Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Siri Kuhusu Biblia | Dondoo 279

Biblia imekuwa sehemu ya historia ya binadamu kwa miaka mingi. Zaidi ya hayo, watu huichukulia kuwa Mungu, kufikia kiwango ambapo katika siku za mwisho, imechukua nafasi ya Mungu, jambo ambalo linamchukiza Mungu. Hivyo, muda uliporuhusu, Mungu alihisi kulazimishwa kubainisha maelezo ya ndani na vyanzo vya Biblia; Asingefanya hivi, Biblia ingeendelea kushikilia nafasi ya Mungu mioyoni mwa watu, na watu wangetumia maneno ya Biblia kupima na kushutumu matendo ya Mungu. Kwa kuelezea asili, muundo na dosari za Biblia, Mungu hakuwa akikana kuwepo kwa Biblia hata kidogo, wala Hakuwa anaishutumu; badala yake, Alikuwa akitoa maelezo yaliyofaa na kustahili yaliyorejesha picha asilia ya Biblia, Akazungumzia suitafahamu za watu kuhusu Biblia, na kuwapa maoni sahihi ya Biblia, ili wasiiabudu Biblia tena, na wasipotee tena; yaani, ili wasichanganye tena imani yao pofu ya Biblia kuwa imani katika Mungu na ibada ya Mungu, wakihofia hata kukabili usuli na dosari zake za kweli. Mara tu watu wanapopata ufahamu wa Biblia usiochanganywa na mambo duni, wanaweza kuiweka kando bila majuto na kuyakubali maneno mapya ya Mungu kwa ujasiri. Hili ndilo lengo la Mungu katika sura hizi kadhaa. Ukweli ambao Mungu angetaka kuwaambia watu hapa ni kwamba hakuna nadharia ama ukweli ambao unaweza kuchukua nafasi ya kazi na maneno ya Mungu ya leo, na kwamba hakuna kitu kinachoweza kuwa mbadala wa Mungu. Ikiwa watu hawawezi kuepuka mtego wa Biblia, hawatawahi kuweza kuja mbele za Mungu. Ikiwa wanataka kuja mbele za Mungu, lazima kwanza waitakase mioyo yao na kuondoa chochote kinachoweza kuchukua nafasi Yake; kisha watamridhisha Mungu. Ingawa Mungu anaifafanua Biblia pekee hapa, usisahau kwamba kuna mambo mengi yenye makosa ambayo watu wanayaabudu kwa kweli kando na Biblia; mambo wasiyoyaabudu ni yale yanayotoka kwa Mungu kwa kweli pekee. Mungu anatumia tu Biblia kama mfano kuwakumbusha watu wasichukue njia mbaya, na wasivuke mipaka tena na kukanganyikiwa wanapomwamini Mungu na kukubali maneno Yake.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp