Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 115

Yona 3 Neno lake Yehova likakuja kwake Yona kwa mara ya pili, likisema, Inuka, nenda Ninawi, mji huo mkuu; na uuhubirie mahubiri ninayokuambia. Kwa hivyo Yona akainuka, na kuenda Ninawi, kulingana na neno la Yehova. Sasa Ninawi ulikuwa mji mkuu wa safari ya siku tatu. Naye Yona akaanza kuingia ndani ya mji huo safari ya siku moja, na akatoa sauti kubwa, na kusema, Imebaki siku arobaini, na Ninawi utashindwa. Basi watu wa hapo Ninawi wakamwamini Mungu, na wakatangaza mfungo, na wakavalia nguo za magunia, kuanzia aliyekuwa mkubwa zaidi kwao mpaka aliyekuwa mdogo zaidi. Kwa kuwa habari ilimfikia mfalme wa Ninawi, na akainuka kutoka kwa kiti chake che enzi, na akaivua nguo yake, na kuvaa nguo ya gunia, na kukaa chini katika majivu. Na akafanya kutangazwe Ninawi kupitia amri yake mfalme na wakubwa wake, ikisema, Mtu wala mnyama, wala kundi la ng’ombe, wala kundi la kondoo wasionje chochote: wasikule, wala kunywa maji: Ila mwanadamu na mnyama wavikwe kwa nguzo za magunia, na kulia kwa nguvu kwa Mungu: ndiyo, na wawageuze watu wote kutoka kwa njia ovu, na kutoka kwa vurugu iliyo mikononi mwao. Nani anayejua iwapo Mungu atabadili na kughairi, na kuiacha ghadhabu yake iliyo kali, ili tusiangamie? Naye Mungu aliona vitendo vyao, kwamba walikuwa wameiacha njia yao ovu; na Mungu akaghairi lile neno ovu, ambalo alikuwa amesema angeliwafanyia; na hakulifanya.

Kutubu kwa Kweli Ndani ya Mioyo ya Waninawi Kunawapa Rehema ya Mungu na Kwabadilisha Hatima Zao Wenyewe

Je, kulikuwa na kuhitilafiana kokote kati ya mabadiliko ya moyo wa Mungu na hasira Yake? Bila shaka la! Hii ni kwa sababu uvumilivu wa Mungu kwa wakati ule ulikuwa na sababu yake. Je, sababu yake yaweza kuwa nini? Ni ile iliyotajwa kwenye Biblia: “Kila mtu aligeuka kutoka kwenye njia yake ya maovu” na “kuacha udhalimu uliokuwa mikononi mwake.”

Hii “Njia ya maovu” hairejelei kusanyiko la vitendo vya maovu, lakini inarejelea chanzo cha maovu katika tabia ya watu. “Kugeuka kutoka njia yake ya maovu” kunamaanisha kwamba wale wanaozungumziwa hawatawahi kutekeleza vitendo hivi tena. Kwa maneno mengine, hawatawahi kuwa na tabia inayoonyesha njia hii ya maovu tena; mbinu, chanzo, kusudio, nia na kanuni za vitendo vyao vyote vimebadilika; hawatawahi tena kutumia mbinu na kanuni hizi kuleta nafuu na furaha mioyoni mwao. Kule “kuacha” katika “kuacha udhalimu ulio mikononi mwao” kunamaanisha kuweka chini au kuweka pembeni, kujitenga kabisa na mambo ya kale na kutorudi nyuma tena. Wakati watu wa Ninawi walipoacha udhalimu uliokuwa mikononi mwao, hii ilithibitisha na vilevile iliwakilisha kutubu kwao kwa kweli. Mungu huangalia kwa makini sehemu ya nje na vilevile ndani ya mioyo ya watu. Wakati Mungu alipoangalia kwa makini kutubu kwa kweli katika mioyo ya Waninawi bila kuuliza swali na pia kutambua kwamba walikuwa wameacha njia zao za maovu na kuacha udhalimu uliokuwa mikononi mwao, Alibadilisha moyo Wake. Hivi ni kusema kwamba mwenendo na tabia ya watu hawa na njia mbalimbali za kufanya mambo, pamoja na kuungama na kutubu kwa kweli kwa dhambi zilizokuwa mioyoni mwao, kulisababisha Mungu kubadilisha Moyo Wake, kubadilisha nia Zake, kufuta uamuzi wake na kutowaadhibu wala kuwaangamiza. Kwa hivyo, watu wa Ninawi waliweza kufikia hatima tofauti. Waliyakomboa maisha yao binafsi na wakati uo huo wakapata kibali cha huruma na uvumilivu wa Mungu, na wakati uo huo Mungu akawa pia amefuta hasira Yake.

Huruma na Uvumilivu wa Mungu si Nadra—Kutubu kwa Kweli kwa Binadamu Ni Nadra

Licha ya vile ambavyo Mungu alikuwa na ghadhabu kwa Waninawi, mara tu walipotangaza kufunga na kuvalia nguo ya gunia pamoja na jivu, moyo Wake ulianza kutulia taratibu, na Akaanza kubadilisha moyo Wake. Wakati Alipowatangazia kwamba Angeangamiza mji wao—ule muda kabla ya kuungama na kutubu kwa dhambi zao—Mungu alikuwa angali na ghadhabu na wao. Baada ya wao kupitia misururu ya vitendo vya kutubu, ghadhabu ya Mungu kwa watu wa Ninawi ikaanza kubadilika kwa utaratibu na Akaanza kuwaonea huruma na uvumilivu. Hakuna kitu kinachohitilafiana kuhusu ufunuo wenye ulinganifu katika dhana hizi mbili za tabia ya Mungu kwenye tukio lilo hilo. Ni vipi ambavyo mtu anafaa kuelewa na kujua ukosefu huu wa kuhitilafiana? Mungu aliweza kuonyesha kwa ufanisi na kufichua vipengele hivi viwili tofauti kabisa wakati watu wa Ninawi walipokuwa wakitubu, na Akawaruhusu watu kuona uhalisi na hali halisi ya kutokosewa kwa Mungu. Mungu alitumia mtazamo Wake kuambia watu yafuatayo: Si kwamba Mungu havumilii watu, au hataki kuwaonyesha huruma; ni kwamba wao hutubu kwa kweli mara nadra sana kwa Mungu, na ni nadra sana kwa watu kuweza kugeuka kwa kweli na kuacha njia zao za maovu na kuacha udhalimu ulio mikononi mwao. Kwa maneno mengine, wakati Mungu ana ghadhabu kwa binadamu, Anatumaini kwamba binadamu ataweza kutubu kwa kweli na Anatumaini kumwona binadamu akitubu kwa kweli, ambapo Ataendelea kwa haki kumpa binadamu huyo huruma na uvumilivu. Hivi ni kusema kwamba mwenendo wa maovu ya mwanadamu ndio husababisha hasira ya Mungu, huku nazo rehema na uvumilivu wa Mungu zikipewa wale wanaomsikiliza Mungu na kutubu mbele yake, kwa wale wanaoweza kugeuka na kuacha njia zao za maovu na kuacha udhalimu ulio kwenye mikono yao. Mtazamo wa Mungu uliweza kufichuliwa waziwazi kuhusiana na vile Alivyowashughulikia Waninawi: Huruma na uvumilivu wa Mungu kwa kweli si vigumu kuvipokea; Anahitaji mtu kuwa na kutubu kwa kweli. Mradi tu watu waweze kugeuka na kuacha njia zao za maovu na kuuacha udhalimu ulio mikononi mwao, Mungu atabadilisha moyo Wake na kubadilisha mtazamo Wake kwao.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp