Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 531

Punde tu anapotajwa Petro, kila mtu anajawa na sifa, akikumbushwa mara moja hizi hadithi zote kumhusu Petro—jinsi alikana kumjua Mungu mara tatu na zaidi ya hayo kumhudumia Shetani, na hivyo kumjaribu Mungu, lakini mwishowe alisulubiwa juu chini kwa ajili Yake, na kadhalika. Sasa Naweka umuhimu mkubwa juu ya kukusimulia jinsi Petro alikuja kunijua na pia matokeo yake ya mwisho. Huyu mwanadamu Petro alikuwa wa kimo bora sana, lakini hali yake ilikuwa tofauti na ile ya Paulo. Wazazi wake walinitesa, walikuwa wa mapepo yaliyomilikiwa na Shetani, na kwa sababu hii mtu hawezi kusema kwamba walipitisha njia kwa Petro. Petro alikuwa na busara nyepesi, alipewa akili asili, kupendwa sana kutoka utotoni na wazazi wake; baada ya kukua, hata hivyo, akawa adui zao, kwani daima alitaka kunijua, na hii ilimfanya kuwapuuza wazazi wake. Hii ilikuwa kwa sababu, kwanza kabisa, aliamini kwamba mbingu na dunia na mambo yote yako mikononi mwa Mwenyezi, na kwamba mambo yote mazuri yanatoka kwa Mungu na yanakuja moja kwa moja kutoka Kwake, bila kupitia usindikaji wowote na Shetani. Na mfano usiofaa wa wazazi wake kuwa kama kikwazo, hii ilimwezesha kwa urahisi kutambua upendo na huruma Yangu, na hivyo kuchochea ndani yake hamu kubwa zaidi ya kunitafuta. Alikuwa makini sana sio tu kula na kunywa maneno Yangu, lakini hata zaidi kufahamu nia Zangu, na daima alikuwa na busara na tahadhari katika mawazo yake, kwa hivyo daima alikuwa mwerevu kwa makini ndani ya roho yake, na hivyo aliweza kuniridhisha kwa vyote alivyofanya. Kwa maisha ya kawaida, alikuwa makini kuunganisha katika maisha masomo ya wale walioshindwa katika siku za nyuma ili kujichochea mwenyewe kufanya juhudi kubwa zaidi, akihofia sana kwamba anaweza kuanguka ndani ya nyavu za ushinde. Alikuwa pia makini kupata imani na upendo wa wote ambao kupitia enzi nyingi walikuwa wamempenda Mungu. Kwa njia hii, aliharakisha maendeleo ya ukuaji wake sio tu kwa masuala hasi, lakini hasa kwa masuala chanya, hadi akawa katika uwepo Wangu mwanadamu pekee aliyenijua bora kabisa. Kwa sababu hii, si vigumu kuwazia jinsi alivyoweza kuweka yote aliyokuwa nayo mikononi Mwangu, kukosa kuwa tena bwana wake mwenyewe hata kwa kula, kuvaa, ama mahali aliishi, lakini alifanya kuniridhisha kwa mambo yote msingi ambao alifurahia fadhila Yangu. Mara nyingi Nilimweka chini ya jaribio, ambalo hakika lilimwacha nusu mfu, lakini hata katikati ya haya mamia ya majaribio, hakupoteza imani Kwangu hata mara moja ama kusikitishwa nami. Hata Niliposema nimemtupa kando, hakufa moyo wala kukata tamaa, lakini aliendelea kama mbeleni kutekeleza kanuni zake ili kutimiza pendo lake Kwangu. Nilipomwambia kwamba, ingawa alinipenda, Sikumsifu ila Ningemtupa katika mikono ya Shetani mwishowe. Katikati ya majaribio haya, ambayo hayakufikia mwili wake lakini yalikuwa majaribio ya njia ya maneno, bado alisali Kwangu: Ee, Mungu! Miongoni mwa mbingu na dunia na mambo lukuki, kuna mwanadamu yeyote, kiumbe chochote, ama kitu chochote kisicho mikononi Mwako, Mwenyezi? Unapotaka kunionyesha huruma, moyo wangu unafurahishwa sana na huruma Yako; unapotaka kunihukumu, ingawa sifai, nahisi hata zaidi siri ya kushangaza ya matendo Yako, kwa sababu Umejawa na mamlaka na hekima. Ingawa mwili wangu unaweza kuteseka, natulizwa ndani ya roho yangu. Ningewezaje kutosifu hekima Yako na matendo Yako? Hata kama nitafa baada ya kuja kukujua, kamwe nitakuwa tayari. Eh, Mwenyezi! Hakika si kwamba Wewe kweli hutaki kuniruhusu nikuone? Hakika si kwamba sistahili kweli kupokea hukumu Yako? Inaweza labda kuwa kwamba kuna kitu ndani yangu usichotaka kuona? Katikati ya majaribu ya aina hizi, hata kama Petro hakuweza kufahamu nia Zangu kwa usahihi, ni wazi kwamba aliliona kuwa suala la fahari na utukufu binafsi kutumiwa na Mimi (iwe tu kupokea hukumu Yangu ili binadamu waweze kuuona ukuu na ghadhabu Yangu), na hakuwa mwenye huzuni kwa ajili ya kuwekwa chini ya jaribio. Kwa sababu ya uaminifu wake mbele Yangu, na kwa sababu ya baraka Zangu juu yake, amekuwa mfano mwema na mfano wa kuigwa kwa mwanadamu kwa maelfu ya miaka. Je, huui si hasa mfano unaopaswa kufuata? Wakati huu, unapaswa kufikiria sana na kujaribu kutatua mbona Nimepeana ripoti ndefu ya Petro. Hii inapaswa kukutumikia kama kanuni ya maadili.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp