Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 76

Unapoweza kutambua kwa kweli fikira na mtazamo wa Mungu kwa wanadamu, wakati unapoweza kuelewa kwa kweli hisia na kujali kwa Mungu kwa kila kiumbe, utaweza kuelewa kule kujitolea na upendo unaotumika kwa kila mmoja wa watu walioumbwa na Muumba. Haya yanapofanyika, utatumia maneno mawili kufafanua upendo wa Mungu—maneno hayo mawili ni yapi? Baadhi ya watu husema “mwenye kujitolea” na baadhi ya watu wakasema “kuwa na huruma nyingi ya kutoa msaada.” Kati ya kauli hizi mbili, “kuwa na huruma nyingi ya kutoa msaada” ndiyo kauli ambayo inafaa kwa kiasi kidogo zaidi kuufafanua upendo wa Mungu. Hii ni kauli ambayo watu hutumia kufafanua fikira na hisia za mtu kwa upana wa akili zake. Naichukia kweli kauli hii kwa sababu inarejelea ule utoaji wa msaada bila mpango na bila ubaguzi, bila kujali kanuni zozote. Ni maelezo ya kihisia za ziada za watu wajinga na waliochanganyikiwa. Wakati neno hili linatumika kufafanua upendo wa Mungu, bila shaka kuna nia ya kukufuru. Nina maneno mawili ambayo yanafafanua kwa usahihi zaidi upendo wa Mungu—maneno hayo mawili ni yapi? Neno la kwanza ni “kubwa.” Je, si neno hili huamsha na kuleta hisia? Neno la pili ni “pana.” Kunayo maana halisi katika maneno haya mawili mbili Ninazotumia katika kufafanua upendo wa Mungu. Kama yatachukuliwa kwa njia ya moja kwa moja, “kubwa” linafafanua ukubwa au wingi wa kitu, lakini haijalishi kitu hicho kina ukubwa gani—ni kitu ambacho watu wanaweza kugusa na kuona. Hii ni kwa sababu kipo, si kifaa cha kidhahania na kinapatia watu hisia kwamba kwa kiasi fulani kina usahihi na hali ya kimatendo. Haijalishi kama unakiangalia kutoka katika mtazamo bapa au wa pande zote tatu; huhitajiki kufikiria uwepo wake, kwa sababu ni kitu ambacho kwa kweli kipo. Hata ingawa kwa kutumia “kubwa sana” kufafanua upendo wa Mungu kunaweza kuhisiwa kana kwamba tunataka kupima wingi wa upendo Wake, lakini hata hivyo linatoa hisia kwamba hauwezi kupimwa. Nasema kwamba upendo wa Mungu unaweza kupimwa kwa sababu upendo Wake si aina fulani ya kitu kisichojulikana, wala hauchipuki tu kutoka kwa ngano yoyote. Badala yake, ni kitu cha kutumiwa kwa pamoja na vitu vyote katika utawala wa Mungu, na ni kitu cha kufurahiwa na viumbe vyote hadi kwa viwango tofauti na kutoka katika mitazamo tofauti. Ingawa watu hawawezi kukiona au kukigusa, upendo huu huleta maendelezo na maisha katika vitu vyote kwani kinafichuliwa hatua kwa hatua katika maisha yao, na wanahesabu na kushuhudia upendo wa Mungu wanaofurahia kila wakati. Nasema kwamba upendo wa Mungu hauwezi kuhesabiwa kwa sababu fumbo la Mungu la Yeye kukidhi na kuimarisha vitu vyote ni kitu ambacho ni kigumu kwa wanadamu kuelewa, kama vile tu zilivyo fikira za Mungu katika vitu vyote na hasa vile vya mwanadamu. Hivyo ni kusema hakuna anayejua damu na machozi ambayo Muumba ametoa kwa sababu ya wanadamu. Hakuna anayeweza kufahamu, hakuna anayeweza kuelewa kina au uzito wa upendo ambao Muumba anao kwa ajili ya wanadamu, aliowaumba kwa mikono Yake binafsi. Kufafanua upendo wa Mungu kama mkubwa sana ni kuwasaidia watu kutambua na kuelewa upana wake na ukweli wa uwepo wake. Iko hivyo ili watu waweze kufahamu kwa kina zaidi maana halisi ya neno “Muumba,” na ili watu waweze kupata ufahamu wa kina zaidi wa maana ya “uumbaji.” Neno “pana” kwa kawaida huwa linafafanua nini? Linatumika kwa ujumla kumaanisha bahari au ulimwengu kama vile ulimwengu mpana au bahari pana. Ule mtanuko na kina kitulivu cha ulimwengu unazidi ufahamu wa binadamu na ni kitu ambacho kinanata fikra za binadamu, ambacho kwacho wamejawa na upendezwaji. Fumbo lake na umuhimu wake vyote vimo katika uwezo wa kuonekana lakini haviwezi kufikika. Unapofikiria kuhusu bahari, unafikiria kuhusu upana wake—yaonekana isiyo na mipaka, na unaweza kuhisi ile hali ya bahari hiyo kuwa fumbo na ujumuishwaji wake pia. Ndiyo maana Nimetumia neno “pana” kufafanua upendo wa Mungu. Ni kuwasaidia watu wahisi namna neno hilo lilivyo na thamani, na ili wahisi ule urembo wa kipekee wa upendo Wake, na kwamba nguvu za upendo wa Mungu haziishi na zimeenea. Ni kwa minajili ya kuwasaidia kuhisi utakatifu wa upendo Wake, na heshima pamoja na hali ya kutoweza kukosewa ya Mungu ambayo inafichuliwa kupitia upendo Wake. Sasa unafikiri kwamba “pana” ni neno linalofaa kufafanua upendo wa Mungu? Je, upendo wa Mungu unaweza kufikia maana ya maneno haya mawili, “kubwa sana” na “pana”? Bila shaka! Katika lugha ya binadamu, maneno haya mawili tu ndiyo ambayo yanafaa kwa kiasi fulani, na kwa kiasi fulani yanakaribia kuufafanua upendo wa Mungu. Je, huoni hivyo? Kama Ningewaulizeni kuufafanua upendo wa Mungu, je, mngetumia kauli hizi mbili? Kuna uwezekano mkubwa zaidi, msingeyatumia kwa sababu ufahamu na utambuzi wenu wa upendo wa Mungu ni finyu na unafikia tu mtazamo bapa, na bado haujakwea ngazi hadi katika ule urefu wa nafasi ya pande zote tatu. Hivyo basi kama Ningetaka mfafanue upendo wa Mungu, mngehisi kwamba mnakosa maneno; huenda pengine hata mtakosa kuongea kabisa. Maneno haya mawili ambayo Nimeyazungumzia leo yanaweza kuwa magumu kwako kuelewa, au pengine kwa ufupi tu hukubali. Hali hii inaweza kuongelea tu hoja kwamba utambuzi na ufahamu wako wa upendo wa Mungu ni wa juujuu na ndani ya upana mwembamba. Nimesema awali kwamba Mungu ni mwenye kujitolea—unakumbuka neno kujitolea? Inaweza kusemekana kwamba upendo wa Mungu unaweza kufafanuliwa tu kuwa wa kujitolea? Je, si haya si mawanda membamba mno? Mnafaa kutafakari suala hili zaidi ili kuweza kufaidika kutoka kwalo.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Kazi ya Mungu, Tabia ya Mungu, na Mungu Mwenyewe III

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp