Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 368

Katika enzi zote, wengi wametoweka duniani kwa taabu, na kusita, na wengi wamekuja duniani kwa matumaini na imani. Nimeandaa kuja kwa wengi, na pia Nimewaondoa wengi. Watu wengi wamepitia mikono Yangu. Roho nyingi zimetupwa Kuzimu, wengi wameishi katika mwili, na wengi wamekufa na wamezaliwa upya duniani. Hata hivyo kamwe hakuna yeyote kati yao aliyepata nafasi ya kufurahia baraka za ufalme leo. Mimi nimewapa wanadamu mengi sana, lakini wamepata kidogo, lakini kwa sababu mashambulizi ya jeshi la Shetani imewafanya wasiweze kufurahia utajiri Wangu wote. Amekuwa tu na bahati nzuri ya kuangalia juu, lakini hajawahi kuwa na uwezo wa kujifurahisha kikamilifu. Mwanadamu hajawahi gundua nyumba ya hazina mwilini mwake ili kupokea utajiri wa mbinguni, kwa hivyo amepoteza baraka ambazo Nimempa. Je, si roho ya mwanadamu ndio haswa uwezo wa kumuunganisha na Roho Wangu? Mbona mwanadamu hajawahi Kunihusisha na roho yake? Mbona ananikaribia kimwili na asiweze kunikaribia kiroho? Je, sura Yangu ya kweli ni ya kimwili? Mbona mwanadamu hatambui kiini Changu? Kuna uwezekano kuwa hakujawahi kuonekana ishara yoyote Yangu ndani ya roho ya mwanadamu? Je, Nimetoweka kabisa katika roho ya mwanadamu? Ikiwa mwanadamu hataingia katika ulimwengu wa kiroho, atawezaje kufahamu nia Zangu? Je, kuna chochote machoni mwa mwanadamu ambacho kinaweza penyeza moja kwa moja mpaka ulimwengu wa kiroho? Ni mara nyingi Nimemwita mwanadamu kwa Roho Wangu, lakini matendo yake huwa ni kama amechomwa kisu na Mimi, anahusiana nami kwa umbali, katika hofu kubwa kuwa Nitamwongoza kwenda ulimwengu mwingine. Kwa mara nyingi Nimepeleleza ndani ya moyo wa mwanadamu, lakini anabaki bila ufahamu kabisa, akiwa na hofu kubwa kabisa kuwa Nitaingia nyumbani mwake na kuchukua fursa hiyo kumnyang’anya mali yake yote. Kwa hivyo, ananifungia nje, kuniacha bila chochote ila mlango uliofungwa na kukazwa na kuniacha nje kwenye baridi. Ni mara nyingi mwanadamu ameanguka na Nimemwokoa, lakini baada ya kuamka ananiacha mara moja, bila kuguswa na upendo Wangu, mwanadamu kunipiga macho ya hadhari; Sijawahi pasha joto moyo wa mwanadamu. Mwanadamu ni kiumbe kikatili kisichokuwa na hisia. Hata kama amepashwa joto na kumbatio Langu, kamwe hajawahi guswa na jambo hili. Mwanadamu ni kama kiumbe katili cha mlimani. Hajawahi thamini upendo Wangu wa binadamu. Hana nia ya kunikaribia, akipendelea kukaa katika milima, ambapo anavumilia tishio la wanyama pori—lakini bado hana nia ya kuchukua makao ndani Yangu. Simshawishi mwanadamu yeyote: Ninafanya tu kazi Yangu. Siku itawadia ambapo mwanadamu ataogelea kuja upande Wangu kutoka katikati ya bahari kuu, ili aweze kufurahia mali yote ya dunia na kuacha hatari ya kumezwa na bahari.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Maneno ya Mungu kwa Ulimwengu Mzima, Sura ya 20

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp