Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 527

Maisha yote ya mwanadamu yamekuwa chini ya himaya ya Shetani, na hakuna mtu yeyote anayeweza kujitoa kutoka katika ushawishi wa Shetani yeye mwenyewe. Wote wanaishi katika dunia chafu, kwa upotovu na utupu, bila maana yoyote au thamani; wanaishi maisha ya kutojali kwa ajili ya mwili, tamaa, na kwa ajili ya Shetani. Hakuna maana yoyote kwa kuwepo kwao. Mwanadamu hana uwezo wa kupata ukweli utakaomweka huru kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Ingawa mwanadamu anaamini katika Mungu na anasoma Biblia haelewi jinsi ya kujitoa kutoka kwa ushawishi wa Shetani. Kutoka kitambo, watu wachache sana wametambua siri hii, wachache sana wameiguza. Hivyo, hata kama mwanadamu anamchukia Shetani, na anachukia mwili, hajui jinsi ya kujitoa kutoka kwa ushawishi mkuu wa Shetani. Je, leo bado hamjamilikiwa na Shetani? Hamjuti juu ya matendo yenu ya uasi, zaidi ya hayo, hamhisi kama wachafu na waasi. Baada ya kumpinga Mungu, bado mna amani ya moyo na mnahisi utulivu mwingi. Je, utulivu wako si kwa sababu wewe ni mpotovu? Je, hii amani ya mawazo haitokani na kuasi kwako? Mwanadamu anaishi katika jehanamu ya binadamu, anaishi katika ushawishi wa giza la Shetani; mkabala katika ardhi, mapepo yanaishi na mwanadamu, yakienea katika mwili wa mwanadamu. Duniani, hauishi katika Paradiso ya kupendeza. Mahali ambapo ulipo ni ulimwengu wa Shetani, jehanamu ya binadamu, dunia ya chini. Mwanadamu asipotakaswa, basi yeye ni wa uchafu; asipolindwa na kutunzwa na Mungu, basi yeye bado ni mfungwa wa Shetani; asipohukumiwa na kuadibiwa, basi hatakuwa na njia ya kuepuka ukandamizaji na ushawishi mbaya wa Shetani. Tabia potovu unayoonyesha, na tabia ya uasi unayoishi kwa kudhihirisha inatosha kuonyesha kwamba bado unaishi katika himaya ya Shetani. Kama akili na mawazo yako hayajatakaswa, na tabia yako haijahukumiwa na kuadibiwa, basi nafsi yako yote bado inadhibitiwa na himaya ya Shetani, akili yako bado inadhibitiwa na Shetani, mawazo yako yanatawaliwa na Shetani, na nafsi yako yote inadhibitiwa na mikono ya Shetani. Je, unajua uko umbali gani, sasa, na kiwango alichokuwa Petro? Je, wewe ni wa kiwango hicho? Ni kiasi gani unajua kuhusu adabu na hukumu ya wakati wa leo? Unacho kiasi gani cha yale Petro alipata kujua? Iwapo, leo, huna uwezo wa kutambua, je utaweza kupata maarifa haya baadaye? Mtu mzembe na mwoga kama wewe hawezi kujua kuhusu adabu na hukumu ya Mungu. Ukifuata amani ya kimwili, na raha za kimwili, basi hutakuwa na njia yoyote ya kutakaswa, na mwishowe utarudi kwa Shetani, kwa sababu hali unayoishi kwa kudhihirisha ni ya Shetani, na ya mwili. Vitu vilivyo sasa, watu wengi hawayafuati maisha, kwa hivyo inamaanisha kuwa hawajali kuhusu kutakaswa, ama kuingia katika uzoefu wa ndani ya maisha. Je, watawezaje kufanywa kuwa wakamilifu? Wale wasiofuata maisha hawana fursa ya kufanywa wakamilifu, na wale wasiofuata maarifa ya Mungu, na hawafuati mabadiliko katika tabia zao, hawataweza kuepuka ushawishi wa giza wa Shetani. Kwa kuashiria maarifa yao kuhusu Mungu na kuingia kwao katika mabadiliko ya tabia zao, hawana umakini kuzihusu, kama wale wanaoamini katika dini pekee, na wale wanaofuata tu sherehe katika kuabudu kwao. Je, hiyo si kupoteza wakati? Kama, kwa imani yake kwa Mungu, mwanadamu hayuko makini katika mambo ya maisha, hafuati kuingia katika ukweli, hazingatii mabadiliko katika tabia yake, ama kufuata maarifa ya kazi ya Mungu, basi hawezi kufanywa mkamilifu. Kama unatamani kufanywa mkamilifu, lazima uelewe umuhimu wa kazi ya Mungu. Hasa, lazima uelewe umuhimu wa adabu na hukumu Yake, na kwa nini haya yanafanywa juu ya mwanadamu. Je, unaweza kukubali? Wakati wa adabu ya aina hii, unaweza kupata uzoefu na maarifa kama Petro? Ukifuata maarifa ya Mungu na ya kazi ya Roho Mtakatifu, na kuzingatia mabadiliko katika tabia yako, basi una fursa ya kufanywa mkamilifu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Matukio Aliyopitia Petro: Ufahamu Wake wa Adabu na Hukumu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp