Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 27

Baraka za Mungu kwa Nuhu Baada ya Gharika

Mwa 9:1-6 Naye Mungu akawabariki Nuhu na wana wake, na akasema kwao, Ninyi Zaeni, na muongezeke, na muijaze tena dunia. Na wanyama wote wa dunia watawaogopa na kuwa na hofu nanyi, na ndege wote wa angani, na vyote vitembeavyo duniani, na kila samaki wa baharini; wamewekwa katika mikono yenu. Kila kisongacho kilicho na uhai kitakuwa chakula chenu, jinsi ambavyo nimewapa mboga ndivyo ninavyowapa vitu vyote. Lakini nyama iliyo na uhai, ambayo ni damu yake, ninyi msiile. Na bila shaka nitahitaji damu yenu ya uhai wenu, nitaihitaji kwa mkono wa kila mnyama, na kwa mkono wa mwanadamu, nitahitaji uhai wa mwanadamu kwa mkono wa ndugu wa kila mwanadamu. Yeyote ambaye atamwaga damu ya mwanadamu, damu yake itamwagika na mwanadamu: kwa kuwa Mungu alimfanya mwanadamu kwa mfano wake.

Baada ya Nuhu kukubali maagizo ya Mungu na kujenga safina na kuishi katika siku zile husika Mungu alitumia gharika ili kuangamiza ulimwengu, familia yake nzima ya wanane ilinusurika. Mbali na familia ya Nuhu ya wanane, wanadamu wote waliangamizwa, na viumbe wote nchini wakaangamizwa. Kwa Nuhu, Mungu alimpa baraka, na akasema baadhi ya mambo kwake na watoto wake wa kiume. Mambo haya yalikuwa yale ambayo Mungu alikuwa akimpa yeye na pia baraka zake kwake yeye. Hizi ndizo baraka na ahadi Mungu humpa yule ambaye anaweza kumsikiliza Yeye na kuyakubali maagizo Yake, na pia namna anavyotuza watu. Hivi ni kusema, haijalishi kama Nuhu alikuwa binadamu mtimilifu au alikuwa binadamu mwenye haki mbele ya macho ya Mungu, na haijalishi ni kiwango kipi alichomjua Mungu, kwa ufupi, Nuhu na watoto wake wa kiume watatu wote waliyasikiliza maneno ya Mungu, wakaratibu na kazi ya Mungu, na kufanya kile walichofaa kufanya kulingana na maagizo ya Mungu. Kutokana na hayo, walimsaidia Mungu kuweza kubakiza binadamu na aina mbalimbali za viumbe walio na uhai baada ya kuangamizwa kwa ulimwengu na gharika, na hivyo wakawa wamefanya mchango mkubwa kwa hatua iliyofuata ya mpango wa usimamizi wa Mungu. Kwa sababu ya kila kitu alichokuwa amefanya, Mungu alimbariki. Pengine kwa watu wa leo, kile alichofanya Nuhu hakikuwa sana na thamani ya kutajwa. Baadhi wanaweza hata kufikiria: Nuhu hakufanya chochote; Mungu alikuwa ameamua akilini Mwake kumhifadhi, hivyo kwa hakika angehifadhiwa. Kuwepo kwake si kwa sababu yake. Hili ndilo jambo ambalo Mungu alitaka lifanyike, kwa sababu binadamu ni mtulivu. Lakini hicho sicho Mungu alikuwa anafikiria. Kwa Mungu, haijalishi kama mtu ni mkubwa au asiye wa maana, mradi tu aweze kumsikiliza Yeye, kutii maagizo Yake na kile anachomwaminia na aweze kushirikiana na kazi Yake, mapenzi Yake, na mpango Wake, ili mapenzi Yake na Mpango Wake iweze kukamilika vizuri, basi mwenendo wake unastahili kukumbukwa na Yeye na kustahili kupokea baraka Zake. Mungu huthamini sana watu kama hao, na Yeye Hupenda sana vitendo vyao na upendo wao na huba yao Kwake. Huu ndio mwelekeo wa Mungu. Hivyo kwa nini Mungu alimbariki Nuhu? Kwa sababu hivi ndivyo Mungu anavyoshughulikia vitendo kama hivyo na utiifu wa mwanadamu.

Kuhusiana na baraka za Mungu kwa Nuhu, baadhi ya watu watasema: “Kama binadamu atamsikiliza Mungu na kumtosheleza Mungu, basi Mungu anafaa kumbariki binadamu. Je, hilo halifanyiki hivyo bila kusema?” Tunaweza kusema hivyo? Baadhi ya watu husema: “La.” Kwa nini hatuwezi kusema hivyo? Baadhi ya watu husema: “Binadamu hastahili kufurahia baraka za Mungu.” Hilo si sahihi kabisa. Kwa sababu wakati mtu anapokubali kile Mungu amemwaminia, Mungu anacho kiwango cha kuhukumu kama vitendo vya mtu huyu ni vizuri au vibaya na kama mtu huyu amemtii, na kama mtu huyu ametosheleza mapenzi ya Mungu na kama kile anachofanya kimeruhusiwa. Kile anachojali Mungu ni kuhusu moyo wa mtu huyu, si vitendo vyake vya juujuu. Si jambo kwamba Mungu anafaa kubariki mtu mradi tu afanye hivyo, licha ya namna anavyofanya hivyo. Huku ni kutoelewa kwa watu kumhusu Mungu. Mungu huangalia tu mwisho wa matokeo ya mambo, lakini Anatilia mkazo zaidi kuhusu namna moyo wa mtu ulivyo na namna mwelekeo wa mtu ulivyo wakati wa maendeleo ya mambo, na Anaangalia kama kunao utiifu, utiliaji maanani, na tamanio ya kumtosheleza Mungu ndani ya moyo wake. Nuhu alijua kiasi kipi kumhusu Mungu wakati huo? Kiasi hicho kilikuwa kingi kama mafundisho ya dini mnayojua sasa? Kuhusu dhana za ukweli kama vile dhana na maarifa ya Mungu, alipokea kunyunyizia na uchungaji kama ninyi? La, hakupokea! Lakini kunao ukweli mmoja ambao haupingiki: Katika fahamu, akili, na hata kina cha mioyo ya watu wa leo, dhana zao na mwelekeo wao kwa Mungu umejaa ukungu na haueleweki. Mnaweza hata kusema kwamba sehemu fulani ya watu inashikilia mwelekeo mbaya kwa uwepo wa Mungu. Lakini katika moyo wa Nuhu na fahamu yake, uwepo wa Mungu ulikuwepo na bila shaka, na hivyo basi utiifu wake kwa Mungu ulikuwa haujatiwa doa wala toa na ungeweza kustahimili majaribio. Moyo wake ulikuwa safi na wazi kwa Mungu. Hakuhitaji maarifa ya mafundisho ya dini mengi mno ili kujishawishi kufuata kila neno la Mungu, wala hakuhitaji ukweli mwingi kuthibitisha uwepo wa Mungu, ili akubali kile Mungu alimwaminia na kuweza kufanya chochote kile ambacho Mungu angemruhusu kufanya. Hii ni tofauti muhimu kati ya Nuhu na watu wa leo, na pia ndio ufasili wa kweli hasa kuhusu binadamu mtimilifu alivyo machoni mwa Mungu. Kile anachotaka Mungu ni watu kama Nuhu. Yeye ni aina ya mtu anayesifiwa na Mungu, na pia hasa mtu wa aina ile ambaye Mungu hubariki. Mmepokea nuru yoyote kutoka haya? Watu huangalia watu kutoka nje, huku naye Mungu anaangalia mioyo ya watu na kiini chao. Mungu hamruhusu yeyote kuwa na moyo wowote wa kukosa ari au shaka kwake Yeye, wala Hawaruhusu watu kushuku au kumjaribu Yeye kwa njia yoyote ile. Hivyo, ingawaje watu wa leo wako uso kwa uso na neno la Mungu, au mnaweza hata sema kwamba wako uso kwa uso na Mungu, kutokana na kitu kilicho ndani ya mioyo yao, uwepo wa kiini chao potovu, na mwelekeo wao wenye ukatili kwake Yeye, wamezuiliwa kutoka kwa imani yao ya kweli kwa Mungu na kuzibwa kutoka kwa utiifu wao kwake Yeye. Kwa sababu ya haya, ni vigumu sana kwao kutimiza baraka sawa ambazo Mungu alikabidhi Nuhu.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe I

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp