Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 487

Kwa sababu unamwamini Mungu, basi lazima uweke imani ndani ya maneno na kazi yote ya Mungu. Hii ni kusema kwamba, kwa sababu unamwamini Mungu, ni lazima umtii. Usipoweza kufanya hivi, basi haijalishi iwapo unamwamini Mungu. Kama umemwamini Mungu kwa miaka nyingi, lakini hujawahi kumtii ama kuyakubali maneno Yake, na badala yake umemwuliza Mungu ajisalimishe kwako na kufuata dhana zako, basi wewe ni mwasi kabisa kwa wote, na wewe si muumini. Mtu kama huyu anawezaje kutii kazi na maneno ya Mungu ambayo hayafuati dhana za mwanadamu? Mtu asiyetii zaidi ni yule anayemkataa na kumpinga Mungu makusudi. Yeye ni adui wa Mungu na ni mpinga Kristo. Mtu kama huyu daima anakuwa na uadui dhidi ya kazi mpya ya Mungu, hajawahi kuonyesha nia hata ndogo ya kutii, na hajawahi kutii ama kujinyenyekea kwa furaha. Anajisifu mbele ya wengine na kamwe hajisalimishi kwa mwingine. Mbele ya Mungu, anajiona kuwa hodari zaidi kuhubiri neno na mwenye ujuzi zaidi kwa kufanya kazi kwa wengine. Kamwe hatupi hazina anazomiliki tayari, lakini anazichukua kama vitu vinavyorithiwa kwa familia vya kuabudiwa, vya kuhubiriwa kwa wengine, na kuvitumia kuhutubia wale wapumbavu wanaomwabudu. Hakika kuna baadhi ya watu kama hawa kanisani. Inaweza kusemwa kwamba wao ni “mashujaa wasioshindwa,” kizazi baada ya kizazi kinakaa kwa muda mfupi ndani ya nyumba ya Mungu. Wanachukua kuhubiri neno (mafundisho ya dini) kama wajibu wao wa juu zaidi. Mwaka baada ya mwaka na kizazi baada ya kizazi, wao huenenda kwa nguvu wakitekeleza wajibu wao “mtakatifu na usiokiukwa”. Hakuna anayethubutu kuwaguza na hakuna anayethubutu kuwapinga kwa uwazi. Wanakuwa “wafalme” katika nyumba ya Mungu, wakienea kote wakiwaonea wengine kutoka enzi hadi enzi. Hili kundi la mapepo linataka kuungana mikono na kuharibu kazi Yangu; Nawezaje kuyaruhusu haya mashetani hai kuwepo mbele Yangu? Hata wale walio tu na moyo nusu wa utii hawawezi kutembea hadi mwisho, sembuse hawa madikteta bila utii hata kidogo kwa mioyo yao. Kazi ya Mungu haikubaliwi virahisi na mwanadamu. Hata mwanadamu atumie nguvu yake yote, ataweza kupata kifungu tu na kufikia ukamilifu mwishowe. Basi, je, watoto wa malaika mkuu wanaotaka kuharibu kazi ya Mungu? Kwani hawana hata matumaini madogo zaidi ya kukubaliwa na Mungu? Madhumuni yangu katika kufanya kazi Yangu ya ushindi si tu kushinda kwa sababu ya ushindi, lakini kushinda ili kufichua haki na udhalimu, kupata ushahidi ili kumwadhibu mwanadamu, kulaani waovu, na hata zaidi, kushinda kwa sababu ya kukamilisha wale walio radhi kutii. Mwishowe, wote watatengwa kulingana na aina, na mawazo ya wale wote waliokamilishwa yatajazwa na utii. Hii ni kazi itakayokamilishwa mwishowe. Lakini Waliojawa na uasi wataadhibiwa, kutumwa kuchomeka kwa moto na milele kulaaniwa. Wakati huo utakapofika, wale “mashujaa wakubwa wasioshindwa” wa awali watakuwa wabaya na wanaoepukwa zaidi “wanyonge na waoga wasio na maana.” Hii tu inaweza kuonyesha haki yote wa Mungu na kwamba tabia ya Mungu hairuhusu kosa lolote. Hii tu inaweza kutuliza chuki iliyo moyoni Mwangu. Je, hamkubali kwamba hii ni ya busara sana?

Sio wote walio na uzoefu wa kazi ya Roho Mtakatifu wanaweza kupata uhai, na sio wote kwa mkondo huu wanaweza kupata uhai. Uhai sio mali ya kawaida inayoshirikisha wanadamu wote, na mabadiliko ya tabia hayafikiwi na wote. Kujisalimisha kwa kazi ya Mungu lazima kugusike na kuishi kwa kudhihirishwa. Kujisalimisha kwa kiwango cha juu juu hakuwezi kupokea idhini ya Mungu, na kutii tu vipengele vya juujuu vya neno la Mungu bila kutaka mgeuzo wa tabia ya mtu, hataweze kuufurahisha moyo wa Mungu. Kumtii Mungu na kujisalimisha kwa kazi ya Mungu ni kitu kimoja. Wale wanaojisalimisha kwa Mungu tu lakini si kwa kazi ya Mungu hawawezi kudhaniwa kuwa watiifu, na hakika wala wasiotii kweli na kwa nje hao ni wa kujipendekeza. Wale ambao kweli wanajisalimisha kwa Mungu wote wanaweza kufaidika kutokana na kazi na kupata ufahamu wa tabia na kazi ya Mungu. Wanadamu kama hawa tu ndio kweli wanajisalimisha kwa Mungu. Wanadamu kama hawa wanaweza kupata maarifa mapya kutokana na kazi mpya na kuwa na uzoefu wa mabadiliko mapya kutoka hayo. Wanadamu kama hawa tu ndio wana idhini ya Mungu; mwanadamu wa aina hii tu ndiye amekamilishwa na amepitia mabadiliko ya tabia yake. Waliokubaliwa na Mungu ni wale wanaojisalimisha kwa Mungu kwa furaha, na pia kwa neno na kazi Yake. Mwanadamu wa aina hii tu ndiye ni sawa; mwanadamu wa aina hii tu ndiye kweli anamtamani na kumtaka Mungu. Na wale wanaozungumzia tu imani yao kwa Mungu, lakini katika hali halisi wanamlaani ni wale waliovaa barakoa. Wana sumu, ni wanadamu wasaliti zaidi. Siku moja hawa walaghai watavuliwa barakoa zao mbovu. Je, hiyo si kazi inayofanywa leo? Walio waovu milele watakuwa waovu na hawataepuka siku ya adhabu. Walio wazuri milele watakuwa wazuri na watafichuliwa kazi itakapoisha. Hakuna hata mmoja wa waovu atakayedhaniwa kuwa wenye haki, wala yeyote mwenye haki atakayedhaniwa kuwa mwovu. Je, Ningemruhusu yeyote ashtakiwe kimakosa?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp