Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Tabia ya Mungu na Kile Anacho na Alicho | Dondoo 261

Yote yaliyo duniani humu yanabadilika upesi sawasawa na mawazo ya mwenye Uweza, mbele ya macho Yake. Mambo ambayo wanadamu hawajawahi kusikia yanaweza kuja kwa ghafla. Ilhali, kile ambacho wanadamu wamemiliki, kinaweza kupotea pasipo wao kujua. Hakuna anayeweza kutambua mahali alipo mwenye Uweza, na zaidi, hakuna anayeweza kuhisi uwepo na ukuu wa nguvu za uzima za mwenye Uweza. Kuzidi Kwake uwezo wa binadamu kuko ndani ya jinsi Anavyoweza kuelewa yale ambayo wanadamu hawawezi. Ukuu wake uko katika jinsi ni Yeye anayekataliwa na wanadamu na bado Anawaokoa wanadamu. Yeye anajua maana ya maisha na mauti. Aidha, Anajua kanuni za kuishi kwa ajili ya wanadamu, Aliyewaumba. Yeye ndiye msingi wa uwepo wa wanadamu na ndiye Mkombozi wa wanadamu kufufuka tena. Yeye huilemea mioyo yenye furaha kwa huzuni na kuiinua mioyo yenye huzuni kwa furaha. Hii yote ni kwa ajili ya kazi Yake, na mpango Wake.

Wanadamu, walioacha ruzuku ya uzima kutoka kwa mwenye Uweza, hawajui kwa nini wanaishi, na bado wanaogopa kifo. Hukuna usaidizi, hakuna msaada, lakini bado wanadamu wanasita kufumba macho yao, wakiyakabili yote bila woga, wanaendeleza kwa muda mrefu kuishi kwa aibu ulimwenguni humu katika miili isiyokuwa na utambuzi wa nafsi. Unaishi hivyo, pasipo matumaini; anaishi hivyo, pasipo kuwa na lengo. Kuna aliye Mtakatifu tu katika hekaya atakayekuja kuwaokoa wale wanaoomboleza kwa maumivu na wanatamani sana majilio Yake. Imani hii haiwezi kutambulika kufikia sasa kwa watu ambao hawana utambuzi. Hata hivyo, watu bado wanaitaka sana. Mwenye Uweza ana rehema kwa watu hawa wanaoteseka sana. Wakati huo huo, Amechoshwa na watu hawa wasio na utambuzi, maana lazima Asubiri sana jibu kutoka kwa wanadamu. Anatamani kutafuta, kuutafuta moyo wako na roho yako. Anataka kukuletea chakula na maji na kukuzindua, ili usione kiu na kuhisi njaa tena. Unapokuwa umechoka na unapoanza kuona huzuni katika ulimwengu huu, usifadhaike, usilie. Mwenyezi Mungu, Mlinzi, atakaribisha kuwasili kwako wakati wowote. Yuko kandokando yako akiangalia, akikusubiri urudi. Anasubiri siku ambayo kumbukumbu yako itarejea: ukiwa na utambuzi wa ukweli kwamba ulitoka kwa Mungu, kwa namna fulani na mahala fulani ulipopotea kwa wakati mmoja, ukianguka barabarani ukiwa hujitambui, halafu pasipo kujua unakuwa na baba. Unatambua zaidi kuwa mwenye Uweza amekuwa akiangalia, akisubiri kurejea kwako muda huu wote. Anangoja kwa uchungu, akisubiri itiko pasipo jibu. Kusubiri Kwake ni kwa thamani mno na ni kwa ajili ya moyo na roho ya wanadamu. Pengine kusubiri huku hakuna mwisho, na pengine kusubiri huku kumefikia mwisho wake. Lakini unapaswa kujua kabisa moyo wako na roho yako viko wapi sasa.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kutanafusi kwa Mwenye Uweza

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp