Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 462

Matakwa mnayohitaji kutimiza leo—kufanya kazi pamoja kwa upatanifu—ni sawa na huduma ambayo Yehova alitaka kutoka kwa Waisraeli: Vinginevyo, acheni tu kufanya huduma. Kwa sababu ninyi ni watu wanaomhudumia Mungu moja kwa moja, angalau lazima muweze kuwa waaminifu na watiifu katika huduma yenu, na pia lazima muweze kupata mafunzo kwa njia ya utendaji. Kwa wale kati yenu wanaofanya kazi kanisani hasa, je, kuna yeyote kati ya akina ndugu walio chini yenu anayeweza kuthubutu kuwashughulikia? Je, mtu yeyote anaweza kuthubutu kuwaambia makosa yenu ana kwa ana? Mko juu ya wengine wote, mnatawala kama wafalme! Hata hamchunguzi ama kuingia katika mafunzo ya utendaji ya aina hii, lakini bado mnazungumza kuhusu kumhudumia Mungu! Kwa sasa, unaombwa uyaongoze makanisa kadhaa, lakini hukosi tu kujitolea, bali hata unashikilia mawazo na maoni yako mwenyewe, ukisema mambo kama, “Nadhani suala hili linapaswa kutendwa kwa namna hii, kwa kuwa Mungu amesema kwamba hatupaswi kuzuiliwa na wengine na kwamba siku hizi hatupaswi kutii bila kufikiria.” Kwa hivyo, kila mmoja wenu anashikilia maoni yake mwenyewe, na hakuna anayemtii mwenzake. Ingawa unajua vyema kwamba huduma yako ina shida kubwa, bado unasema, “Jinsi nionavyo, njia yangu ni sahihi kiasi. Haidhuru, kila mmoja wetu ana upande wake: Wewe zungumzia upande wako, nami nitazungumzia upande wangu; wewe shiriki kuhusu maono yako, nami nitazungumzia kuingia kwangu.” Kamwe huwajibikii mambo mengi ambayo yanapaswa kushughulikiwa, ama unaridhika tu, kila mmoja wenu akijadili maoni yake mwenyewe na kuilinda hadhi, sifa na heshima yake mwenyewe kwa uangalifu. Hakuna yeyote kati yenu aliye tayari kujinyenyekeza, na hakuna atakayechukua hatua ya kwanza kujitolea na kufidiana kasoro zenu ili maisha yasonge mbele upesi zaidi. Mnaposhirikiana pamoja, mnapaswa kujifunza kuutafuta ukweli. Unaweza kusema, “Sielewi vyema kuhusu kipengele hiki cha ukweli. Je, una uzoefu upi kuuhusu?” Ama unaweza kusema, “Una uzoefu mwingi kuniliko kuhusu kipengele hiki; tafadhali unaweza kuniongoza kiasi?” Je, hiyo haitakuwa njia nzuri ya kulitatua? Mmesikiliza mahubiri mengi, na mna uzoefu kiasi kuhusu kufanya huduma. Msipojifunza kutoka kwa kila mmoja, msaidiane, na kufidiana dosari zenu mnapofanya kazi makanisani, basi mnawezaje kupata mafunzo yoyote? Wakati wowote mnapokabiliwa na chochote, mnapaswa kufanya ushirika ninyi kwa ninyi ili maisha yenu yaweze kufaidika. Aidha, mnapaswa kufanya ushirika kwa makini kuhusu mambo ya aina yoyote kabla kufanya maamuzi yoyote. Ni kwa kufanya hivyo tu ndipo mnawajibikia kanisa badala ya kutenda kwa uzembe tu. Baada ya kutembelea makanisa yote, mnapaswa kukusanyika pamoja na kushiriki kuhusu masuala yote mnayogundua na matatizo yoyote mliyokumbana nayo katika kazi yenu, na kisha mnapaswa kuwasiliana kuhusu nuru na mwangaza ambao mmepokea—huu ni utendaji wa msingi wa huduma. Lazima mfanikishe ushirikiano wa upatanifu kwa ajili ya kazi ya Mungu, kwa manufaa ya kanisa, na ili muwahimize ndugu zenu mbele. Mnapaswa kushirikiana, kila mmoja akimrekebisha mwenzake na kufikia matokeo bora ya kazi, ili kuyatunza mapenzi ya Mungu. Hii ndiyo maana ya ushirikiano wa kweli, na ni wale tu wanaoshiriki katika ushirikiano huo ndio watakaopata kuingia kwa kweli. Mnaposhirikiana, baadhi ya maneno mnayozungumza yanaweza kuwa yasiyofaa, lakini hilo si muhimu. Shirikini kulihusu baadaye, na mlielewe vyema; msilipuuze. Baada ya ushirika wa aina hii, mnaweza kufidia kasoro za ndugu zenu. Ni kwa kusonga kwa kina daima katika kazi yenu kwa namna hii ndipo mnaweza kupata matokeo bora. Kama watu wanaomhudumia Mungu, kila mmoja wenu lazima aweze kulinda maslahi ya kanisa katika kila kitu mnachofanya, badala ya kuzingatia tu masilahi yenu wenyewe. Haikubaliki ninyi kutenda kila mtu peke yake, daima mkidhoofishana. Watu wanaotenda kwa namna hiyo hawafai kumhudumia Mungu! Watu kama hao wana tabia mbaya sana; hawana ubinadamu hata kidogo ndani yao. Wao ni Shetani asilimia mia moja! Wao ni wanyama! Hata sasa, mambo kama haya bado hutokea miongoni mwenu; hata mnafika kiasi cha kushambuliana wakati wa ushirika; mkitafuta visingizio kwa makusudi na kughadhabika sana mnapogombana kuhusu suala fulani lisilo la maana, pasiwe na mtu aliye radhi kujiweka kando, kila mtu akimfichia mwenzake fikira zake za ndani, akimtazama yule mwingine kwa makini na kuwa mwangalifu daima. Je, tabia ya aina hii inafaa katika kumhudumia Mungu? Je, kazi kama hiyo yako inaweza kuwapa ndugu zako chochote? Huwezi tu kuwaongoza watu kwenye njia sahihi ya maisha, lakini kwa kweli unawajaza ndugu zako tabia zako potovu. Je, huwadhuru wengine? Dhamiri yako ni mbaya na ni mbovu kabisa! Huingii katika uhalisi, wala huuweki ukweli katika vitendo. Aidha, unawafichulia wengine asili yako mbaya mno bila aibu. Huna aibu hata kidogo! Umeaminiwa ndugu hawa, lakini unawapeleka kuzimuni. Je, wewe si mtu ambaye dhamiri yake imekuwa mbovu? Huna aibu hata kidogo!

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Hudumu Jinsi Waisraeli Walivyohudumu

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp