Wale Wanaomtii Mungu kwa Moyo wa Kweli Hakika Watakubaliwa na Mungu

Kazi ya Roho Mtakatifu inabadilika kutoka siku hadi siku, ikipanda juu kwa kila hatua; ufunuo wa kesho unakuwa hata juu kuliko wa leo, hatua kwa hatua ukikwea hata juu zaidi. Hii ndiyo kazi anayotumia Mungu kumkamilisha mwanadamu. Iwapo mwanadamu hawezi kwenda sambamba, basi anaweza kuachwa wakati wowote. Kama mwanadamu hana moyo wa kutii, basi hawezi kufuata hadi mwisho. Enzi ya kale imepita; sasa ni enzi mpya. Na katika enzi mpya, kazi mpya lazima ifanywe. Hasa katika enzi ya mwisho ambapo mwanadamu atakamilishwa, Mungu atafanya kazi mpya hata haraka zaidi. Hivyo, bila utii kwa moyo wake, mwanadamu ataona vigumu kufuata nyayo za Mungu. Mungu hafuati kanuni, wala hachukulii hatua yoyote ya kazi Yake kama isiyobadilika. Badala yake, kazi inayofanywa na Mungu daima ni mpya zaidi na daima ni juu zaidi. Kazi Yake inazidi kuwa ya vitendo kwa kila hatua, sambamba zaidi na matendo halisi ya mwanadamu. Baada tu ya mwanadamu kuwa na uzoefu wa aina hii ya kazi ndipo anaweza kufikia mabadiliko ya mwisho ya tabia yake. Maarifa ya mwanadamu ya maisha inakua hata juu zaidi, hivyo kazi ya Mungu pia inakuwa juu zaidi. Mwanadamu anaweza kufikia ukamilifu kwa njia hii tu na kufaa kwa matumizi ya Mungu. Kwa upande mmoja, Mungu anafanya hivi ili kupinga na kubadilisha dhana za mwanadamu, na kwa upande mwingine, kumwongoza mwanadamu katika hali ya juu zaidi na kweli zaidi, kwa ulimwengu wa juu zaidi wa imani kwa Mungu, ili mwishowe, mapenzi ya Mungu yanafanyika. Wote walio na asili isiyotii wanaopinga kwa kusudi wataachwa nyuma na hatua hii ya kazi ya Mungu ya haraka na yenye kusonga mbele kwa nguvu; wale tu walio na moyo mtiifu na wako tayari kuwa wanyonge wataendelea hadi mwisho wa njia. Kwa kazi kama hii, nyote mnapaswa kujua jinsi ya kusalimisha na kuweka kando dhana zenu. Kila hatua inapaswa kuchukuliwa kwa uangalifu. Kama nyinyi ni wazembe, hakika mtakuwa wamoja wa wale wanaochukiwa na kukataliwa na Roho Mtakatifu na yule anayevuruga kazi ya Mungu. Kabla ya kufanyiwa hatua hii ya kazi, kanuni na sheria za mwanadamu za zamani zilikuwa nyingi sana hadi akawa na msisimko zaidi, na mwishowe, akawa wenye majivuno na kujisahau. Hivi vyote ni vikwazo kwa njia ya mwanadamu kuikubali kazi mpya ya Mungu na ni adui kwa mwanadamu kuja kujua Mungu. Iwapo mwanadamu hana utii kwa moyo wake wala tamaa ya kujua ukweli, basi atakuwa hatarini. Ukitii tu kazi na maneno yaliyo rahisi, na huwezi kukubali yoyote yaliyo na ugumu zaidi, basi wewe ni yule anayeendelea na njia ya zamani na hawezi kwenda sambamba na kazi ya Roho Mtakatifu. Kazi inayofanywa na Mungu ni tofauti kutoka kipindi kimoja hadi kingine. Ukionyesha utii mkubwa kwa awamu moja, lakini katika awamu ifuatayo uonyeshe utii mdogo ama usionyeshe wowote, basi Mungu atakuacha. Ukienda sambamba na Mungu anapopaa hatua hii, basi lazima uendelee kuwa sambamba Anapopaa ifuatayo. Wanadamu kama hawa tu ndio wanatii Roho Mtakatifu. Kwa sababu unamwamini Mungu, lazima ubakie daima kwa utii wako. Huwezi tu kutii unapotaka na kutotii usipotaka. Namna hii ya utii haijakubaliwa na Mungu. Kama huwezi kwenda sambamba na kazi mpya Ninayoshiriki na kuendelea kuyashikilia maneno ya zamani, basi kutakuaje na ukuaji katika maisha yako? Katika kazi ya Mungu, Anakuletea kupitia neno Lake. Unapotii na kulikubali neno Lake, basi Roho Mtakatifu hakika atafanya kazi ndani yako. Roho Mtakatifu anafanya kazi kwa njia Ninayozungumza kabisa. Fanya Nilivyosema, na Roho Mtakatifu atafanya kazi ndani yako mara moja. Natoa mwangaza mpya ili muweze kuona na kuwaleta kwa mwangaza wa sasa. Unapotembea katika mwangaza huu, Roho Mtakatifu ataanza kazi ndani yako mara moja. Wengine wanaweza kuwa waasi na kusema, “Sitafanya tu usemavyo,” Basi Nakwambia kwamba sasa ni mwisho wa njia. Umenyauka na huna maisha zaidi. Hivyo, kwa kupitia mabadiliko ya tabia yako, ni muhimu kabisa kwenda sambamba na mwangaza wa sasa. Roho Mtakatifu hafanyi kazi tu kwa baadhi ya wanadamu wanaotumiwa na Mungu, lakini hata zaidi kanisani. Anaweza kuwa akifanya kazi kwa yeyote. Anaweza kufanya kazi ndani yako sasa, na baada ya wewe kuwa na uzoefu nayo, Anaweza kufanya kazi kwa mtu mwingine ajaye. Fuata kwa makini; unapozidi kufuata mwangaza wa sasa, ndipo maisha yako yanaweza kuzidi kua. Haijalishi yeye ni mwanadamu wa aina gani, alimradi Roho Mtakatifu anafanya kazi ndani yake, kuwa na hakika kufuata. Chukua ndani uzoefu wake kupitia wako mwenyewe, na utapokea mambo ya juu hata zaidi. Ukifanya hivyo utaona ukuaji haraka zaidi. Hii ni njia ya ukamilifu wa mwanadamu na njia ambayo maisha hukua. Njia ya ukamilifu inafikiwa kupitia utii wako wa kazi ya Roho Mtakatifu. Hujui kupitia mtu wa aina gani Mungu Atafanya kazi kukukamilisha, wala kupitia mtu yupi, tukio, ama jambo Atakuwezesha kuingia katika umiliki na kupata ufahamu fulani. Ukiweza kutembea kwenye njia hii sawa, hii inaonyesha kwamba kuna matumaini makubwa kwako kukamilishwa na Mungu. Kama huwezi kufanya hivyo, hii inaonyesha kwamba maisha yako ya baadaye ni ya dhalili na giza. Unapotembea kwenye njia sawa, utapewa ufunuo kwa mambo yote. Bila kujali yale Roho Mtakatifu atafichua kwa wengine, ukiendelea kwa uzoefu wako kwa msingi wa maarifa yao, kupitia mambo wewe mwenyewe, basi uzoefu huu utakuwa sehemu ya maisha yako, na utaweza kuwasambazia wengine kwa sababu ya huu uzoefu. Wale wanaosambazia wengine kwa kuyarudia maneno ni wale wasio na uzoefu; itakulazimu kujifunza kupata, kupitia mwangaza na kupatiwa nuru ya wengine, njia ya kutenda kabla ya kuzungumza kuhusu uzoefu na maarifa yako halisi. Hii itakuwa ya manufaa zaidi kwa maisha yako binafsi. Unapaswa kuwa na uzoefu kwa njia hii, kutii yote yatokayo kwa Mungu. Unapaswa kutafuta akili ya Mungu kwa vitu vyote na kujifunza masomo kwa vitu vyote, ukijenga ukuaji kwa maisha yako. Vitendo hivyo vitamudu ukuaji wa haraka zaidi.

Roho Mtakatifu Anakupatia nuru kupitia uzoefu wa vitendo vyako na Anakukamilisha kupitia imani yako. Uko tayari kweli kukamilishwa? Kama kweli uko tayari kukamilishwa na Mungu, basi utakuwa na ujasiri kuweka kando mwili wako, na kuweza kufanya asemavyo Mungu na kutokuwa mtu mtulivu ama mnyonge. Utaweza kutii yote yatokayo kwa Mungu, na vitendo vyako vyote, viwe vimefanywa hadharani au faraghani, vitastahiki kwa Mungu. Kuwa mtu mwaminifu na fanya mazoezi ya ukweli kwa mambo yote, na utakamilishwa. Wale wanadamu wadanganyifu wanaotenda njia moja mbele ya wengine na nyingine nyuma yao hawako tayari kukamilishwa. Wote ni wana wa laana na uharibifu; si wa Mungu lakini wa Shetani. Hao si aina ya wanadamu waliochaguliwa na Mungu! Kama vitendo na tabia yako haiwezi kustahiki mbele ya Mungu ama kufikiriwa na Roho wa Mungu, basi hii inaonyesha wewe una shida. Ukikubali tu hukumu na kuadibu kwa Mungu, na kuweka umuhimu katika mabadiliko ya tabia yako ndipo utawekwa kwa njia ya kukamilishwa. Ikiwa kweli uko tayari kukamilishwa na Mungu na kufanya mapenzi ya Mungu, basi unapaswa kutii kazi yote ya Mungu na kutotoa neno la malalamiko, wala hupaswi kutathmini ama kuhukumu kazi ya Mungu utakavyo. Haya ni masharti ya msingi kabisa ya kukamilisha na Mungu. Mahitaji ya wale wanaotaka kukamilishwa na Mungu ni haya: fanya mambo yote kwa moyo unaompenda Mungu. Inamaanisha nini “kufanya mambo kwa moyo unaompenda Mungu”? Inamaanisha kwamba vitendo na tabia yako yote inaweza kuletwa mbele ya Mungu. Kwa sababu una nia sawa, iwapo vitendo vyako ni sawa ama vibaya, huogopi vikionyeshwa kwa Mungu ama kwa ndugu na dada zako; unathubutu kuapa kwa Mungu. Kwamba kila nia, fikra, na wazo lako linaweza kufaa kuchunguzwa mbele ya Mungu: ukitenda na kuingia kwa njia hii, basi maendeleo katika maisha yako yatakuwa mepesi.

Kwa sababu unamwamini Mungu, basi lazima uweke imani ndani ya maneno na kazi yote ya Mungu. Hii ni kusema kwamba, kwa sababu unamwamini Mungu, ni lazima umtii. Usipoweza kufanya hivi, basi haijalishi iwapo unamwamini Mungu. Kama umemwamini Mungu kwa miaka nyingi, lakini hujawahi kumtii ama kuyakubali maneno Yake, na badala yake umemwuliza Mungu ajisalimishe kwako na kufuata dhana zako, basi wewe ni mwasi kabisa kwa wote, na wewe si muumini. Mtu kama huyu anawezaje kutii kazi na maneno ya Mungu ambayo hayafuati dhana za mwanadamu? Mtu asiyetii zaidi ni yule anayemkataa na kumpinga Mungu makusudi. Yeye ni adui wa Mungu na ni mpinga Kristo. Mtu kama huyu daima anakuwa na uadui dhidi ya kazi mpya ya Mungu, hajawahi kuonyesha nia hata ndogo ya kutii, na hajawahi kutii ama kujinyenyekea kwa furaha. Anajisifu mbele ya wengine na kamwe hajisalimishi kwa mwingine. Mbele ya Mungu, anajiona kuwa hodari zaidi kuhubiri neno na mwenye ujuzi zaidi kwa kufanya kazi kwa wengine. Kamwe hatupi hazina anazomiliki tayari, lakini anazichukua kama vitu vinavyorithiwa kwa familia vya kuabudiwa, vya kuhubiriwa kwa wengine, na kuvitumia kuhutubia wale wapumbavu wanaomwabudu. Hakika kuna baadhi ya watu kama hawa kanisani. Inaweza kusemwa kwamba wao ni “mashujaa wasioshindwa,” kizazi baada ya kizazi kinakaa kwa muda mfupi ndani ya nyumba ya Mungu. Wanachukua kuhubiri neno (mafundisho ya dini) kama wajibu wao wa juu zaidi. Mwaka baada ya mwaka na kizazi baada ya kizazi, wao huenenda kwa nguvu wakitekeleza wajibu wao “mtakatifu na usiokiukwa”. Hakuna anayethubutu kuwaguza na hakuna anayethubutu kuwapinga kwa uwazi. Walikuwa “mfalme” kwa nyumba ya Mungu, wakitenda kama dikteta kupitia enzi nyingi. Haya mapepo yanataka kuungana mikono na pamoja kuharibu kazi Yangu; Nawezaje kuyaruhusu haya mashetani hai kuwepo mbele Yangu? Hata wale walio tu na moyo nusu wa utii hawawezi kutembea hadi mwisho, sembuse hawa madikteta bila utii hata kidogo kwa mioyo yao. Kazi ya Mungu haikubaliwi virahisi na mwanadamu. Hata mwanadamu atumie nguvu yake yote, ataweza kupata kifungu tu na kufikia ukamilifu mwishowe. Basi, je, watoto wa malaika mkuu wanaotaka kuharibu kazi ya Mungu? Kwani hawana hata matumaini madogo zaidi ya kukubaliwa na Mungu? Madhumuni yangu katika kufanya kazi Yangu ya ushindi si tu kushinda kwa sababu ya ushindi, lakini kushinda ili kufichua haki na udhalimu, kupata ushahidi ili kumwadhibu mwanadamu, kulaani waovu, na hata zaidi, kushinda kwa sababu ya kukamilisha wale walio radhi kutii. Mwishowe, wote watatengwa kulingana na aina, na mawazo ya wale wote waliokamilishwa yatajazwa na utii. Hii ni kazi itakayokamilishwa mwishowe. Lakini Waliojawa na uasi wataadhibiwa, kutumwa kuchomeka kwa moto na milele kulaaniwa. Wakati huo utakapofika, wale “mashujaa wakubwa wasioshindwa” wa awali watakuwa wabaya na wanaoepukwa zaidi “wanyonge na waoga wasio na maana.” Hii tu inaweza kuonyesha haki yote wa Mungu na kwamba tabia ya Mungu hairuhusu kosa lolote. Hii tu inaweza kutuliza chuki iliyo moyoni Mwangu. Je, hamkubali kwamba hii ni ya busara sana?

Sio wote walio na uzoefu wa kazi ya Roho Mtakatifu wanaweza kupata uhai, na sio wote kwa mkondo huu wanaweza kupata uhai. Uhai sio mali ya kawaida inayoshirikisha wanadamu wote, na mabadiliko ya tabia hayafikiwi na wote. Kujisalimisha kwa kazi ya Mungu lazima kugusike na kuishi kwa kudhihirishwa. Kujisalimisha kwa kiwango cha juu juu hakuwezi kupokea idhini ya Mungu, na kutii tu vipengele vya juujuu vya neno la Mungu bila kutaka mgeuzo wa tabia ya mtu, hataweze kuufurahisha moyo wa Mungu. Kumtii Mungu na kujisalimisha kwa kazi ya Mungu ni kitu kimoja. Wale wanaojisalimisha kwa Mungu tu lakini si kwa kazi ya Mungu hawawezi kudhaniwa kuwa watiifu, na hakika wala wasiotii kweli na kwa nje hao ni wa kujipendekeza. Wale ambao kweli wanajisalimisha kwa Mungu wote wanaweza kufaidika kutokana na kazi na kupata ufahamu wa tabia na kazi ya Mungu. Wanadamu kama hawa tu ndio kweli wanajisalimisha kwa Mungu. Wanadamu kama hawa wanaweza kupata maarifa mapya kutokana na kazi mpya na kuwa na uzoefu wa mabadiliko mapya kutoka hayo. Wanadamu kama hawa tu ndio wana idhini ya Mungu; mwanadamu wa aina hii tu ndiye amekamilishwa na amepitia mabadiliko ya tabia yake. Waliokubaliwa na Mungu ni wale wanaojisalimisha kwa Mungu kwa furaha, na pia kwa neno na kazi Yake. Mwanadamu wa aina hii tu ndiye ni sawa; mwanadamu wa aina hii tu ndiye kweli anamtamani na kumtaka Mungu. Na wale wanaozungumzia tu imani yao kwa Mungu, lakini katika hali halisi wanamlaani ni wale waliovaa barakoa. Wana sumu, ni wanadamu wasaliti zaidi. Siku moja hawa walaghai watavuliwa barakoa zao mbovu. Je, hiyo si kazi inayofanywa leo? Walio waovu milele watakuwa waovu na hawataepuka siku ya adhabu. Walio wazuri milele watakuwa wazuri na watafichuliwa kazi itakapoisha. Hakuna hata mmoja wa waovu atakayedhaniwa kuwa wenye haki, wala yeyote mwenye haki atakayedhaniwa kuwa mwovu. Je, Ningemruhusu yeyote ashtakiwe kimakosa?

Maisha yako yakiendelea, lazima daima uwe na kiingilio kipya na ufahamu mpya na wa juu zaidi, unaokua kwa kina na kila hatua. Hiki ndicho wanadamu wote wanapaswa kuingia ndani. Kupitia kuwasiliana, kusikiza ujumbe, kusoma neno la Mungu, ama kushughulikia suala, utapata ufahamu mpya na kupata nuru upya. Huishi ndani ya kanuni za zamani na nyakati za zamani. Unaishi milele ndani ya mwangaza mpya, na hupotei mbali na neno la Mungu. Hii ndiyo inafikiriwa kuwa kwa njia sawa. Kulipa tu gharama ya juu juu hakutasaidia. Neno la Mungu linakuwa juu zaidi na mambo mapya yanajitokeza kila siku. Ni muhimu pia kwa mwanadamu kuingia upya kila siku. Mungu anavyozungumza, ndivyo Anatimiza yote ambayo Amezungumzia; kama huwezi kwenda sambamba, basi unalegea nyuma. Maombi yako lazima yawe ya kina; lazima ule na kunywa zaidi neno la Mungu, kuimarisha ufunuo unaopokea, na kupunguza mambo ambayo ni hasi. Lazima uimarishe hekima yako ili uweze kupata ufahamu, na kwa kuelewa kile kilicho kwa roho, kupata ufahamu wa mambo ya nje na kuelewa kiini cha suala lolote. Kama huna sifa kama hizi, utawezaje kuliongoza kanisa? Iwapo unazungumzia tu barua na mafundisho ya dini bila uhalisi wowote na bila njia ya kutenda, unaweza tu kuendelea kwa muda mfupi. Inaweza kukubaliwa kidogo kwa waumini wapya, lakini baada ya muda, wakati waumini wapya wanapata tajriba halisi, basi hutaweza tena kuwasambazia. Basi unafaa aje kwa matumizi ya Mungu? Huwezi kufanya kazi bila kupata nuru upya. Walio bila kupata nuru upya ni wale wasiojua jinsi ya kuwa na uzoefu, na wanadamu kama hao kamwe hawapati elimu mpya ama tajriba. Na hawawezi kamwe kufanya jukumu lao la kusambaza uhai, wala hawawezi kufaa kwa ajili ya matumizi na Mungu. Mwanadamu kama huyu ni dhaifu na hana maana. Kwa kweli, wanadamu kama hawa hawawezi kufanya jukumu lao kabisa kwa kazi na wote hawana faida. Wanashindwa kufanya jukumu lao na pia kwa kweli wanaweka mzigo mwingi usiohitajika juu ya kanisa. Nawahimiza hawa “wanaume wazee” kuharakisha na kuondoka kanisani ili wengine wasilazimishwe kuwaona tena. Wanaume kama hawa hawaelewi kazi mpya lakini wamejawa na dhana. Hawafanyi chochote kanisani; badala, wanachochea na kusambaza asili hasi, hata kushiriki katika kila namna ya utovu wa nidhamu na vurugu kanisani, na hivyo kuwarusha wale wasiobagua katika vurugu na machafuko. Haya mashetani hai, haya mapepo mabaya wanapaswa kuondoka kanisani haraka iwezekanavyo, isije kanisa likaharibiwa kama matokeo. Labda huogopi kazi ya leo, lakini huogopi adhabu ya haki ya kesho? Kuna idadi kubwa ya watu kanisani ambao ni vimelea, na pia kuna mbwa mwitu wengi wanaotaka kuvuruga kazi asili ya Mungu. Hawa wote ni mapepo yaliyotumwa na Ibilisi na ni mbwa mwitu wakali wanaotaka kuwala kondoo wasio na hatia. Kama hawa wanaodaiwa kuwa wanadamu hawatafukuzwa, basi wanakuwa vimelea kwa kanisa na nondo wanaokula sadaka. Hawa nondo wanaochukiza, wajinga, wabaya, na makuruhu wataadhibiwa siku moja karibuni!

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp