Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kupata Mwili | Dondoo 137

Wakati Mungu Anakuja duniani, Yeye Anafanya tu kazi ya Uungu. Hili ni agizo la Roho wa mbinguni kwa Mungu mwenye mwili. Yeye Anakuja tu kwenda kila mahali na kuzungumza, kupaza sauti Yake kwa njia tofauti na kutoka kwa mitazamo tofauti. Yeye kimsingi Anachukulia kumruzuku mwanadamu na kumfundisha mwanadamu kama malengo Yake na kanuni Zake za kazi. Yeye hajihusishi na vitu kama uhusiano kati ya wanadamu au maelezo ya maisha ya wanadamu. Huduma Yake kuu ni kuzungumza kwa niaba ya Roho. Wakati Roho wa Mungu Anaonekana katika mwili kwa hali iliyo wazi, Yeye hukimu kwa ajili ya uzima wa mwanadamu na kuuweka wazi ukweli. Yeye hajihusishi katika kazi ya mwanadamu, yaani, Yeye hashiriki katika kazi ya ubinadamu. Binadamu hawezi kufanya kazi ya Mungu, na Mungu hashiriki katika kazi za binadamu. Katika miaka yote ya Mungu kufanya kazi katika dunia hii, Yeye daima Ametumia wanadamu kufanya kazi Yake. Lakini wanadamu hawa hawawezi kuchukuliwa kama Mungu mwenye mwili; wao wanaweza tu kuchukuliwa kama wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Lakini Mungu wa leo Anaweza kuzungumza moja kwa moja kutoka katika mtazamo wa Uungu, Apeleke sauti ya Roho, na kufanya kazi kwa niaba ya Roho. Wanadamu wote ambao Mungu Ametumia katika enzi nyingi huonekana kuwa Roho wa Mungu Anafanya kazi kupitia miili yao, hivyo basi kwa nini hawawezi kuitwa Mungu? Mungu wa leo ni Roho wa Mungu Anayefanya kazi moja kwa moja katika mwili, na Yesu pia Alikuwa Roho wa Mungu Aliyefanya kazi katika mwili. Hawa wawili wa mwisho wanaitwa Mungu. Basi tofauti ni nini? Tangu mwanzo, wanadamu ambao Mungu Ametumia wote wana mawazo ya kawaida na fikra. Wao wote wanajua jinsi ya kujiendesha na kushughulikia mambo ya maisha. Wanashikilia itikadi za kawaida za binadamu na kuwa na vitu vyote ambavyo wanadamu wa kawaida wanapaswa kuwa navyo. Wengi wao wana vipaji vya pekee na werevu wa kiasili. Kwa kufanya kazi kupitia wanadamu hawa, Roho wa Mungu Anakusanya na kutumia vipaji vyao, ambavyo ni zawadi yao Aliyowapa Mungu. Ni Roho wa Mungu Ndiye Anayeleta vipaji vyao katika kazi, na kuwasababisha kutumia uwezo wao kumhudumia Mungu. Hata hivyo, kiini cha Mungu hakina itikadi na hakina fikira. Hakiungani na mawazo ya binadamu na hata kinakosa vitu ambavyo binadamu wa kawaida huwa navyo. Yaani, Mungu hata hafahamu vizuri kanuni za maadili ya binadamu. Hivi ndivyo ilivyo Mungu wa leo Anapokuja duniani. Kazi Yake na maneno Yake hayajachafuliwa na nia au fikira za binadamu, bali ni dhihirisho la moja kwa moja la Roho, na Anafanya kazi moja kwa moja kwa niaba ya Mungu. Hii ina maana Roho huja kufanya kazi, ambayo Haweki ndani mawazo ya mwanadamu hata kidogo. Yaani, Mungu katika mwili Anajumuisha Uungu moja kwa moja, Hana mawazo ya binadamu au itikadi, na Haelewi kanuni za maadili ya binadamu. Kama kungekuwa na kazi ya Uungu tu (kumaanisha iwapo ingekuwa Mungu mwenyewe pekee ndiye Anayefanya kazi hiyo), kazi ya Mungu haingeweza kufanyika duniani. Kwa hivyo Mungu Anapokuja duniani, lazima Awe na wanadamu wachache Anaowatumia kufanya kazi katika ubinadamu pamoja na kazi Yake katika Uungu. Kwa maneno mengine, Yeye Anatumia kazi ya mwanadamu ili kusaidia kazi Yake takatifu. La sivyo, mwanadamu hangeweza kuja katika mawasiliano ya moja kwa moja na kazi ya Mungu. Hivi ndivyo ilivyokuwa baina ya Yesu na wanafunzi wake. Wakati wa maisha Yake duniani Yesu alipiga marufuku sheria za zamani na kuanzisha amri mpya. Pia alizungumza mengi. Yote haya yalifanyika katika Uungu. Wafuasi Wake, kama vile Petro, Paulo, na Yohana, wote waliweka kazi yao ya baadaye juu ya maneno ya Yesu kama msingi wake. Yaani, Mungu Alikuwa Akifanya kazi ya uzinduzi katika enzi hiyo, Akiialika Enzi ya Neema. Alileta enzi mpya, Akaiondoa ile ya zamani, na Alifanya maneno haya “Mungu ni Mwanzo na Mwisho” kutimika. Kwa maneno mengine, mwanadamu lazima afanye kazi ya mwanadamu juu ya msingi wa kazi ya Mungu. Yesu alipomaliza kusema yote Aliyohitajika kusema na kumaliza kazi Yake hapa duniani, alitoka katika mwanadamu. Na wanadamu baada Yake walifanya kazi kwa mujibu wa kanuni katika maneno Yake na kutenda kwa mujibu wa ukweli Alioongea. Hawa wote walikuwa watu waliomfanyia Yesu kazi. Kama ingekuwa ni Yesu pekee Yake anafanya kazi, haijalishi kiasi gani Yeye Angezungumza, bado wanadamu hawangeweza kuwa na uhusiano na neno Lake, kwa sababu Yeye Alifanya kazi katika Uungu na usemi Wake ulikuwa wa Uungu peke yake. Ilikuwa vigumu Kwake kueleza mambo kwa namna ambayo wanadamu wa kawaida wangeweza kuelewa neno Lake. Hivyo basi ilimpasa kuwa na mitume na manabii waliokuja kabla Yake kuongezea kazi Yake. Hii ni kanuni ya jinsi Mungu mwenye mwili Hufanya kazi—kwa kutumia mwili kusema na kutenda ili kukamilisha kazi ya Uungu, na kisha kwa kutumia wanadamu wachache au zaidi wanaopendeza moyo wa Mungu ili kujaliza kazi ya Mungu. Yaani, Mungu Anatumia wanadamu wanaopendeza moyo Wake kuongoza na kunyunyiza ubinadamu ili kila mwanadamu aweze kupokea ukweli.

Kama Mungu Anakuja tu katika mwili na anafanya kazi ya Uungu bila kuwa na wanadamu wachache wa ziada wanaopendeza moyo Wake kushirikiana na Yeye, basi mwanadamu hatakuwa na uwezo wa kuelewa mapenzi ya Mungu na hataweza kuwa katika mawasiliano na Mungu. Mungu Anatumia wanadamu wa kawaida wanaopendeza moyo Wake ili kukamilisha kazi hii, kutunza na kuchunga makanisa, ili kwamba fikra za mwanadamu na ubongo wake uweze kufikiria kazi ya Mungu. Kwa maneno mengine, Mungu anatumia wanadamu wachache wanaopendeza moyo wake “kutafsiri” kazi Yake katika Uungu, kuifichua, yaani, kubadilisha lugha ya Mungu kuwa lugha ya binadamu, hivyo kwamba wanadamu wote waweze kuielewa lugha Yake. Kama Mungu hangefanya hivyo, hakuna mwanadamu angeweza kuelewa lugha ya Mwenyezi Mungu, kwa sababu idadi ya wanadamu walio na moyo unaompendeza Mungu, ni wachache mno, na uwezo wa mwanadamu kufahamu ni dhaifu. Hiyo ndiyo maana Mungu Hutumia njia hii wakati wa kufanya kazi katika mwili. Kama kungekuwa na kazi ya Uungu peke yake, mwanadamu hangeweza kujua au kuwa katika mawasiliano na Mungu kwa sababu mwanadamu haelewi lugha ya Mungu. Mwanadamu anaweza kuelewa lugha hii tu kupitia kwa wanadamu wanaopendeza moyo wa Mungu kufafanua maneno Yake. Hata hivyo, kama kungekuwa na wanadamu kama hao pekee wakifanya kazi katika ubinadamu, ingeweza tu kudumisha maisha ya kawaida ya mwanadamu; isingekuwa na uwezo wa kubadilisha tabia ya mwanadamu. Kazi ya Mungu haingeweza kuwa na mwanzo mpya; kungekuwa tu na nyimbo zile za zamani, na maelezo yale ya zamani. Ni kupitia kwa Mungu Aliye katika mwili Akisema yote aliyohitaji kusema na kufanya yote ambayo yanafaa kufanyika katika hali ya mwili, na wanadamu wanaofanana na Yeye kufanya kazi na kuishi kulingana na maneno Yake, ndipo tabia ya maisha yao inaweza kubadilika na waweze kusonga na nyakati. Yeye ambaye Anafanya kazi katika Uungu Anawakilisha Mungu, ilhali wale wanaofanya kazi katika ubinadamu ni wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Yaani, Mungu katika mwili ana utofauti halisi na wanadamu wanaotumiwa na Mungu. Mungu mwenye mwili Anaweza kufanya kazi ya Uungu, lakini wanadamu wanaotumiwa na Mungu hawawezi. Mwanzoni mwa kila enzi, Roho wa Mungu anaongea binafsi kuzindua enzi mpya na kuleta mwanadamu kwenye mwanzo mpya. Wakati Yeye Atamaliza mazungumzo Yake, itaashiria kwamba kazi ya Mungu katika Uungu imekamilika. Baada ya hapo, wanadamu wote hufuata mwongozo wa wale hutumiwa na Mungu kuingia katika uzoefu wa maisha. Vile vile, katika hatua hii Mungu huleta mwanadamu katika enzi mpya na Anampa kila mwanadamu mwanzo mpya. Na hivyo, kazi ya Mungu katika mwili inahitimishwa.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Tofauti Muhimu Kati ya Mungu Mwenye Mwili na Watu Wanaotumiwa na Mungu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp