Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 206

Hatua moja ya kazi ya enzi mbili za awali ilifanyika Israeli; nyingine ilifanyika Uyahudi. Kuzungumza kwa jumla, hakuna hatua ya kazi hii iliyotoka Israeli; zilikuwa ni hatua za kazi zilizofanywa miongoni mwa wateule wa mwanzo. Hivyo, kwa mtazamo wa Wanaisraeli, Yehova Mungu ni Mungu wa Wanaisraeli pekee. Kwa sababu ya kazi ya Yesu huko Uyahudi, na kwa sababu ya kukamilisha Kwake kwa kazi ya kusulubiwa, kwa mtazamo wa Wayahudi, Yesu ni Mkombozi wa watu wa Kiyahudi. Yeye ni Mfalme wa Wayahudi pekee, sio wa watu wengine wowote; Yeye si Bwana anayewakomboa Waingereza, wala Bwana anayewakomboa Wamarekani, lakini Yeye ni Bwana anayewakomboa Wanaisraeli, na katika Israeli ni Wayahudi ndio Anaowakomboa. Kwa kweli, Mungu ni Bwana wa mambo yote. Yeye ndiye Mungu wa viumbe vyote. Yeye si Mungu wa Wanaisraeli pekee, na si Mungu wa Wayahudi pekee; ni Mungu wa viumbe vyote. Hatua mbili za awali za kazi Yake zilifanyika Israeli, na kwa njia hii, dhana zingine zimepata umbo ndani ya watu. Watu wanafikiri kuwa Yehova alikuwa anafanya kazi Israeli na Yesu Mwenyewe alifanya kazi Yake Yudea—zaidi ya hayo, ilikuwa kupitia kupata mwili ndiyo Alifanya kazi Yudea—na hata hivyo, kazi hii haikuenea zaidi ya Israeli. Hakuwa kazini na Wamisri; Hakuwa kazini na Wahindi; Alikuwa tu kazini na Wanaisraeli. Watu basi wanaunda dhana mbalimbali; zaidi ya hayo, wanapanga kazi ya Mungu ndani ya mawanda fulani. Wanasema kwamba wakati Mungu yuko kazini, ni lazima ifanywe miongoni mwa wateule na ndani ya Israeli; mbali na Israeli, Mungu hana mpokeaji mwingine wa kazi Yake, wala Hana mawanda mengine ya kazi Yake; wana madhubuti hasa ya “kumwadhibu” Mungu mwenye mwili, kutomruhusu kuenda zaidi ya eneo la Israeli. Hizi zote ni dhana za mwanadamu? Mungu aliunda mbingu na dunia yote na vitu vyote, na kuumba viumbe vyote; Anawezaje kuzuia kazi Yake kwa Israeli peke yake? Katika hali hiyo, kungekuwa na haja gani ya kufanya uumbaji Wake wote? Aliiumba dunia nzima; Ametekeleza mpango Wake wa usimamizi wa miaka elfu sita sio tu ndani ya Israeli lakini pia na kila mtu ulimwenguni. Bila kujali kama wanaishi Uchina, Amerika, Uingereza ama Urusi, kila mtu ni uzao wa Adamu; wote wameumbwa na Mungu. Hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuondoka katika mawanda ya uumbaji wa Mungu, na hakuna mtu hata mmoja anayeweza kuepuka utambulisho wa “ukoo wa Adamu.” Wote ni viumbe vya Mungu, na wote ni wa ukoo wa Adamu; pia ni wazawa wapotovu wa Adamu na Hawa. Sio tu Wanaisraeli ndio viumbe vya Mungu, lakini ni watu wote; hata hivyo, wengine miongoni mwa viumbe wamelaaniwa, na wengine wamebarikiwa. Kuna mambo mengi ya kupendeza kuwahusu Wanaisraeli; Mungu awali alikuwa kazini nao kwa sababu walikuwa watu wenye upotovu wa kiasi kidogo zaidi. Wachina ni wa chini wakilinganishwa nao, na hawawezi hata kutumaini kulingana nao; hivyo, Mungu awali alifanya kazi miongoni mwa watu wa Israeli, na hatua ya pili ya kazi Yake ilifanywa tu Uyahudi. Kwa sababu hii, watu huunda dhana nyingi na kanuni nyingi. Kwa kweli, iwapo Angetenda kulingana na dhana za binadamu, Mungu angekuwa tu Mungu wa Waisraeli; kwa njia hii Asingeweza kupanua kazi Yake katika mataifa yasiyo ya Kiyahudi, kwa sababu Angekuwa tu Mungu wa Wanaisraeli badala ya Mungu wa viumbe vyote. Unabii ulisema kuwa jina la Yehova lingekuwa kubwa kwa mataifa yasiyo ya kiyahudi na kuwa jina la Yehova lingeenezwa kwa mataifa yasiyo ya kiyahudi—mbona walisema hivi? Iwapo Mungu angekuwa Mungu wa Wanaisraeli tu, basi Angefanya kazi tu Israeli. Zaidi ya hayo, Asingepanua kazi hii, na Asingefanya huu unabii. Kwa sababu Alifanya huu unabii, Angehitaji kuipanua kazi Yake katika mataifa yasiyo ya kiyahudi na katika kila taifa na mahali. Kwa sababu Alisema hivi, basi Atafanya hivyo. Huu ndio mpango Wake, kwani Yeye ndiye Bwana aliyeumba mbingu na dunia na vitu vyote, na Mungu wa viumbe vyote. Bila kujali iwapo yuko kazini na Waisraeli ama Uyahudi nzima, kazi Anayoifanya ni kazi ya ulimwengu mzima na kazi ya binadamu wote. Kazi Anayoifanya leo katika taifa la joka kubwa jekundu—katika taifa lisilo Israeli—bado ni kazi ya binadamu wote. Israeli inaweza kuwa kituo cha kazi Yake duniani; vivyo hivyo, Uchina pia inaweza kuwa kituo cha kazi Yake duniani miongoni mwa mataifa yasiyo ya kiyahudi. Sasa Hajatimiza unabii kwamba “jina la Yehova litakuwa kubwa katika mataifa yasiyo ya kiyahudi”? Hatua ya kwanza ya kazi Yake miongoni mwa mataifa yasiyo ya kiyahudi inahusu kazi hii Anayoifanya katika taifa la joka kuu jekundu. Kwa Mungu mwenye mwili kufanya kazi katika nchi hii na kuwa miongoni mwa hawa watu waliolaaniwa inaenda hasa kinyume na mawazo ya mwanadamu; hawa watu ni wadogo zaidi na wasio na thamani yoyote. Hawa wote ni watu ambao Yehova alikuwa amewaacha mbeleni. Watu wanaweza kuachwa na watu wengine, lakini wakiachwa na Mungu, hawa watu hawatakuwa na hadhi, na watakuwa na thamani ya kiwango cha chini kabisa. Kama sehemu ya viumbe, kukaliwa na Shetani ama kuachwa na watu wengine yote mawili ni mambo machungu, lakini sehemu ya viumbe ikiachwa na Mungu wa uumbaji, hii inaashiria kwamba hadhi yake iko katika kiwango cha chini kabisa. Uzao wa Moabu ulilaaniwa, na ulizaliwa ndani ya nchi hii isiyo na maendeleo makubwa; bila shaka, uzao wa Moabu ni watu walio na hadhi ya chini kabisa chini ya ushawishi wa giza. Kwa sababu hawa watu walimiliki hadhi ya chini kabisa zamani, kazi inayofanywa miongoni mwao inaweza kabisa kuzivunja dhana za mwanadamu, na pia ni kazi yenye faida kubwa zaidi kwa mpango Wake mzima wa usimamizi wa miaka elfu sita. Ili Afanye kazi miongoni mwa watu hawa ni kitendo kinachoweza zaidi kuzivunja dhana za mwanadamu; Akiwa na hili Anazindua enzi; na jili Anavunja dhana za mwanadamu; Akiwa na hili Anatamatisha kazi ya Enzi ya Neema. Kazi Yake ya awali ilifanywa Uyahudi, ndani ya eneo la Israeli; katika mataifa yasiyo ya kiyahudi Hakufanya kazi yoyote ya uziduzi wa enzi. Hatua ya mwisho ya kazi Yake haifanywi tu miongoni mwa watu wa mataifa yasiyo ya kiyahudi; hata zaidi ya hayo, inafanywa miongoni mwa watu waliolaaniwa. Jambo hili moja ndiyo ushahidi unaoweza zaidi kumwaibisha Shetani; hivyo, Mungu “anakuwa” Mungu wa viumbe vyote ulimwenguni na kuwa Bwana wa vitu vyote, chombo cha kuabudiwa na kila kiumbe chenye uhai.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Mungu Ndiye Bwana wa Viumbe Vyote

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp