Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 426

02/11/2020

Kutangazwa rasmi kwa amri katika enzi mpya ni ushahidi wa ukweli kwamba wanadamu wote katika mkondo huu na wale ambao husikia sauti ya Mungu leo wameingia katika enzi mpya. Huu ni mwanzo mpya kwa ajili ya kazi ya Mungu nao ni mwanzo wa sehemu ya mwisho ya kazi katika mpango wa usimamizi wa Mungu katika kipindi cha miaka elfu sita. Amri za enzi mpya zinaashiria kuwa Mungu na binadamu wameingia katika eneo la mbingu mpya na nchi mpya, na kwamba Mungu, kama vile Yehova alifanya kazi miongoni mwa Waisraeli naye Yesu alifanya kazi miongoni mwa Wayahudi, Ataifanya kazi zaidi ya vitendo na kuifanya kazi zaidi na kubwa zaidi duniani. Pia zinaashiria kwamba kundi hili la watu watapokea agizo zaidi na kubwa zaidi kutoka kwa Mungu, nao watapokea ugavi wa vitendo, malisho, msaada, huduma na ulinzi kutoka kwa Mungu. Zaidi ya hayo watafanywa kupitia katika mazoezi zaidi ya vitendo, na pia kushughulikiwa, kuvunjwa na kusafishwa kwa neno la Mungu. Maana ya amri za enzi mpya ni kubwa sana. Zinaonyesha kwamba Mungu kweli ataonekana kwenye ardhi naye Mungu ataushinda ulimwengu mzima juu ya nchi, akiuonyesha utukufu Wake wote katika mwili. Pia zinaonyesha kwamba Mungu wa vitendo anaenda kuifanya kazi zaidi ya vitendo duniani ili akamilishe yote ambayo Amechagua. Zaidi ya hayo, Mungu atatimiza kila kitu kwa maneno duniani na kufanya wazi amri kwamba “Mungu mwenye mwili huinuka juu zaidi naye ametukuzwa, nao watu wote na mataifa yote hupiga magoti kumwabudu Mungu—ambaye ni mkuu.” Ingawa amri za enzi mpya ni za mwanadamu kuzishika, na ingawa kufanya hivyo ni wajibu wa mwanadamu na jukumu lake, maana ambazo zinawakilisha ni ya kina sana kuweza kuonyeshwa kikamilifu katika neno moja au mawili. Amri za enzi mpya zinachukua nafasi ya sheria za Agano la Kale na maagizo ya Agano Jipya kama zilivyotangazwa rasmi na Yehova na Yesu. Hili ni somo la ndani zaidi, sio jambo rahisi kama mtu anavyoweza kufikiria. Amri za enzi mpya zinazo kipengele cha maana ya vitendo: Zinatumika kama kipengee kinachojitokeza kati ya Enzi ya Neema na Enzi ya Ufalme. Amri za enzi mpya zinahitimisha mazoea yote na maagizo yote ya enzi ya zamani na pia zinahitimisha mazoea yote ya enzi ya Yesu na zile kabla yake. Zinamleta mwanadamu katika uwepo wa Mungu wa vitendo zaidi na kumruhusu mtu kuanza kuupokea ukamilifu wa binafsi wa Mungu, ambazo ni mwanzo wa njia ya kukamilika. Kwa hiyo, ninyi mtamiliki mtazamo sahihi kuelekea amri za enzi mpya na wala hamtazifuata ovyo wala kuzidharau. Amri za enzi mpya zinasisitiza hoja moja: kwamba mwanadamu atamwabudu Mungu wa vitendo Mwenyewe wa leo, ambayo ni kutii kiini cha Roho katika matendo zaidi. Pia zinasisitiza kanuni ambayo Mungu atamhukumu mwanadamu kuwa na hatia au haki Atakapoonekana kama Jua la haki. Amri zinaeleweka kwa urahisi kuliko kutendwa. Hivyo, kama Mungu anataka kumkamilisha mwanadamu, lazima Atafanya hivyo kupitia kwa maneno Yake mwenyewe na mwongozo, mwanadamu hawezi kufikia ukamilifu kupitia asili ya akili yake peke yake. Ikiwa mwanadamu anaweza kuzishika amri za enzi mpya au la inahusiana na maarifa ya mwanadamu ya Mungu wa vitendo. Kwa hiyo, kama unaweza kuzishika amri au la sio swali litakalotatuliwa katika siku chache. Hili ni somo la kina.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp