Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 132

23/07/2020

Bidii na Faida za Ayubu katika Maisha Zamruhusu Kukabiliana na Kifo kwa Utulivu

Katika Maandiko imeandikwa kuhusu Ayubu: “Kwa hivyo Ayubu akafariki, akiwa mzee na aliyejawa na siku” (Ayubu 42:17). Hii inamaanisha kwamba wakati Ayubu alipoaga dunia, hakuwa na majuto na hakuhisi maumivu, lakini aliondoka kimaumbile ulimwenguni. Kama vile kila mmoja anavyojua, Ayubu alikuwa mwanamume aliyemcha Mungu na aliyeambaa maovu alipokuwa hai; Mungu alimpongeza kwa matendo yake ya haki, watu waliyakumbuka, na maisha yake, zaidi ya yeyote yule mwengine, yalikuwa na thamani na umuhimu. Ayubu alifurahia baraka za Mungu na aliitwa mtakatifu na Yeye hapa duniani, na aliweza pia kujaribiwa na Mungu na kujaribiwa na Shetani; alisimama kuwa shahidi wa Mungu na alistahili kuwa mtu mtakatifu. Kwenye miongo mbalimbali baada ya kujaribiwa na Mungu, aliishi maisha ambayo yalikuwa yenye thamani zaidi, yenye maana zaidi, yaliyokita mizizi, na yenye amani zaidi kuliko hata awali. Kutokana na matendo yake ya haki, Mungu alimjaribu; kwa sababu ya matendo yake ya haki, Mungu alionekana kwake na kuongea naye moja kwa moja. Kwa hiyo, kwenye miaka yake baada ya kujaribiwa, Ayubu alielewa na kushukuru thamani ya maisha kwa njia thabiti zaidi, aliweza kutimiza ufahamu wa kina zaidi wa ukuu wa Muumba, na akapata maarifa yenye hakika na usahihi zaidi kuhusu namna ambavyo Muumba anavyotoa na kuzichukua baraka zake. Biblia inarekodi kwamba Yehovah Mungu alimpa hata baraka nyingi zaidi Ayubu kuliko hapo awali, Akimweka Ayubu katika nafasi bora zaidi ya kujua ukuu wa Muumba na kujua kukabiliana na kifo akiwa mtulivu. Kwa hiyo, Ayubu alipozeeka na kukabiliana na kifo, bila shaka asingekuwa na wasiwasi na mali yake. Hakuwa na wasiwasi wowote, hakuwa na chochote cha kujutia, na bila shaka hakuogopa kifo; kwani aliishi maisha yake akitembea ile njia ya kumcha Mungu, kuepuka maovu, na hakuwa na sababu yoyote ya kuwa na wasiwasi kuhusu mwisho wake mwenyewe. Ni watu wangapi leo wanaweza kuchukua hatua kwa njia zote hizo ambazo Ayubu alitumia alipokabiliwa na kifo chake mwenyewe? Kwa nini hakuna mtu anayeweza kuendeleza mwelekeo wa mtazamo rahisi kama huu? Kunayo sababu moja tu: Ayubu aliishi maisha kwenye harakati ya kutafuta kimsingi kusadiki, utambuzi, na unyenyekevu kwa ukuu wa Mungu, na ilikuwa katika kusadiki huku, utambuzi huu na unyenyekevu huu ambapo aliweza kupitia zile awamu muhimu za maisha, aliishi kwa kudhihirisha miaka yake ya mwisho na akajuliana hali na awamu yake ya mwisho ya maisha. Licha ya kile ambacho Ayubu alipitia, bidii zake na shabaha zake katika maisha zilikuwa za furaha na wala si zenye maumivu. Alikuwa na furaha si tu kwa sababu ya baraka au shukrani aliyopewa yeye na Muumba, lakini muhimu zaidi kwa sababu ya shughuli zake na shabaha za maisha, kwa sababu ya maarifa yaliyoongezeka kwa utaratibu na ufahamu wa kweli wa ukuu wa Muumba ambao alitimiza kupitia kwa kumcha Mungu na kwa kuepuka maovu, na zaidi, kwa sababu ya matendo Yake ya maajabu ambayo Ayubu alipitia kibinafsi wakati huu akiwa chini ya ukuu wa Muumba, na hali aliyopitia yenye uchangamfu na isiyosahaulika na kumbukumbu za kuwepo kwake, kuzoeana na wenzake, na kuzoeana kati yake yeye na Mungu; kwa sababu ya tulizo na furaha zilizotokana na kujua mapenzi ya Muumba; kwa sababu ya kustahi kulikotokea baada ya kuona kwamba Yeye ni mkubwa, ni wa ajabu, Anayependeka, na ni mwaminifu. Sababu ya Ayubu kuweza kukabiliana na kifo bila ya kuteseka ni kwamba alijua kwamba, kwa kufa, angerudi kwenye upande wa Muumba. Na zilikuwa shughuli zake katika maisha zilizomruhusu kukabiliana na kifo akiwa ametulia, kukabiliana na matarajio ya Muumba kuchukua tena maisha yake, kwa moyo mzuri, na zaidi ya yote, kusimama wima, kutotikisika na kuwa huru kutokana na mashaka mbele ya Muumba. Je, watu wanaweza siku hizi kutimiza aina ya furaha ambayo Ayubu alikuwa nayo? Je, nyinyi wenyewe mko katika hali ya kufanya hivyo? Kwa sababu watu siku hizi wako hivyo, kwa nini hawawezi kuishi kwa furaha, kama alivyofanya Ayubu? Kwa nini hawawezi kutoroka mateso yanayotokana na woga wa kifo? Wakati wanapokabiliwa na kifo, baadhi ya watu hujiendea haja ndogo; wengine hutetemeka, wakazirai, na wakalalamika dhidi ya Mbinguni na binadamu vilevile, wengine hata wakalia kwa huzuni na kutokwa machozi. Kwa vyovyote vile, hii ndiyo miitikio ya ghafla inayofanyika wakati kifo kinapokaribia. Watu huwa na tabia hii ya kuaibisha haswa kwa sababu, ndani ya mioyo yao, wanaogopa kifo, kwa sababu hawana maarifa yaliyo wazi na uwezo wa kushukuru ukuu wa Mungu na mipangilio yake, na isitoshe hata kujinyenyekeza mbele ya vitu hivi; kwa sababu watu hawataki chochote ila kupangilia na kutawala kila kitu wenyewe, kudhibiti hatima zao binafsi, maisha yao binafsi na hata kifo. Si ajabu, hivyo basi, kwamba watu hawajawahi kuweza kuacha woga wa kifo.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Only Those Who Revere God Are Happy

I

There lived a righteous man named Job, who always feared God and always shunned evil, his deeds praised by God, remembered by man. Job’s life had meaning, Job’s life had worth. Job was blessed by God, but he also was tested by Satan and tried by God. As he stood witness for God he feared, he deserved to be called a righteous man. Regardless of what Job had been through, his life was happy, there was no pain. Job was happy not only because he was blessed or commended by God, but also because of his pursuit, ’cause he pursued the reverence of God. Job was happy.

II

In the few decades after Job was tried, his life was more grounded and meaningful. He pursued belief and recognition and also submission to God’s sovereignty. All important junctures in Job’s life were marked by these pursuits and goals. With them he lived out his last years in peace, and greeted the end with happiness. Regardless of what Job had been through, his life was happy, there was no pain. Job was happy not only because he was blessed or commended by God, but also because of his pursuit, ’cause he pursued the reverence of God. Job was happy.

III

In seeking to fear God and to shun evil, Job had come to know God’s sovereignty. And in his experience of it, he realized how wondrous the Creator’s deeds were. Job was happy because of his association with God, his acquaintance with God, and the understanding between him and God. Job was happy. Job was happy not only because he was blessed or commended by God, but also because of his pursuit, ’cause he pursued the reverence of God. Job was happy. Job was happy because of the comfort and joy that came from knowing the Creator’s will, because of his fear after seeing how great, wondrous, lovable, and faithful God is. Job was happy.

from Follow the Lamb and Sing New Songs

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp