Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 1

Kila mmoja anapaswa kuchunguza maisha yake upya ya kumwamini Mungu ili kuona iwapo, katika kumtafuta Mungu, ameelewa kwa dhati, amefahamu kwa dhati, na kuja kumjua Mungu kwa dhati, iwapo anajua kweli ni mawazo gani Mungu Anayo kwa aina tofauti za binadamu, na iwapo kweli anaelewa kile ambacho Mungu Anafanya juu yake na jinsi Mungu Anaeleza kila tendo lake. Huyu Mungu, Ambaye yuko kando yako, Akiongoza mwelekeo wa kuendelea kwako, Akiamuru hatima yako, na kukupa mahitaji yako—ni kiasi gani ambacho, katika uchambuzi wako, unaelewa nani kiasi gani ambacho kweli unajua kumhusu Yeye? Je, unajua Anachofanyia kazi kwako kila siku? Je, unajua kanuni na makusudi Anayozingatia katika matendo Yake yote? Unajua jinsi Anavyokuongoza? Unajua mbinu Anazotumia kukupa mahitaji yako? Unajua mbinu ambazo Anatumia kukuongoza? Je, unajua kile Anachotaka kupata kutoka kwako na kile Anachotaka kutimiza kwako? Je, unajua mtazamo Anaochukua katika namna nyingi ambazo unatenda? Unajua iwapo wewe ni mtu Anayependwa na Yeye? Unajua chanzo cha furaha, hasira, huzuni na uchangamfu Wake, fikira na dhana zinazohusiana na hayo, na kiini Chake? Unajua, hatimaye, huyu Mungu ni Mungu wa aina gani ambaye unamwamini? Je, maswali haya na mengine ya aina hii kitu ambacho hujawahi kuelewa ama kuwaza kuyahusu? Katika kufuata imani yako kwa Mungu, umewahi, katika ufahamu halisi na kuyatambua maneno ya Mungu, umeondoa hali za kutomwelewa? Je, baada ya kupokea adhabu na kurudi kwa Mungu, umefikia unyenyekevu halisi na kujali kwa kweli? Je, wakati wa kuadibu kwa Mungu na hukumu, umepata kutambua uasi na asili ya kishetani ya mwanadamu na kupata kiasi kidogo cha kuelewa kuhusu utakatifu wa Mungu? Je, chini ya uongozi na kupata nuru kwa maneno ya Mungu, umeanza kuwa na mtazamo mpya wa maisha? Katika majaribu yaliyotumwa na Mungu, umepata kufahamu kutovumilia Kwake kwa makosa ya mwanadamu na pia kile Anachohitaji kutoka kwako na vile Anavyokuokoa? Iwapo hujui kutomwelewa Mungu ni nini, au jinsi ya kumaliza kutoelewa huku, basi mtu anaweza kusema hujawahi kuingia katika ushirika wa kweli na Mungu na hujawahi kumwelewa Mungu, ama angalau mtu anaweza kusema kuwa hujawahi kuwa na nia ya Kumwelewa. Iwapo hujui nidhamu ya Mungu na kuadibu ni nini, basi kwa hakika hujui kujiwasilisha na kujali ni nini, ama angalau hujawahi kujiwasilisha kwa Mungu kwa kweli au kumjali. Iwapo hujawahi kupitia kuadibu kwa Mungu na hukumu, basi kwa kweli hutajua utakatifu Wake ni nini, na utakuwa hata na ufahamu dhahiri kiasi kidogo kwa mintarafu ya uasi wa mwanadamu ni nini. Iwapo hujawahi kuwa na mtazamo sahihi wa maisha, au lengo sahihi katika maisha, bali bado uko katika hali ya mshangao na kutokuwa na uamuzi kuhusu njia yako ya maisha ya baadaye, hata kwa kiwango cha kusita kuenda mbele, basi ni dhahiri kuwa hujawahi kupokea nuru na uongozi wa Mungu kwa kweli, na mtu anaweza tu kusema kuwa hujawahi kupewa au kujazwa tena na maneno ya Mungu kwa kweli. Iwapo bado hujapitia majaribu ya Mungu, basi ni hakika kuwa bila shaka hutajua kutovumilia kwa Mungu kwa makosa ya mwanadamu ni nini, wala hutaelewa kile ambacho Mungu Anahitaji hatimaye kutoka kwako, ama hata kidogo zaidi, hatimaye, kazi Yake ya kumsimamia na kumwokoa mwanadamu ni nini. Haijalishi ni kwa miaka mingapi mwanadamu ameamini katika Mungu, iwapo hajawahi kupitia ama kutambua chochote katika maneno ya Mungu, basi kwa hakika hatembei katika njia ya kuelekea wokovu, imani yake katika Mungu kwa hakika haina chochote, maarifa yake kumhusu Mungu pia kwa hakika ni sufuri, na ni hakika kuwa hana ufahamu wowote kuhusu ni nini kumcha Mungu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp