Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 114

Yona 3 Neno lake Yehova likakuja kwake Yona kwa mara ya pili, likisema, Inuka, nenda Ninawi, mji huo mkuu; na uuhubirie mahubiri ninayokuambia. Kwa hivyo Yona akainuka, na kuenda Ninawi, kulingana na neno la Yehova. Sasa Ninawi ulikuwa mji mkuu wa safari ya siku tatu. Naye Yona akaanza kuingia ndani ya mji huo safari ya siku moja, na akatoa sauti kubwa, na kusema, Imebaki siku arobaini, na Ninawi utashindwa. Basi watu wa hapo Ninawi wakamwamini Mungu, na wakatangaza mfungo, na wakavalia nguo za magunia, kuanzia aliyekuwa mkubwa zaidi kwao mpaka aliyekuwa mdogo zaidi. Kwa kuwa habari ilimfikia mfalme wa Ninawi, na akainuka kutoka kwa kiti chake che enzi, na akaivua nguo yake, na kuvaa nguo ya gunia, na kukaa chini katika majivu. Na akafanya kutangazwe Ninawi kupitia amri yake mfalme na wakubwa wake, ikisema, Mtu wala mnyama, wala kundi la ng’ombe, wala kundi la kondoo wasionje chochote: wasikule, wala kunywa maji: Ila mwanadamu na mnyama wavikwe kwa nguzo za magunia, na kulia kwa nguvu kwa Mungu: ndiyo, na wawageuze watu wote kutoka kwa njia ovu, na kutoka kwa vurugu iliyo mikononi mwao. Nani anayejua iwapo Mungu atabadili na kughairi, na kuiacha ghadhabu yake iliyo kali, ili tusiangamie? Naye Mungu aliona vitendo vyao, kwamba walikuwa wameiacha njia yao ovu; na Mungu akaghairi lile neno ovu, ambalo alikuwa amesema angeliwafanyia; na hakulifanya.

Kama Imani Yako kwa Mungu ni ya Kweli, Utapokea Utunzaji Wake Mara Nyingi

Kubadilisha kwa nia zake Mungu kwa watu wa Ninawi hakukuhusisha kusitasita au kutoeleweka kokote. Badala yake kulikuwa ni mabadiliko kutoka kwa hasira tupu hadi uvumilivu mtupu. Huu ni ufunuo wa kweli kuhusu hali halisi ya Mungu. Mungu hajawahi kusitasita au kufikiria mara mbili kuhusu hatua Zake; kanuni na makusudio yaliyo katika matendo Yake ni wazi na dhahiri yasiyo na kasoro wala hatia, yasiyo na njama yoyote kamwe ama mifumo iliyoingiliana. Kwa maneno mengine, hali halisi ya Mungu haina giza wala maovu mengine. Mungu alikasirikia Waninawi kwa sababu ya vitendo vya maovu ambavyo vilikuwa vimefikia macho Yake; wakati ule hasira Yake ilitokana na hali Yake halisi. Hata hivyo, wakati hasira ya Mungu ilipotoweka na akatoa uvumilivu Wake kwa watu wa Ninawi kwa mara nyingine tena, kila kitu Alichofichua kilikuwa bado ni hali Yake halisi. Uzima wa badiliko hili ulitokana na badiliko katika mtazamo wa mwanadamu kwa Mungu. Kwenye kipindi hiki chote cha muda, tabia ya Mungu isiyoweza kukosewa haikubadilika; hali halisi ya uvumilivu wa Mungu haikubadilika; hali halisi ya upendo na huruma ya Mungu haikubadilika. Wakati watu wanapotekeleza vitendo vya maovu na kumkosea Mungu atawashushia ghadhabu Yake. Wakati watu wanatubu kwa kweli, moyo wa Mungu utabadilika, na hasira Yake itasita. Wakati watu wanapoendelea kumpinga Mungu kwa usumbufu, hasira Yake kali haitasita; hasira Yake itaendelea kuwa kwao hatua kwa hatua mpaka watakapoangamizwa. Hii ndiyo hali halisi ya tabia ya Mungu. Haijalishi kama Mungu anaonyesha hasira au huruma na upole, mwenendo wa binadamu, tabia na mtazamo wake kwa Mungu ndani ya kina cha moyo wake vinatoa masharti ya kile ambacho kinaonyeshwa kupitia kwa ufunuo wa tabia ya Mungu. Kama Mungu anaendelea kuonyesha mtu hasira Yake, moyo wa mtu huyu bila shaka humpinga Mungu. Kwa sababu hajawahi kutubu kwa kweli, kuinamisha kichwa chake mbele ya Mungu au kumiliki imani ya kweli kwa Mungu, hajawahi kupata huruma na uvumilivu wa Mungu. Kama mtu anapokea utunzaji wa Mungu na mara nyingi hupokea huruma na uvumilivu wake, basi mtu huyo bila shaka anaamini Mungu kwa kweli ndani ya moyo wake, na moyo wake haumpingi Mungu. Yeye kwa mara nyingi anatubu kwa kweli mbele ya Mungu; kwa hivyo, hata kama nidhamu ya Mungu mara nyingi humshukia mtu huyu, hasira Yake haitamshukia.

Ufafanuzi huu mfupi unaruhusu watu kuuona moyo wa Mungu, kuona uhalisia wa hali Yake halisi ili kuona kwamba ghadhabu ya Mungu na mabadiliko katika moyo Wake yana sababu. Licha ya Utofautishaji mkavu ambao Mungu alionyesha Alipoghadhabishwa na pale Alipobadilisha moyo Wake, jambo ambalo linafanya watu kusadiki kwamba utofautishaji mkavu au nafasi kubwa yaonekana kuwepo kati ya dhana hizi mbili za hali halisi ya Mungu—ghadhabu Yake na Uvumilivu Wake—Mtazamo wa Mungu kwa kule kutubu kwa Waninawi kwa mara nyingine kunaruhusu watu kuweza kuona ule upande mwingine wa tabia halisi ya Mungu. Mabadiliko katika moyo wa Mungu yanaruhusu kwa kweli binadamu kwa mara nyingine kuuona ukweli wa huruma na upole wenye upendo wa Mungu na kuona ufunuo wa kweli wa hali halisi ya Mungu. Binadamu hawana budi kutambua kwamba rehema ya Mungu na upole wenye upendo si hadithi za uwongo tu, wala si ughushi. Hii ni kwa sababu hisia za Mungu kwa wakati huo zilikuwa kweli; Mabadiliko ya Mungu yalikuwa kweli; Mungu kwa kweli aliwapa binadamu kwa mara nyingine tena rehema na uvumilivu Wake.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp