Unyakuo ni lazima utegemezwe maneno ya Mungu na sio dhana na mawazo ya mwanadamu
“Kunyakuliwa” si kuchukuliwa kutoka mahali pa chini kwenda mahali pa juu jinsi watu wanavyofikiria. Hili ni kosa kubwa sana. Kunyakuliwa kunarejelea kujaaliwa Kwangu na kuchagua. Kunawalenga wale wote ambao Nimewaamua kabla na kuwachagua. Wale ambao wamepata hadhi ya mzaliwa wa kwanza, hadhi ya wana, au watu, ni wale wote ambao wamenyakuliwa. Hili halilingani kabisa na mawazo ya watu. Wale walio na sehemu katika nyumba Yangu katika siku zijazo wote ni watu ambao wamenyakuliwa mbele Yangu. Hii ni kweli kabisa, haibadiliki kamwe, na haiwezi kukataliwa na mtu yeyote. Hili ni jibu la mapigo dhidi ya Shetani. Mtu yeyote Niliyemwamua kabla atanyakuliwa mbele Yangu.
Unyakuo wa kweli ni nini?
Sisi ni kundi la watu wa kawaida tu, waliomilikiwa na tabia potovu ya kishetani, wale waliochaguliwa na Mungu kabla ya enzi, na wale maskini ambao Mungu ameinua kutoka jaani. Kuna wakati tulipomkataa na kumshutumu Mungu, lakini sasa tumeshindwa na Yeye. Kutoka kwa Mungu tumepokea uzima, njia ya uzima wa milele. Licha ya mahali ambapo tunaweza kuwa duniani, licha ya mateso na dhiki tunazovumilia, hatuwezi kuwa mbali na wokovu wa Mwenyezi Mungu. Kwa kuwa Yeye ndiye Muumba wetu, na ukombozi wetu pekee!