Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Hatua Tatu za Kazi | Dondoo 18

Kazi ambayo Yehova Alifanya kwa Waisraeli ilianzishwa miongoni mwa binadamu mahali pa asili pa Mungu hapa ulimwenguni, pahali patakatifu ambapo Alikuwepo. Hii kazi Aliiwekea mipaka miongoni mwa watu wa Israeli tu. Kwanza, hakufanya kazi nje ya Israeli; badala yake, Alichagua watu Alioona kwamba walifaa ili kuwawekea mipaka upana wa kazi Yake. Israeli ndipo mahali ambapo Mungu Aliwaumba Adamu na Hawa, na kutoka kwenye vumbi la mahali hapo, Yehova Alimwumba mwanadamu; ndio msingi wa kazi Yake ya hapo ulimwenguni. Waisraeli, ambao ni kizazi cha Nuhu na Adamu, ndio waliokuwa msingi wa kazi ya Yehova ulimwenguni.

Umuhimu, kusudio, na hatua ya kazi ya Yehova nchini Israeli vyote vilikuwa vya kuanzisha kazi Yake katika ulimwengu mzima, na taratibu kuieneza kwenye nchi za Mataifa kutoka kwenye kitovu chake cha Israeli. Hii ndiyo kanuni ambayo Alitumia katika kufanya kazi kotekote ulimwenguni—kuanzisha mfano, kisha kuupanua mpaka watu wote ulimwenguni waweze kukubali injili Yake. Waisraeli wa kwanza walikuwa kizazi cha Nuhu. Watu hao walikuwa tu na pumzi za Yehova, na waliweza kujitunza wakatilia maanani mahitaji ya kimsingi ya maisha, lakini hawakujua Yehova Alikuwa Mungu aina gani, wala hawakujua mapenzi Yake kwa binadamu, na hata namna ambavyo walitakikana kumstahi Bwana wa viumbe vyote. Na kuhusu iwapo kulikuwa na amri na sheria za kutiiwa, na kama kulikuwa na kazi ambayo viumbe walioumbwa wanapaswa kumfanyia Muumba: Ukoo wa Adamu haukujua chochote kuhusu mambo haya. Kile walichojua tu kilikuwa kwamba mume lazima atoke jasho na atie bidii ili kutosheleza familia yake, na kwamba mke lazima amtii mume wake na kuendeleza kizazi cha binadamu ambacho Yehova Aliumba. Kwa maneno mengine, watu hawa walikuwa tu na pumzi za Yehova na maisha Yake, lakini hawakujua namna ya kufuata sheria za Mungu au namna ya kumtosheleza Bwana wa viumbe vyote. Walielewa kidogo sana. Kwa hivyo ingawaje hakukuweko na chochote kisichostahili au chenye ujanja katika mioyo yao, na ingawaje ilikuwa nadra sana kwao kuwa na wivu au hata ugomvi, hawakumjua wala kumwelewa Yehova, Bwana wa viumbe vyote. Vizazi hivi vya binadamu vilijua tu kula kile ambacho Yehova Alikuwa Ameunda, kufurahia kile ambacho Yehova Alikuwa ameunda, lakini hawakujua kumstahi Yehova; hawakujua kwamba Yehova ndiye walipaswa kumwabudu huku wakiwa wamepiga magoti. Wangeitwaje viumbe Wake? Kama hali ingekuwa hivyo, je, maneno “Yehova ni Bwana wa viumbe vyote” na “Alimwumba binadamu ili mwanadamu aweze kumridhisha, kumtukuza na kumwakilisha”—je, hayangekuwa yamesemwa bure bilashi? Watu wasiomstahi Yehova wangewezaje kuwa ushuhuda kwa utukufu Wake? Wangewezaje kuwa dhihirisho la utukufu Wake? Je, maneno ya Yehova “Nilimwumba binadamu kwa mfano Wangu” yakawa silaha kwenye mikono ya Shetani—yule mwovu? Je, haya Maneno hayangekuwa basi alama ya udhalilishaji kwa uumbaji wa binadamu na Yehova? Ili kukamilisha awamu hiyo ya kazi, Yehova, baada ya kumwumba mwanadamu, hakumwelekeza wala kumwongoza kuanzia kwa Adamu hadi Nuhu. Haukuwa mpaka wakati wa mafuriko ndipo Alianza rasmi kuwaongoza Waisraeli waliokuwa vizazi vya Adamu na Nuhu. Kazi na maneno Yake nchini Israeli vyote viliongoza watu wote wa Israeli walipokuwa wakiishi maisha yao kotekote nchini Israeli, na kwa njia hii kuonyesha binadamu kwamba Yehova hakuweza tu kutia pumzi ndani ya binadamu, ili apate maisha kutoka Kwake, na ainuke kutoka kwenye vumbi na kuwa mwanadamu aliyeumbwa, lakini pia aliweza kumteketeza mwanadamu kwa moto, na kumlaani mwanadamu kwa kutumia kiboko Chake ili kumtawala mwanadamu. Kwa hivyo, wao pia, waliweza kuona kwamba Yehova angeweza kuyaongoza maisha ya binadamu ulimwenguni na kuongea na kufanya kazi miongoni mwao kulingana na saa za mchana na za usiku. Alifanya tu kazi hiyo ili viumbe Vyake viweze kujua kwamba binadamu alitoka kwenye vumbi na akachukuliwa na Yeye, kwamba binadamu aliumbwa na Yeye. Aidha, kazi Aliyoianza Israeli ilikuwepo ili watu wengine na mataifa mengine (ambao kwa hakika hawakuwa kando na wale wa Israeli, lakini walikuwa wamejitenga na wana wa Israeli, ilhali bado walikuwa kizazi cha Adamu na Hawa) waweze kupokea injili ya Yehova kutoka Israeli, ili viumbe vyote ulimwenguni vingemstahi na kumchukulia kuwa mkuu. Kama Yehova Asingekuwa Ameanza kazi yake Israeli, lakini badala yake baada ya kumwumba mwanadamu, na kumwacha kuishi vivyo hivyo tu hapa ulimwenguni, basi kwa sababu ya asili ya kimaumbile ya binadamu (asili inamaanisha kwamba binadamu hawezi kujua yale mambo ambayo hayaoni, yaani, hajui kwamba Yehova Alimwumba mwanadamu, na vilevile hata hajui kwa nini Alifanya hivyo), asingewahi kujua kwamba Yehova Alimwumba mwanadamu na kwamba ndiye Bwana wa mambo yote. Kama Yehova Angemwumba mwanadamu na kumweka ulimwenguni kwa raha Zake, kisha kuikung’uta tu mikono Yake na kuondoka badala ya kumwongoza miongoni mwa wenzake kwa kipindi cha muda, basi kizazi chote cha binadamu kingerudi katika hali ya kutokuwa na maana; hata mbingu na ardhi na vitu vyote vilivyoumbwa na Yeye, wakiwemo binadamu wote, vingerudi na kuwa katika hali isiyokuwa na maana na kutupiliwa mbali na kukanyagwa na Shetani. Na kwa hivyo, mapenzi ya Yehova kwamba “Ulimwenguni, yaani, miongoni mwa viumbe Vyake, Anafaa kuwa na mahali pa kusimama, mahali patakatifu” yasingetimia. Kwa hiyo badala yake, baada ya Mungu kuumba wanadamu Aliwaongoza katika maisha yao na kuwazungumzia, wote ili waweze kutambua matamanio yake, kufikia mpango Wake. Kazi ya Mungu nchini Israeli ilinuiwa kutekeleza kazi Aliyokuwa Ameiweka wazi mbele ya viumbe Vyake vyote, na kwa hivyo Yeye kufanya kazi kwanza miongoni mwa Waisraeli na viumbe Wake kati ya vitu vyote havikuwa katika mgongano, lakini vyote hivi vilikuwa kwa minajili ya usimamizi Wake, kazi Yake na utukufu Wake, na kuzidisha maana ya kuumba Kwake wanadamu. Aliyaongoza maisha ya wanadamu ulimwenguni kwa miaka elfu mbili baada ya Nuhu ambapo Aliwafunza namna ya kumstahi Yehova Bwana wa vitu vyote, Akawafunza namna ya kujiendeleza na kuisha maisha yao, na muhimu kuliko vyote, namna ya kuwa shahidi wa Yehova, kumtii Yeye na kumstahi Yeye, na kumsifu Yeye kwa muziki kama Daudi na kuhani wake walivyofanya.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp