Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 173

4. Nuru

Kitu cha nne kinahusiana na macho ya watu—nacho ni, nuru. Hiki pia ni muhimu sana. Unapoona nuru inayong’aa, na mwangaza wa nuru hiyo ukafikia kiasi fulani, macho yako yatapofushwa. Hata hivyo, macho ya wanadamu ni macho ya mwili. Hayana kinga dhidi ya madhara. Je, kuna yeyote anayethubutu kulitazama jua moja kwa moja? (La.) Yeyote amewahi kujaribu? Watu wengine wamejaribu. Unaweza kutazama ukiwa umevaa miwani ya jua, sivyo? Hilo linahitaji usaidizi wa vifaa. Bila vifaa, macho makavu ya mwanadamu hayathubutu kutazama jua moja kwa moja. Hata hivyo, Mungu aliumba jua ili awape wanadamu nuru, na pia aliendesha nuru hii. Mungu hakuliacha tu jua na kulipuuza baada ya kuliumba. “Nani anajali iwapo macho ya mwanadamu yanaweza kulistahimili!” Mungu hafanyi vitu hivyo. Yeye hufanya vitu kwa uangalifu sana na huzingatia vipengele vyote. Mungu aliwapa wanadamu macho ili waweze kuona, lakini Mungu ametayarisha pia umbali wa mwangaza ambao wanaweza kutazama chini yake. Haitawezekana iwapo hakuna nuru ya kutosha. Iwapo kuna giza sana mpaka watu hawawezi kuona mkono wao ulio mbele yao, kisha macho yao yatapoteza kazi yake na hayatakuwa na faida yoyote. Sehemu iliyo na mwangaza mwingi itakuwa haivumiliki kwa macho ya mwanadamu na pia hawataweza kuona chochote. Hivyo katika mazingira wanayoishi ndani wanadamu, Mungu amewapa kiasi cha nuru kinachofaa macho ya wanadamu. Nuru hii haitaumiza wala kudhuru macho ya watu. Zaidi ya hayo, haitayafanya macho ya watu yapoteze matumizi yake. Hii ndiyo sababu ambayo Mungu aliongeza mawingu yanayozunguka jua na dunia, na uzito wa hewa unaweza pia kuchuja kwa kawaida nuru inayoweza kuumiza macho ya watu au ngozi. Haya yanahusiana. Kuongezea, rangi ya dunia iliyoumbwa na Mungu huakisi pia nuru ya jua na kuondoa ile sehemu ya mwangaza katika nuru inayofanya macho ya wanadamu kutokuwa na raha. Kwa njia hiyo, watu hawahitaji kila mara kuvaa miwani myeusi sana ya jua ili waweze kutembea huko nje na kufanya shughuli za maisha yao. Katika hali za kawaida, macho ya wanadamu yanaweza kuona vitu vilivyo katika eneo la kuona kwao na hayataingiliwa kati na nuru. Yaani, nuru hii haiwezi kuwa ya kuchoma sana wala ya kufifiliza, ikiwa ya kufifiliza sana, macho ya watu yatadhuriwa na hawataweza kuyatumia kwa muda mrefu sana kabla ya macho yao kuacha kutumika; ikiwa ina mwangaza sana, macho ya watu hayataweza kuistahimili, na macho yao hayataweza kutumika katika miaka ya 30 hadi 40 au miaka 40 hadi 50. Hiyo ni kusema, nuru hii inafaa kwa macho ya wanadamu kuona, na madhara yanayoletwa kwa macho ya wanadamu na nuru yamepunguzwa na Mungu kupitia kwa mbinu mbalimbali. Haijalishi ikiwa nuru huleta faida au kikwazo kwa macho ya wanadamu, inatosha kuyawezesha macho ya watu kuendelea kuishi mpaka mwisho wa maisha yao. Je, Mungu hajalifikiria hilo kikamilifu sana? Lakini wakati Shetani, ibilisi, anafanya mambo, hafikirii mambo haya. Nuru hiyo ama ina mwangaza sana au inafifiliza sana Hivi ndivyo Shetani hufanya vitu.

Mungu alifanya vitu hivi katika vipengele vyote vya mwili wa mwanadamu—kuona, kusikia, kuonja, kupumua, hisia … kuongeza hadi upeo uwezo wa kubadilisha wa kuendelea kuishi kwa wanadamu ili waweze kuishi, waweze kuishi kwa kawaida na kuendelea kuishi. Yaani ni kusema, mazingira ya kuishi kama hayo yaliyopo yaliyoumbwa na Mungu ni mazingira ya kuishi yanayofaa zaidi na yenye faida kwa kuendelea kuishi kwa wanadamu. Wengine wanaweza kufikiri kwamba hii haitoshi na kwamba yote ni ya kawaida sana. Sauti, nuru, na hewa ni vitu ambavyo watu hufikiria kwamba walizaliwa navyo, vitu wanavyoweza kufurahia tangu wakati wa kuzaliwa. Lakini kile alichofanya Mungu kinachosababisha kufurahia kwao kwa vitu hivi ni kitu wanachohitaji kujua na kuelewa. Haijalishi ikiwa unahisi kuna haja ya kuelewa au kujua vitu hivi, kwa ufupi, Mungu alipoumba vitu hivi, alikuwa ametumia fikira, Alikuwa na mpango, Alikuwa na mawazo fulani. Hakuwaweka wanadamu katika mazingira ya kuishi kama haya kwa kawaida, kwa bahati, au bila kufikiria. Huenda mkadhani kwamba kila kitu ambacho Nimezungumzia si muhimu, lakini kwa mtazamo Wangu, kila kitu ambacho Mungu aliwapa wanadamu ni muhimu kwa kuendelea kuishi kwa binadamu. Kuna tendo la Mungu katika hili.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee VIII

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp