Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 172

Kazi katika mkondo wa Roho Mtakatifu, bila kujali ni kazi ya Mungu Mwenyewe au ni kazi ya watu wanaotumiwa, ni kazi ya Roho Mtakatifu. Kiini cha Mungu Mwenyewe ni Roho, ambaye anaweza kuitwa Roho Mtakatifu au Roho mwenye nguvu mara saba. Kwa vyovyote, ni Roho wa Mungu. Ni kwamba tu Roho wa Mungu anaitwa majina tofauti katika enzi tofauti tofauti. Lakini nafsi Yao bado ni moja. Hivyo, kazi ya Mungu mwenyewe ni kazi ya Roho Mtakatifu; kazi za Mungu mwenye mwili hazitofautiani na kazi za Roho Mtakatifu. Kazi ya wanadamu wanaotumiwa pia ni kazi ya Roho Mtakatifu. Ni kwamba tu kazi ya Mungu ni dhihirisho kamili la Roho Mtakatifu, na hakuna tofauti, ilhali kazi ya wanadamu wanaotumiwa inachanganyika na mambo mengi ya kibinadamu, na wala sio udhihirishaji wa moja kwa moja wa Roho Mtakatifu, wala udhihirishaji kamili. Kazi ya Roho Mtakatifu ina mawanda mapana na wala haizuiliwi na hali yoyote ile. Kazi hiyo inatofautiana kwa watu tofauti tofauti, na kutoa dutu tofauti tofauti zifanyazo kazi. Kazi pia inatofautiana katika enzi mbali mbali, kama pia ilivyo kazi tofauti katika nchi mbalimbali. Bila shaka ingawa Roho Mtakatifu hufanya kazi katika njia nyingi tofauti tofauti na kulingana na kanuni nyingi, haijalishi kazi imefanyikaje au kwa watu wa aina gani, kiini ni tofauti daima, na kazi Anazofanya kwa watu tofauti zote zina kanuni na zote zinaweza kuwakilisha kiini cha mhusika anayefanyiwa kazi. Hii ni kwa sababu kazi ya Roho Mtakatifu ni mahususi kabisa kwa mapana yake na inapimika. Kazi inayofanywa katika mwili uliopatikana si sawa na kazi inayofanywa kwa watu, na kazi hii pia inatofautiana kulingana na tabia mbalimbali za watu. Kazi inayofanywa katika mwili uliopatikana si sawa na kazi inayofanywa kwa watu, na katika mwili uliopatikana Hafanyi kazi ile ile kama aliyoifanya kwa watu. Kwa ufupi, haijalishi Anafanya kazi jinsi gani, kazi katika vitu mbalimbali haifanani, na kanuni ambazo Anazitumia kufanya kazi zinatofautiana kulingana na hali na asili ya watu mbalimbali. Roho Mtakatifu Anafanya kazi kwa watu tofautitofauti kulingana na kiini chao cha asili na haweki mahitaji ambayo ni zaidi ya kiini chao cha asili, na wala Hafanyi kazi zaidi ya tabia yao halisi. Kwa hivyo, kazi ya Roho Mtakatifu kwa mwanadamu inawaruhusu watu kuona dutu ya mtu anayefanyiwa kazi. Utu wa asili wa mwanadamu haubadiliki; tabia halisi ya mwanadamu ina mipaka. Kama Roho Mtakatifu huwatumia watu au anawafanyia watu kazi, kazi hiyo siku zote inafanywa kulingana na tabia za watu ili waweze kunufaika kutoka kwayo. Roho Mtakatifu anapofanya kazi kwa wanadamu wanaotumika, karama zao na tabia zao halisi zinatumiwa pia na wala haziachwi. Tabia zao halisi zinatumiwa zote kwa ajili ya kutoa huduma kwa kazi. Tunaweza kusema kuwa Anafanya kazi kwa kutumia sehemu zilizopo za wanadamu ili kupata matokeo yatendayo kazi. Kinyume chake, kazi inayofanyika katika mwili uliopatikana ni kumdhihirisha moja kwa moja Roho na wala haichanganywi na akili na mawazo ya mwanadamu, haifikiwi na karama za mwanadamu, uzoefu wa mwanadamu au hali ya ndani ya mwanadamu. Kazi nyingi mno ya Roho Mtakatifu yote inalenga kumnufaisha na kumwadilisha mwanadamu. Lakini baadhi ya watu wanaweza kukamilishwa wakati wengine hawana vigezo vya kuweza kukamilishwa, ni sawa na kusema, hawawezi kukamilishwa na ni vigumu sana kuokolewa, na ingawa wanaweza kuwa walishakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu, mwishowe wanaondolewa. Hii ni sawa na kusema kwamba kazi ya Roho Mtakatifu ni kuwaadilisha watu, hii haimaanishi kwamba wale wote waliokwisha kuwa na kazi ya Roho Mtakatifu wanapaswa kukamilishwa kikamilifu, kwa sababu njia wanayoiendea watu wengi si njia ya kukamilishwa. Wana kazi moja tu ya Roho Mtakatifu, na wala si ushirikiano wa kibinafsi wa binadamu au njia sahihi za kibinadamu. Kwa njia hii, kazi ya Roho Mtakatifu kwa watu hawa inakuwa kazi katika huduma ya wale ambao wanakamilishwa. Kazi ya Roho Mtakatifu haiwezi kuonwa moja kwa moja na watu au kuguswa moja kwa moja na watu wenyewe. Inaweza kudhihirishwa tu kwa njia ya msaada wa watu wenye karama ya kufanya kazi, ikiwa na maana kwamba kazi ya Roho Mtakatifu inatolewa kwa wafuasi Wake kwa njia ya udhihirisho wa wanadamu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Kazi ya Mungu na Kazi ya Mwanadamu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp