Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 476

Petro alikuwa mtu aliyefanywa mkamilifu. Ni baada tu ya kupitia kuadibu na hukumu, na hivyo kupata upendo safi wa Mungu, ndipo alifanywa mkamilifu kabisa; njia ambayo alipitia ilikuwa ni njia ya kukamilishwa. Ambayo ni kusema kuwa, tangu hapo mwanzo kabisa, njia ambayo Petro alipitia ilikuwa ya haki, na motisha ya kumwamini Mungu ilikuwa sahihi, na kwa hivyo akawa mtu aliyekuwa amefanywa kamili. Yeye alifuata njia mpya ambayo mwanadamu kamwe hajawahi kuitembelea hapo awali, ilhali njia ambayo Paulo alitembea tangu mwanzo ilikuwa njia ya upinzani kwa Kristo, na ni kwa sababu tu Roho Mtakatifu alitaka kumtumia, na kufaidika na vipaji vyake na ustahili wake wote kwa kazi yake, kwamba alifanya kazi kwa ajili ya Kristo kwa miongo mingi. Alikuwa mtu tu ambaye alitumiwa na Roho Mtakatifu, na hakutumika kwa sababu Yesu alitazama ubinadamu wake kwa mapendeleo, lakini ni kwa sababu ya vipaji vyake. Aliweza kufanya kazi ya Yesu kwa sababu alipigwa, na sio kwa sababu alifurahia kufanya hivyo. Aliweza kufanya kazi kama hiyo kwa sababu ya kupata nuru na uongozi wa Roho Mtakatifu, na kazi aliyoifanya haiwakilishi harakati yake kwa njia yeyote, au ubinaadamu wake. Kazi ya Paulo inawakilisha kazi ya mtumishi, ambayo ni kusema kuwa yeye alifanya kazi ya mtume. Petro, hata hivyo, alikuwa tofauti: Yeye pia alifanya baadhi ya kazi, na ingawa haikuwa kuu kama kazi ya Paulo, alifanya kazi huku akiwa na harakati ya kuingia kwake mwenyewe, na kazi yake ilikuwa tofauti na kazi ya Paulo. Kazi ya Petro ilikuwa utekelezaji wa wajibu wa kiumbe wa Mungu. Yeye hakufanya kazi katika nafasi ya mtume, lakini wakati wa ufukuziaji wake wa upendo wa Mungu. Mwendo wa kazi ya Paulo pia ulikuwa na harakati yake binafsi. Harakati yake ilikuwa tu kwa ajili ya matumaini yake ya siku za baadaye, na shauku yake ya hatima nzuri. Yeye hakukubali usafishaji wakati wa kazi yake, wala hakukubali upogoaji na ushughulikaji. Yeye aliamini kuwa ilmradi kazi aliyoifanya iliridhisha mapenzi ya Mungu, na yote aliyofanya yalimpendeza Mungu, basi tuzo hatimaye ilikuwa unamsubiri. Hakukuwa na matukio ya kibinafsi katika kazi yake—yote yalikuwa kwa ajili yake mwenyewe, na hayakufanyika huku kukiwa na harakati ya mabadiliko. Kila kitu katika kazi yake kilikuwa shughuli, na hakukuwa na wajibu wowote au kujisalimisha kwa kiumbe cha Mungu. Wakati wa safari ya kazi yake, hakuna mabadiliko yaliyotokea katika tabia ya zamani ya Paulo. Kazi yake ilikuwa tu ya kufanya huduma kwa ajili ya wengine, na haikuwa na uwezo wa kuleta mabadiliko katika tabia yake. Paulo alifanya kazi yake moja kwa moja, bila ya kufanywa mkamilifu ama kushughulikiwa, na alivutiwa na thawabu. Petro alikuwa tofauti: alikuwa mtu ambaye alikuwa amepitia upogoaji, na alikuwa amepitia ushughulikiaji na usafishaji. Lengo na motisha za kazi ya Petro zilikuwa tofauti kimsingi na zile za Paulo. Ingawa Petro hakufanya sehemu kubwa ya kazi, tabia yake ilipitia mabadiliko mengi, na alichotafuta ni ukweli, na mabadiliko ya kweli. Kazi yake haikufanyika tu kwa ajili ya kazi yenyewe. Ingawa Paulo alifanya kazi nyingi, yote ilikuwa kazi ya Roho Mtakatifu, na ingawa Paulo alishirikiana katika kazi hii, yeye, hakuipitia. Kwamba Petro alifanya kazi ndogo ilikuwa tu kwa ajili Roho Mtakatifu hakufanya kazi kubwa kupitia yeye. Wingi wa kazi zao haukuamua iwapo walikuwa wamefanywa wakamilifu; harakati ya mmoja ilikuwa ili kupokea tuzo, na ile ya mwingine ilikuwa ili kufikia upendo wa mwisho wa Mungu na kutimiza wajibu wake kama kiumbe cha Mungu, kwa kiasi kwamba angeweza kuishi kwa kudhihirisha picha inayopendeza ili kukidhi mapenzi ya Mungu. Nje walikuwa tofauti, na pia vile vile viini vyao vilikuwa tofauti. Huwezi kuamua ni nani kati yao alifanywa mkamilifu kwa msingi wa kazi waliyofanya. Petro alitafuta kuishi kwa kudhihirisha picha ya yule ambaye hupenda Mungu, kuwa mtu ambaye alimtii Mungu, kuwa mtu ambaye alikubali ushughulikaji na upogoaji, na kuwa mtu aliyetekeleza wajibu wake kama kiumbe wa Mungu. Aliweza kujitolea kwa Mungu, kuweka nafsi yake kamilifu katika mikono ya Mungu, na kumtii hadi kifo. Hilo ndilo alilokuwa ameamua kufanya na, zaidi ya hayo, hilo ndilo alilotimiza. Hii ndiyo sababu ya msingi ya kwani hatima yake ilikuwa tofauti na ile ya Paulo. Kazi ambayo Roho Mtakatifu alifanya ndani ya Petro ilikuwa kumfanya mkamilifu, na kazi ambayo Roho Mtakatifu alifanya ndani ya Paulo ilikuwa kumtumia. Hii ni kwa sababu asili zao na mitazamo yao kuhusu harakati hazikuwa sawa. Wote walikuwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Petro alitumia kazi hii kwake mwenyewe, na pia akawapa watu wengine; Paulo, kwa upande mwingine, aliwapa wengine kazi nzima ya Roho Mtakatifu, na mwenyewe hakufaidika na chochote kutoka kwa kazi hiyo. Kwa njia hii, baada ya yeye kushuhudia kazi ya Roho Mtakatifu kwa miaka mingi, mabadiliko ndani ya Paulo yalikuwa karibu na kutokuwepo. Yeye bado alibaki karibu katika hali yake ya asili, na bado alikuwa Paulo wa awali. Ni baada tu ya kuvumilia ugumu wa miaka mingi ya kazi, ndivyo alikuwa amejifunza jinsi ya kufanya kazi, na kujifunza uvumilivu, lakini asili yake ya zamani—ushindani wake mkuu na asili wa kimamluki—bado ilibaki. Baada ya kufanya kazi kwa miaka mingi, hakufahamu asili yake potovu, wala hakuwa amejiondoa mwenyewe kutoka kwa asili yake ya zamani, na bado ilikuwa inaonekana katika kazi yake. Kwake, kulikuwepo tu na uzoefu wa kazi zaidi, lakini uzoefu mdogo kiasi hicho pekee haukuwa na uwezo wa kumbadilisha, na hukuweza kubadilisha maoni yake kuhusu kuwepo au umuhimu wa harakati yake. Ingawa alimfanyia Kristo kazi kwa miaka mingi, na hakumtesa tena Bwana Yesu, ndani ya Moyo wake hakukuwa na mabadiliko katika elimu kuhusu Mungu. Ambayo ina maana kuwa hakufanya kazi ili awe mwaminifu kwa Mungu, lakini alikuwa, badala yake, amelazimika kufanya kazi kwa ajili ya hatima yake ya siku zijazo. Kwa kuwa, hapo mwanzo, alimtesa Kristo, na hakumtii Kristo; kiasili yeye alikuwa mwasi ambaye alimpinga Kristo kimakusudi, na mtu ambaye hakuwa na elimu kuhusu kazi ya Roho Mtakatifu. Katika hitimisho la kazi yake, yeye bado hakujua kazi ya Roho Mtakatifu, na yeye tu alitenda kwa hiari yake mwenyewe kwa mujibu wa asili yake mwenyewe, bila hata kidogo kutilia maanani mapenzi ya Roho Mtakatifu. Na hivyo asili yake ilikuwa katika uhasama na Kristo na haikutii ukweli. Mtu kama huyu, ambaye alikuwa ameachwa na kazi ya Roho Mtakatifu, ambaye hakujua kazi ya Roho Mtakatifu, na ambaye pia alimpinga Kristo—je, ni jinsi gani mtu kama huyu angeokolewa? Iwapo mtu ataweza kuokolewa au la haitegemei kiasi cha kazi anayoifanya, au ni kiasi gani anajitolea, lakini badala yake kuamuliwa na iwapo anajua au hajui kazi ya Roho Mtakatifu, iwapo anaweza kuweka ukweli kwenye vitendo au la, na iwapo maoni yake kuhusu harakati yanalingana na ukweli au la.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mafanikio au Kushindwa Kunategemea Njia Ambayo Mwanadamu Hutembea

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp