Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 456

Kuanzia leo, Mungu ataweza kuwafanya watu wasiokuwa na fikira za kidini kuwa watimilifu kwa njia rasmi, ambao wako tayari kuweka pembeni nafsi zao za kale, na ambao wanamtii tu Mungu, pamoja na kuwafanya kuwa watimilifu wale wanaotamani neno la Mungu. Watu hawa wanafaa kusimama na kumhudumia Mungu. Kwake Mungu kunayo na hekima nyingi na isiyoisha. Kazi yake ya kustaajabisha na matamshi yake yenye thamani ni vitu ambavyo vipo ili watu wengi zaidi kuweza kufurahia. Kama ilivyo sasa, vitu hivi vipya haviwezi kukubaliwa na wale walio na fikira za kidini, wanaochukua hali ya ukubwa, na wale ambao hawaweki pembeni nafsi zao za kale. Roho Mtakatifu hana fursa ya kuwafanya watu kama hao kuwa watimilifu. Kama mtu hana hamu ya kutii, na hana kiu cha neno la Mungu, basi mtu huyo hataweza kupokea mambo mapya. Wataendelea tu kuasi zaidi na zaidi, kuwa wajanja zaidi na zaidi, na hatimaye kujipata kwenye njia mbaya. Katika kazi ya Mungu ya sasa, Atawainua watu zaidi wanaompenda Yeye kwa kweli na wanaoweza kukubali mwangaza mpya. Na Atakatiza kabisa maafisa wa kidini wanaoonyesha ukubwa wao. Hataki mtu hata mmoja anayekataa mabadiliko. Je, unataka kuwa mmoja wa watu hao? Je, unatekeleza huduma yako kulingana na mapendeleo yako, au unafanya kile Mungu anachotaka? Hili ni jambo ambalo lazima ujijulie mwenyewe. Je, wewe ni mmojawapo wa maafisa wa kidini, au wewe ni mtoto mchanga aliyezaliwa na anayefanywa kuwa mtimilifu na Mungu? Je, ni kiwango kipi cha huduma yako ambacho kinapongezwa na Roho Mtakatifu? Kati ya kiwango hiki ni kipi ambacho Mungu hatakumbuka? Baada ya miaka mingi ya huduma, umeleta mabadiliko kiasi kipi katika maisha yako? Je, uko wazi kuhusu mambo haya yote? Kama unayo imani ya kweli, basi utaweka pembeni fikira zako za kale za kidini na utahudumia Mungu kwa njia bora zaidi na kwa njia mpya. Kama utajitahidi zaidi sasa, hujachelewa sana. Fikira za kale za kidini zitamnyima mtu maisha mazuri. Uzoefu ambao anapata utamwongoza mbali na Mungu, kufanya mambo kwa njia yake mwenyewe. Kama hutatupilia mbali vitu hivi, vitakuwa kikwazo katika kukua kwa maisha yako. Mungu siku zote amewafanya wote wanaomhudumia Yeye kuwa watimilifu. Hawatupilii mbali vivihivi tu. Kutakuwa na mustakabali kwako kama tu utakubali kwa kweli hukumu na vilevile kuadibiwa kwa neno la Mungu, kama unaweza kuweka pembeni matendo na mafundisho ya kidini yako ya kale ya kidini, na kuepuka kutumia fikira za kale za kidini kama kipimo cha neno la Mungu hii leo. Lakini kama utashikilia vitu vya kale, kama bado unavithamini, basi huwezi kupata wokovu. Mungu hatawatambua watu kama hao. Kama kweli unataka kufanywa kuwa mtimilifu, basi lazima uamue kutupilia mbali kabisa kila kitu cha kale. Hata kama kile kilichokuwa kimefanywa awali kilikuwa sahihi, hata kama ilikuwa ni kazi ya Mungu, utaiweka pembeni; hufai kuishikilia. Hata kama ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu iliyo wazi, iliyofanywa moja kwa moja na Roho Mtakatifu, leo lazima uiweke pembeni. Hufai kuishikilia. Hivi ndivyo Mungu anavyotuamuru. Kila kitu lazima kipate upya wake. Katika kazi ya Mungu na neno la Mungu, Mungu harejelei vitu vya kale ambavyo vilishapita, na vilevile hafukui historia ya kale. Mungu siku zote ni mpya na hajawahi kuwa mzee. Hashikilii hata maneno Yake mwenyewe aliyoyasema kale. Hii inaonyesha kwamba Mungu hafuati mafundisho ya dini yoyote. Katika hali hii, kama mwanadamu, kama siku zote unashikilia kabisa vitu vya kale na kuvitumia vivyohivyo fomula huku naye Mungu hafanyi kazi tena katika njia Alizokuwa akifanya awali, basi maneno yako na matendo yako hayakatizi? Je, hujawa adui wa Mungu? Je, uko radhi kuyaharibu maisha yako yote kwa sababu ya mambo haya ya kale? Mambo haya ya kale yanakufanya kuwa mtu anayezuia kazi ya Mungu. Je, mtu kama huyu ndiye wewe unataka kuwa? Kama kweli hutaki kuwa hivyo, basi acha mara moja kile unachofanya na ubadilike; anza tena upya. Mungu hakumbuki huduma yako ya kale.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Njia ya Huduma ya Kidini Lazima Ipigwe Marufuku

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp