Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 38

Watu Wa Siku Za Mwisho Wanaiona tu Hasira Ya Mungu Katika Maneno Yake, na Hawaipitii kwa Kweli Hasira Ya Mungu

Kuanzia wakati wa uumbaji mpaka leo, hakuna kikundi ambacho kimefurahia neema au huruma nyingi za Mungu pamoja na upole wa upendo kama kikundi hiki cha mwisho. Ingawaje, kwenye awamu ya mwisho, Mungu amefanya kazi Yake ya hukumu na kuadibu, na Amefanya kazi Yake kwa adhama na hasira, wakati mwingi Mungu anatumia tu maneno kukamilisha kazi Yake; Anatumia maneno ili kufunza, kunyunyiza na kutosheleza, na kulisha. Hasira ya Mungu, wakati haya yakiendelea, siku zote imefichwa, na mbali na kuipitia tabia ya Mungu yenye hasira kwa maneno Yake, watu wachache sana wamepitia ghadhabu Yake ana kwa ana. Hivi ni kusema, kwamba wakati wa kazi ya hukumu na kuadibu kwa Mungu, ingawaje hasira iliyofichuliwa katika maneno ya Mungu inawaruhusu watu kupitia adhama na kutovumilia kosa kwa Mungu, hasira hii haizidi maneno Yake. Kwa maneno mengine, Mungu hutumia maneno ili kukemea binadamu, kumfichua binadamu, kuhukumu binadamu, kumwadhibu binadamu na hata kumshutumu binadamu—lakini Mungu angali hajawa mwenye wingi wa ghadhabu kwa binadamu, na hata hajaachilia hasira Yake kwa binadamu nje ya maneno yake. Hivyo, rehema na upole wa upendo wa Mungu uliopitiwa na binadamu kwenye enzi hii ni ufunuo wa tabia ya kweli ya Mungu, huku hasira ya Mungu iliyoipitiwa na binadamu ikiwa tu ni athari ya sauti na hisia za matamko Yake. Watu wengi wanachukulia athari hii kimakosa na kuiona kuwa njia ya kweli ya kupitia na maarifa ya kweli ya hasira ya Mungu. Hivyo basi, watu wengi wanasadiki kwamba wameiona huruma ya Mungu na upole wa upendo ndani ya maneno Yake, kwamba wameweza pia kushuhudia kutovumilia Kwake kwa kosa la binadamu, na wengi wao wamekuja hata kutambua huruma na uvumilivu wa Mungu kwake binadamu. Haijalishi tabia ya binadamu ni mbaya kiasi kipi, au upotovu wa tabia yake, Mungu siku zote anavumiliwa. Katika kuvumiliwa, nia Yake ni kusubiria maneno Aliyokuwa Ametamka, jitihada Alizofanya na gharama Aliyolipia ili kutimiza athari iliyo ndani ya wale Anaotaka kupata. Kusubiria matokeo kama haya yanachukua muda, na yanahitaji uumbaji wa mazingira tofauti ya binadamu, kwa njia sawa ambayo watu hawawi watu wazima pindi tu wanapozaliwa; huchukua miaka kumi na minane au kumi na tisa na baadhi ya watu hata huhitaji miaka ishirini au thelathini kabla hawajakomaa na kuwa mtu mzima halisi. Mungu husubiria kukamilika kwa mchakato huu, Yeye husubiria kuwadia kwa muda huo, na Yeye husubiria kufika kwa matokeo haya. Na kwa muda wote Anaousubiria, Mungu huwa mwenye wingi wa huruma. Kwenye kipindi cha kazi ya Mungu, hata hivyo, kiwango kidogo sana cha watu kinaangamizwa, na baadhi wanaadhibiwa kwa sababu ya upinzani wao mkuu kwa Mungu. Mifano kama hiyo ni ithibati kubwa zaidi ya tabia ya Mungu ambayo haivumilii kosa la binadamu, na inathibitisha kabisa uwepo wa kweli wa uvumilivu na ustahimilivu wa Mungu kwa wale wateule. Bila shaka, katika mifano hii halisi, ufunuo wa sehemu ya tabia ya Mungu kwa watu hawa hauathiri jumla ya mpango wa usimamizi wa Mungu. Kwa hakika, kwenye awamu hii ya mwisho ya kazi ya Mungu, Mungu amevumilia kwenye kipindi hiki chote ambacho Amekuwa akisubiria na Amebadilisha uvumilivu Wake na maisha Yake kwa wokovu wa wale wanaomfuata Yeye. Mnayaona haya yote? Mungu haharibu mpango Wake bila sababu. Anaweza kuiachilia hasira Yake na Anaweza pia kuwa mwenye huruma; huu ndio ufunuo wa sehemu mbili kuu za tabia ya Mungu. Je, hii iko au haiko wazi kabisa? Kwa maneno mengine, tunapokuja kwa Mungu, sahihi na isiyokuwa sahihi, yenye haki na dhalimu, nzuri na mbaya—hivi vyote vimeonyeshwa waziwazi kwa binadamu. Kile Atakachofanya, kile Anachopenda, kile Anachochukia—yote haya yanaweza kuonyeshwa moja kwa moja katika tabia Yake. Mambo kama hayo yanaweza pia kuwa ya waziwazi sana na ya kuonekana katika kazi ya Mungu na hayako juujuu au kwa jumla; badala yake, yanaruhusu watu wote kutazama tabia ya Mungu na kile Anacho na alicho hasa kwa njia thabiti, ya kweli na ya kimatendo. Huyu ndiye Mungu Mwenyewe wa kweli.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe II

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp