Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 434

Ikiwa watu wanataka kumjua Mungu, ni sharti kwanza wajue kuwa Mungu ni Mungu halisi, na ni sharti wajue maneno ya Mungu, kuonekena halisi kwa Mungu katika mwili, kazi halisi ya Mungu. Ni baada tu ya kujua kwamba kazi ya Mungu ni halisi ndiyo utaweza kweli kushirikiana na Mungu, na ni kupitia kwa njia hii tu ndipo utaweza kutimiza ukuaji wa maisha yako. Wale wote wasiokuwa na ufahamu wa uhalisi hawana namna ya kuyapitia maneno ya Mungu, wametekwa katika dhana zao, wanaishi katika mawazo yao, na hivyo hawana ufahamu wa maneno ya Mungu. Kadiri ufahamu wako kuhusu uhalisi ulivyo mkubwa, ndivyo unakuwa karibu zaidi na Mungu, na ndivyo unakuwa rafiki Yake wa karibu zaidi; jinsi unavyotafuta zaidi kutokuwa yakini na udhahania, na mafundisho ya kidini, ndivyo unavyojitenga zaidi na Mungu, na ndivyo utakavyohisi zaidi kuwa kuyapitia maneno ya Mungu ni kazi na ni kugumu, na kwamba huna uwezo wa kuingia. Ikiwa unataka kuingia katika uhalisi wa maneno ya Mungu, na katika njia sahihi ya maisha yako ya kiroho, ni sharti kwanza ujue uhalisi na ujitenge na vitu visivyo yakini na vya miujiza—ambako ni kumaanisha kuwa, kwanza ni sharti uelewe jinsi Roho Mtakatifu anapeana nuru na kukuongoza kutoka ndani. Kwa njia hii, ikiwa kwa kweli unaweza kuielewa kazi ya Roho Mtakatifu ndani yako, utakuwa umeingia katika njia sahihi ya kufanywa mkamilifu na Mungu.

Leo, kila kitu kinaanza kwa uhalisi. Kazi ya Mungu ndiyo halisi zaidi, na inaweza kuguswa na watu; ndicho kitu kinachoweza kupitiwa na wanadamu, na kufanikisha. Ndani ya watu mna mengi ambayo si yakini na ya miujiza, ambayo yanawazuia kuijua kazi ya sasa ya Mungu. Hivyo katika mazoea yao mara zote hupotoka na kuhisi vigumu, ambayo yote yanasababishwa na dhana zao. Watu wanashindwa kuelewa kanuni za kazi ya Roho Mtakatifu, hawajui uhalisi, na kwa hivyo daima njia zao za kuingia ni hasi. Wanatazama mahitaji ya Mungu kwa mbali, bila kuweza kuyatimiza; wanaona tu kwamba maneno ya Mungu kwa hakika ni mazuri, ila hawawezi kupata njia ya kuingilia. Roho Mtakatifu anafanya kazi kwa kanuni hii: kupitia ushirikiano na watu, kupitia kwa wao kuomba kimatendo, kumtafuta na kusonga karibu na Mungu, matokeo yanaweza kupatikana na wanaweza kupata nuru na kuangaziwa na Roho Mtakatifu. Si kwamba Roho Mtakatifu anafanya kazi kivyake, au mwanadamu anafanya kazi kivyake. Wote ni wa muhimu, na jinsi wanadamu wanavyoshiriki zaidi na jinsi wanavyotaka zaidi kufikia viwango vya mahitaji ya Mungu, ndivyo kazi ya Roho Mtakatifu inaimarika. Ni ushirikiano halisi tu wa wanadamu, kupitia kazi ya Roho Mtakatifu, ndivyo vinaweza kutoa matukio halisi na ufahamu wa kweli wa kazi ya Mungu. Hatua kwa hatua, kupitia kwa mazoea kwa njia hii, mwanadamu mkamilifu hatimaye huzalishwa. Mungu hafanyi vitu vya miujiza; katika dhana za mwanadamu, Mungu ni mwenye uweza, na kila kitu kinafanywa na Mungu—na hutokea kwamba watu wanasubiri tu bila kufanya chochote, hawasomi maneno ya Mungu au kuomba, na wanasubiri tu kuguswa na Roho Mtakatifu. Walio na ufahamu sahihi, hata hivyo, wanaamini hili: matendo ya Mungu yanaweza kufikia pale ambapo ushirikiano wangu umefikia, na athari ya kazi ya Mungu kwangu inategemea namna ninavyoshirikiana. Mungu anenapo, ninapaswa kufanya lolote niwezalo na kuyaelekea maneno ya Mungu; hili ndilo ninapaswa kufanikisha.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Jinsi ya Kujua Uhalisi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp