Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 401

Katika Enzi ya Ufalme wa Milenia, iwapo umeingia katika enzi hii mpya inaamuliwa na kama umeingia kwenye uhalisia wa maneno ya Mungu na kama maneno Yake yanakuwa uhalisia katika maisha yako. Neno la Mungu linajuzwa kwa wote, ili hatimaye, binadamu wote waweze kuishi katika ulimwengu wa neno na neno la Mungu litawapa nuru na kuangaza kila mtu kotekote. Kama katika kipindi hiki cha muda, una haraka na uzembe katika kusoma neno la Mungu, na huna kivutio katika neno Lake, yaonyesha kwamba kuna jambo baya na hali yako. Kama huwezi kuingia katika Enzi ya Neno, basi Roho Mtakatifu Hafanyi kazi ndani yako; kama umeingia katika enzi hii, Atafanya kazi Yake. Ni nini unachoweza kufanya kwa sasa, mwanzo wa Enzi hii ya Neno, ili kupata kazi ya Roho Mtakatifu? Katika enzi hii, Mungu atafanya jambo la uhalisia miongoni mwenu ili kwamba kila binadamu aweze kuishi kwa kudhihirisha neno la Mungu, aweze kutia ukweli katika matendo, na kumpenda Mungu kwa dhati; kwamba binadamu wote waweze kutumia neno la Mungu kama msingi na uhalisia wao na kuwa na mioyo ya kumcha Mungu; na kwamba, kupitia kwa kutenda neno la Mungu, binadamu basi anaweza kutawala pamoja na Mungu. Hii ndiyo kazi ambayo Mungu atatimiza. Unaweza kuendelea na maisha bila ya kusoma neno la Mungu? Kuna wengi sasa wanaohisi kwamba hawawezi kukaa hata siku moja au mbili bila ya kusoma neno la Mungu. Lazima wasome neno Lake kila siku, na kama muda hauruhusu, kusikiliza neno Lake kunatosha. Hii ndiyo hisia ambayo Roho Mtakatifu anampa binadamu na namna ambavyo Anaanza kumbadilisha binadamu. Yaani, Hutawala binadamu kupitia kwa maneno ili binadamu aweze kuingia katika uhalisia wa neno la Mungu. Kama unahisi giza na kiu baada ya kula na kunywa neno la Mungu, na unapata kwamba hali hiyo haikubaliki, hii inamaanisha kwamba umeguswa na Roho Mtakatifu, na Hajakugeukia. Basi wewe ndiye mmoja aliye katika mkondo huu. Hata hivyo, kama huna utambuzi au huhisi kiu baada ya siku moja au mbili za kukosa kula na kunywa neno la Mungu, na huhisi kwamba umeguswa, hii inaonyesha kwamba Roho Mtakatifu amekugeukia. Hii inamaanisha, basi, kuwa hali iliyo ndani yako si sahihi; bado hujaingia katika Enzi ya Neno, na wewe ni mmoja aliyebaki nyuma. Mungu hutumia neno ili kumtawala binadamu; unahisi vyema kama utakula na kunywa neno la Mungu, na kama huhisi hivyo, hutakuwa na njia yoyote ya kufuata. Neno la Mungu linakuwa chakula cha binadamu na nguvu zinazomwendesha. Biblia inasema kwamba “Mwanadamu hatadumu kwa mkate pekee, lakini kwa kila neno linalotoka kinywani mwa Mungu.” Hii ndiyo kazi ambayo Mungu ataikamilisha leo. Atafanikisha ukweli huu ndani yenu. Ikoje kwamba binadamu katika siku za kale angekaa siku nyingi bila ya kusoma neno la Mungu lakini angeendelea kula na kufanya kazi? Na kwa nini hali sivyo hivi sasa? Katika enzi hii, Mungu hutumia kimsingi neno ili kutawala yote. Kupitia kwa neno la Mungu, binadamu anahukumiwa na kufanywa mtimilifu, kisha hatimaye kupelekwa katika ufalme. Ni neno la Mungu tu linaloweza kuruzuku maisha ya binadamu, na ni neno la Mungu tu ndilo linaloweza kumpa binadamu nuru na njia ya kutenda, hasa katika Enzi ya Ufalme. Mradi tu kila siku unakula na kunywa neno Lake na huachi uhalisia wa neno la Mungu, Mungu ataweza kukufanya mtimilifu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

In the Age of Kingdom God Perfects Man by Words

I

In this age, God’ll realize this among you: that all practice His truth, that all live out His word and love Him with their hearts. God’s word is the base of their life. They all have hearts that fear God. Through practicing God’s words, they’ll rule and reign with God. Only God’s word provides man with life. Only His word can bring man light, pointing out the way of practice. This is more true in the Age of Kingdom.

II

God’s words, they govern man. God’s word is food and might. Feel good when you eat it. Eat not and you’ll find no way to go. In the Bible, it says: Man shall not live by just bread, but by the words from God’s mouth. Now God will realize this in you. Only God’s word provides man with life. Only His word can bring man light, pointing out the way of practice. This is more true in the Age of Kingdom.

III

Before, man went for days without reading God’s words; they worked and lived their lives. But things have changed today, for God governs all by word. People are judged and perfected, able to enter His kingdom, all because of His word. Only God’s word provides man with life. Only His word can bring man light, pointing out the way of practice. This is more true in the Age of Kingdom. Daily drink God’s word. Daily eat God’s word. Don’t leave the truth in it. And you will be made perfect.

from Follow the Lamb and Sing New Songs

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp