatia kila kitu, ni kutoa mchango mkuu kwa binadamu. Anamkimu tu mwanadamu kimyakimya na kwa unyamavu, kwa njia Yake mwenyewe na kupitia kwa kiini Chake na kile Anacho na alicho. Haijalishi ni toleo kiasi kipi na ni msaada kiasi kipi ambao wanadamu wanapokea kutoka kwa Yeye, Mungu siku zote hajawahi kufikiri kuhusu au kujaribu kutaka sifa yoyote. Hii inaamuliwa na kiini cha Mungu, na pia hasa ni maonyesho ya kweli pia ya tabia ya Mungu. Na ndio maana, haijalishi kama iko kwa Biblia au kitabu chochote kingine, hatujawahi kumpata Mungu akionyesha fikira Zake, na hatujawahi kumpata Mungu akifafanua au akitangazia wanadamu ni kwa nini Anafanya mambo haya, au ni kwa nini Anamjali sana mwanadamu, ili kumfanya mwanadamu kumshukuru Yeye au kumsifu Yeye. Hata wakati Amejeruhiwa, wakati moyo Wake umo katika maumivu makali, Hajawahi kusahau jukumu Lake kwa mwanadamu au wasiwasi Wake kwa mwanadamu, huku haya yote yakiendelea, Anavumilia madhara na maumivu akiwa pekee katika ukimya. Kinyume cha mambo ni kwamba, Mungu anaendelea kumkimu mwanadamu kama Anavyofanya siku zote. Ingawaje mwanadamu mara nyingi humsifia Mungu au huwa na ushuhuda Kwake, hakuna kati ya tabia hii ambayo imedaiwa na Mungu. Hii ni kwa sababu Mungu hajawahi kunuia mambo yoyote mazuri Anayomfanyia binadamu yeye pia naye kumfanyia vivyo hivyo kama ishara ya shukrani au ili iweze kuonekana kwamba anafanyiwa mazuri aliyofanya. Kwa mkono mwingine, wale wanaomcha Mungu na kujiepusha na maovu, wale wanaomfuata Mungu kwa kweli, wanaomsikiliza Yeye, na walio waaminifu Kwake yeye, na wale wanaomtii Yeye—hawa ndio watu ambao mara nyingi watapokea baraka za Mungu, na Mungu atawakabidhi baraka hizo bila kusita. Isitoshe, baraka ambazo watu hupokea kutoka kwa Mungu mara nyingi zinazidi kufikiria kwao na pia zinazidi kitu chochote ambacho binadamu wanaweza kubadilishana na yale waliyofanya au gharama waliyolipia. Wakati mwanadamu anafurahia baraka za Mungu, Je, yupo yeyote anayejali ni nini Mungu anafanya? Je, yupo yeyote anayeonyesha wasiwasi wowote kuhusu vile ambavyo Mungu anahisi? Je, yupo yeyote anayethamini maumivu ya Mungu? Jibu la uhakika la maswali haya ni: La! Je, mwanadamu yeyote, akiwemo Nuhu, anaweza kuthamini yale maumivu ambayo Mungu alikuwa akihisi wakati huo? Je, mtu yeyote anaweza kufahamu ni kwa nini Mungu alianzisha agano kama hilo? Hakuna anayeweza! Mwanadamu hathamini maumivu ya Mungu si kwa sababu hawezi kuelewa maumivu ya Mungu, na si kwa sababu ya nafasi iliyopo kati ya Mungu na mwanadamu au tofauti kati ya hadhi yao; badala yake, ni kwa sababu mwanadamu hata hajali kuhusu hisia zozote za Mungu. Mwanadamu anafikiria Mungu yuko huru—Mungu hahitaji watu wa kujali kuhusu Yeye, kumwelewa au kumwonyesha namna anavyomfikiria. Mungu ni Mungu, hivyo Hana maumivu, hana hisia; Hatakasirika, Hahisi huzuni, hata Halii. Mungu ni Mungu, hivyo Hahitaji maonyesho yoyote ya kihisia na Hahitaji faraja yoyote ya kihisia. Kama Hahitaji mambo haya katika hali fulani, basi Atatatua mwenyewe na Hatahitaji usaidizi wowote kutoka kwa mwanadamu. Lakini kinyume chake ni kuwa, ni wale binadamu wanyonge, wanaohitaji tulizo, toshelezo, himizo la Mungu na hata pia kwake Yeye kuweza kutuliza hisia zao wakati wowote mahali popote. Fikira kama hiyo inajificha ndani kabisa ya mioyo ya mwanadamu: Binadamu ndiye mnyonge; wanahitaji Mungu ili awatunze kwa kila njia, wanastahili utunzaji wote wanaopokea kutoka kwa Mungu, na wanafaa kudai kutoka kwa Mungu chochote kile wanachohisi kinafaa kuwa ni chao. Mungu ndiye mwenye Nguvu; Anacho kila kitu, na Anahitaji kuwa mlezi wa mwanadamu na Anayetoa baraka. Kwa sababu Yeye tayari ni Mungu, Yeye Mwenyezi na Hahitaji katu chochote kutoka kwa mwanadamu.

Kwa vile binadamu hatilii maanani ufunuo wowote wa Mungu, hajawahi kuhisi huzuni, maumivu au furaha ya Mungu. Lakini kinyume chake ni kwamba, Mungu anajua maonyesho yote ya binadamu kama vile anavyojua sehemu ya kiganja cha mkono Wake. Mungu hutosheleza mahitaji ya kila mtu siku zote na pahali pote, akiangalia fikira zinazobadilika za kila mmoja na hivyo basi kuwatuliza na kuwahimiza, na kuwaongoza na kuwaangazia. Kuhusu mambo yote ambayo Mungu amemfanyia mwanadamu, na gharama zote Alizolipia kwa sababu yao, watu wanaweza kupata kifungu kutoka kwa Biblia au kutoka kwa chochote ambacho Mungu amesema mpaka sasa kinachoelezea waziwazi kwamba Mungu atadai kitu kutoka kwa binadamu? La! Kinyume cha mambo, haijalishi ni vipi watu wanapuuza kufikiria kwa Mungu, Bado Anawaongoza kwa marudio wanadamu, Anamkimu kwa kurudia mwanadamu na kumsaidia, kuwaruhusu kufuata njia za Mungu ili waweze kupokea hatima nzuri ambayo Amewatayarishia. Inapokuja kwa Mungu, kile Anacho na alicho, neema Yake, rehema Yake, na tuzo Zake zote, zitakabidhiwa bila ya kusita kwa wale wanaompenda na kumfuata Yeye. Lakini hajawahi kufichua kwa mtu yeyote maumivu aliyopitia Yeye au hali ya akili Yake, na katu halalamiki kuhusu yeyote ambaye hamtilii Yeye maanani au hajui mapenzi Yake. Anavumilia tu haya yote kimyakimya, akisubiria siku ambayo mwanadamu ataweza kuelewa.

Kwa nini Nasema mambo haya hapa? Ni nini mnachoona kutoka kwa mambo haya Niliyosema? Kuna kitu katika kiini na tabia ya Mungu ambacho ndicho rahisi zaidi kupuuza, kitu ambacho kinamilikiwa tu na Mungu na wala si mtu yeyote, wakiwemo wale wengine wanafikiria kwamba ni watu wakubwa, watu wazuri, au Mungu wa kufikiria kwao. Kitu hiki ni nini? Ni kule kutokuwa na nafsi kwa Mungu. Tunapozungumzia kutokuwa na nafsi, unaweza kufikiria kwamba pia wewe huna nafsi, kwa sababu inapokuja kwa watoto wako, haujadiliani juu ya bei na wao na wewe ni mkarimu sana kwao, au unafikiria kwamba wewe huna nafsi sana inapokuja kwa wazazi wako. Haijalishi ni nini unafikiria, angaa unayo dhana ya neno “kutokuwa na nafsi” na unalifikiria kama neno zuri, na kwamba kuwa mtu asiye na nafsi ni jambo la kipekee. Wakati huna nafsi, unafikiri kuwa wewe ni mkubwa. Lakini hakuna mtu anayeweza kuona kutokuwa na nafsi kwa Mungu miongoni mwa viumbe wote, miongoni mwa watu, hafla, na vitu, na kupitia kazi ya Mungu. Kwa nini hali iko hivi? Kwa sababu binadamu ni mchoyo sana! Kwa nini Ninasema hivyo? Mwanadamu anaishi katika ulimwengu wa uyakinifu. Unaweza kumfuata Mungu, lakini huoni wala kushukuru namna ambavyo Mungu anakukimu, anavyokupenda na anavyoonyesha kwamba anakujali. Kwa hivyo unaona nini? Unaona watu wako wa ukoo wanaokupenda au kukupenda sana. Unayaona mambo ambayo ni ya manufaa kwa mwili wako, unajali kuhusu watu na vitu unavyopenda. Huku ndiko kutokuwa na nafsi kwa binadamu kunakodaiwa. Watu kama hao “wasiokuwa na nafsi” hata hivyo, huwa hawajali katu kuhusu Mungu anayewapa maisha. Kinyume na Mungu, kutokuwa na nafsi kwa binadamu kunakuwa cha nafsi na yenye uchoyo. Kutokuwa na nafsi ambako binadamu anasadiki katika ni ulio mtupu na usio halisi, uliotiwa madoa, usiolingana na Mungu, na usiohusika na Mungu. Kutokuwa na nafsi kwa binadamu ni kwa ajili yake, huku kutokuwa na nafsi kwa Mungu ni ufunuo wa kweli wa kiini Chake. Ndipo hasa kutokana na kujitolea nafsi kwa Mungu ndipo binadamu anapokea mfululizo usiosita wa ujazo kutoka kwake. Huenda msiathirike sana na mada hii Ninayozungumza kuhusu leo na unaweza kuwa tu unatikisa kichwa chako kwa kukubaliana nami, lakini wakati unapojaribu kufurahia moyo wa Mungu katika moyo wako, utaweza kwa kutojua kugundua: Miongoni mwa watu wote, masuala, na mambo unaweza kuhisi katika ulimwengu huu ni kutokuwa na nafsi tu kwa Mungu ambako ni kweli na dhabiti, kwa sababu ni upendo wa Mungu tu kwako ndio ambao hauna masharti na hauna madoa. Mbali na Mungu, kutokuwa na kile kinachodaiwa kutokuwa na nafsi wa mtu mwingine ni bandia, cha juujuu, kisicho na msingi; kina kusudio, nia fulani, kinatekeleza shughuli ya masikilizano, na hakiwezi kupimwa kamwe. Mnaweza hata kusema kwamba ni ki chafu, na cha kudharauliwa. Je, mnakubali?

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp