Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 149

Jinsi Ambavyo Shetani Hutumia Desturi ya Kitamaduni Kumpotosha Mwanadamu

Je, kuna mambo mengi yanayochukuliwa kuwa sehemu ya desturi ya kitamaduni? (Ndiyo.) Hii desturi ya kitamaduni inamaanisha nini? (Inapitishwa kutoka kwa mababu.) Inapitishwa kutoka kwa mababu, hiki ni kipengele kimoja. Kutoka mwanzo, familia, vikundi vya makabila, na hata jamii ya binadamu imepitisha njia yao ya maisha, ama mila, misemo, na kanuni, ambazo zimeingizwa kwenye fikira za watu. Watu wanafikiria nini kuhusu mambo haya? Watu wanayachukulia kuwa yasiyoweza kutengwa na maisha yao. Wanayachukua mambo haya na kuyachukulia kuwa kanuni na uhai wa kutii, na hata kamwe hawataki kuyabadilisha ama kuyaacha mambo haya kwa sababu yalipitishwa kutoka kwa mababu. Kuna vipengele vingine vya desturi ya kitamaduni, kama kile kilichopitishwa na Confucius ama Mencius, ama mambo waliyofunzwa watu na Utao ama Uconfucius ambayo yamekuwa sehemu ya kila mtu hadi ndani kwa mifupa yao. Sivyo? (Ndiyo.) Desturi ya kitamaduni inajumuisha nini? Inajumuisha likizo ambazo watu wanasherehekea? Kwa mfano, Tamasha la Majira ya machipuko, Tamasha la Taa, Siku ya Kufagia Kaburi, Tamasha la Mashua ya Joka, pamoja na Tamasha ya Zimwi na Tamasha ya Katikati ya Majira ya Kupukutika kwa Majani. Baadhi za familia hata husherehekea wakati wazee wanahitimu umri fulani, ama wakati watoto wanahitimu umri wa mwezi 1 na wakati wako na umri wa siku 100. Hizi zote ni likizo za desturi. Je, si usuli wa likizo hizi unajumuisha desturi ya kitamaduni? Ni nini kiini cha desturi ya kitamaduni? Kina chochote cha kufanya na kumwabudu Mungu? Kina chochote cha kufanya na kuwaambia watu kuweka katika vitendo ukweli? (La.) Kuna likizo zozote za watu kutoa sadaka kwa Mungu, kwenda kwa madhabahu ya Mungu na kupokea mafunzo Yake? Kuna likizo kama hizi? (La.) Watu hufanya nini katika likizo hizi zote? (Kumwabudu Shetani. Kula, kunywa na shughuli za burudani.) Katika nyakati za sasa zinaonekana kuwa hafla za kula, kunywa, na kujiburudisha. Ni nini chanzo cha desturi ya kitamaduni? Desturi ya kitamaduni imetoka kwa nani? (Shetani.) Imetoka kwa Shetani. Katika usuli wa hizi likizo za desturi, Shetani anaingiza mambo ndani ya mwanadamu, haya ni mambo gani? Kuhakikisha kwamba watu wanakumbuka mababu zao, hili ni mojawapo ya mambo haya? Kwa mfano, wakati wa Tamasha la Kufagia Kaburi watu husafisha makaburi na kutoa sadaka kwa mababu zao hivyo watu hawatasahau mababu zao. Pia, Shetani anahakikisha kwamba watu wanakumbuka kuwa wazalendo, kama katika Tamasha la Mashua ya Joka. Je, Tamasha la Katikati ya Majira ya Kupukutika kwa Majani? (Kupatana kwa familia.) Ni nini usuli wa kupatana kwa familia? Sababu zake ni nini? (Hisia.) Kuwasiliana na kuunganika kihisia. Bila shaka, iwapo ni kusherehekea Mkesha wa Mwaka Mpya wa Mwezi ama Tamasha la Taa, kuna njia nyingi za kuelezea sababu za usuli. Haijalishi mtu anaelezea sababu iliyo nyuma yazo, kila moja ni njia ya Shetani ya kuingiza filosofia yake na kufikiria kwake kwa watu, ili waweze kupotea kutoka kwa Mungu na wasijue kwamba kuna Mungu, na kwamba watoe sadaka ama kwa mababu zao au Shetani, ama kwamba ni udhuru wa kula, kunywa na kujifurahisha kwa ajili ya matamanio ya mwili. Kila ya likizo hizi inaposherehekewa, fikira na mitazamo ya Shetani yanapandwa kwa kina ndani ya akili za watu na hata hawajui. Wakati watu wanafika umri wa kati ama zaidi, fikira na mitazamo hii ya Shetani tayari yamekita mizizi ndani sana ya mioyo yao. Zaidi, watu wanafanya juhudi zao kabisa kueneza fikira hizi, ziwe sahihi ama si sahihi, kwa kizazi kifuatacho bila wasiwasi pasipo kuchagua. Sivyo? (Ndiyo.) Ni jinsi gani desturi hii ya kitamaduni na likizo hizi zinapotosha vipi watu? Unajua? (Watu wanawekewa mipaka na kufungwa na kanuni za hizi desturi kana kwamba hawana muda ama nguvu kumtafuta Mungu.) Hiki ni kipengele kimoja. Kwa mfano, kila mtu anasherehekea wakati wa Mwaka Mpya wa Mwezi, usingesherehekea, hungehisi huzuni? Je, kuna miiko yoyote ambayo unapaswa kushikilia? Hungehisi, “Wai, sikusherehekea Mwaka Mpya. Siku hii ya Mwaka Mpya wa Mwezi ilikuwa mbaya sana; mwaka huu wote utakuwa mbaya”? Si ungehisi kutokuwa na utulivu na kuogopa kiasi? Kuna hata watu wengine ambao hawajatoa sadaka kwa mababu zao kwa miaka mingi na ghafla wamekuwa na ndoto ambapo mtu aliyekufa anawaomba pesa, watahisi nini ndani yao? “Inahuzunisha kwamba huyu mtu aliyekufa anahitaji pesa ya kutumia! Nitawachomea baadhi ya pesa ya karatasi, nisipo hiyo hakika haitakuwa sawa. Sisi tunaoishi tunaweza kupatana na shida kidogo nisipochoma baadhi ya pesa ya karatasi, ni nani anayeweza kusema wakati janga litatokea?” Daima watakuwa na wingu hili dogo la hofu na wasiwasi katika mioyo yao. Ni nani anayewapa wasiwasi? (Shetani.) Shetani huleta wasiwasi. Si hii ndiyo njia moja ambayo Shetani anampotosha mwanadamu? Anatumia mbinu na udhuru mbalimbali ili kukudhibiti, kukutishia, kukufunga, hadi kiasi kwamba unachanganyikiwa na kumkubali na kumnyenyekea; hivi ndivyo Shetani anampotosha mwanadamu. Nyakati nyingi ambapo watu ni wanyonge ama hawaelewi vyema hali ilivyo, wanaweza bila kutaka, kufanya kitu kwa njia iliyochanganyikiwa, yaani, wanaanguka chini ya mshiko wa Shetani bila kusudi na wanaweza kufanya kitu bila kusudi na wasijue wanafanya nini. Hii ni njia ambayo Shetani anampotosha mwanadamu. Hata kuna watu wachache sasa ambao wanasita kuachana na desturi za kitamaduni ambazo zimekita mizizi na hawawezi tu kuziacha. Ni hasa wakati ni wanyonge na wasipoonyesha hisia ndipo wanataka kusherehekea likizo za aina hizi na wanataka kukutana na Shetani na kumridhisha Shetani tena, ambako kupitia huko wanaweza pia kujifariji ndani yao. Ni nini usuli wa hizi desturi za kitamaduni? Mkono mweusi wa Shetani unavuta nyuzi nyuma ya pazia? Asili ovu ya Shetani inatawala na kudhibiti vitu? Shetani anadhibiti hivi vitu vyote? (Ndiyo.) Wakati watu wanaishi katika desturi ya kitamaduni na kusherehekea likizo za desturi za aina hizi, tunaweza kusema kwamba haya ni mazingira ambapo wanadanganywa na kupotoshwa na Shetani, na zaidi ya hayo wana furaha kupotoshwa na Shetani? (Ndiyo.) Hiki ni kitu ambacho nyinyi nyote mnakiri, ambacho nyote mnakijua.

Neno, Vol. 2. Kuhusu Kumjua Mungu. Mungu Mwenyewe, Yule wa Kipekee V

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp