Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 467

02/11/2020

Roho Mtakatifu Anafanya kazi vipi katika kanisa sasa? Je, una ufahamu wa hilo? Ni matatizo gani makubwa zaidi yanayowakumba ndugu na dada? Wamepungukiwa na nini zaidi? Kwa sasa, kuna watu ambao wako hasi katikati ya majaribio, na wengine wao hata wanalalamika, na wengine hawasongi mbele tena kwa sababu Mungu Hazungumzi tena. Watu hawajaingia njia sahihi ya imani katika Mungu. Hawawezi kuishi wakijitegemea, na hawezi kudumisha maisha yao ya kiroho. Kuna watu wengine ambao wanafuata, wanaofuatilia kwa nguvu, na wako tayari kutenda Mungu Akinena. Lakini Mungu Asiponena, hawasongi mbele tena. Watu bado hawajaelewa mapenzi ya Mungu katika mioyo yao na hawana mapenzi kwa Mungu moja kwa moja; kufuata kwao Mungu hapo awali ilikuwa kwa sababu walikuwa wamelazimishwa. Sasa kuna watu ambao wamechoka na kazi ya Mungu. Je, hawako hatarini? Watu wengi wako katika hali ya kuvumilia tu. Ingawa wanakula na kunywa maneno ya Mungu na kumuomba, yote ni kwa kusitasita. Hawana bidii waliyokuwa nayo mwanzoni, na watu wengi hawana shauku katika kazi ya Mungu ya uboreshaji na ukamilisho. Ni kana kwamba hawana bidii ya ndani kamwe, na wanalemewa na maasi hawahisi kuwa wana deni kwa Mungu, wala hawajuti wenyewe. Hawaufuatilii ukweli ama kuondoka kanisani. Wanafuata tu raha za muda. Huyu ni aina ya mjinga mkuu wa kipumbavu! Wakati utakapofika, wote watatupwa nje, na hakuna mmoja atakayeokolewa! Je, unafikiri kuwa kama mtu ameokolewa mara moja ataokolewa kila wakati? Hii ni kujaribu tu kuwapumbaza watu! Wale wote wasiofuata kuingia katika maisha wataadibiwa. Watu wengi hawana shauku hata kidogo ya kuingia katika maisha, katika maono, ama kuweka ukweli katika matendo. Hawafuati kuingia ndani, na kwa hakika hawafuati kuingia ndani zaidi. Je, hawajiangamizi wenyewe? Wakati huu, kuna sehemu ya watu ambao hali zao zinaendelea kuwa nzuri na nzuri zaidi. Roho Mtakatifu Anapofanya kazi zaidi, wanajiamini zaidi, na wanapozoea zaidi ndipo wanapohisi siri ya kushangaza ya kazi ya Mungu. Wanapoingia ndani zaidi, ndipo wanaelewa zaidi. Wanahisi kuwa upendo wa Mungu ni mkubwa sana, na wanahisi imara na kupata nuru ndani. Wana uelewa wa kazi ya Mungu. Hawa ni watu ambao Roho Mtakatifu Anafanya kazi ndani yao. Watu wengine wanasema, “Ingawa hakuna maneno mapya kutoka kwa Mungu, lazima bado niendelee kuingia ndani katika ukweli, lazima niwe na bidii katika kila kitu katika mazoea yangu na kuingia katika ukweli wa maneno ya Mungu.” Mtu kama huyu ana kazi ya Roho Mtakatifu. Ingawa Mungu Haonyeshi uso Wake na Amejifichika kutoka kwa kila mtu, na Haneni neno lolote, na kuna nyakati ambazo watu wanapitia usafishaji wa ndani, ilhali Mungu hajawaacha watu Wake kabisa. Kama mtu hawezi kudumisha ukweli ambao anafaa kutekeleza, hatakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu. Katika wakati wa usafishaji, wa Mungu kutojionyesha, kama hujiamini na unaogopa, usipo lenga kuwa na uzoefu wa maneno Yake, hii ni kutoroka kutoka kwa kazi ya Mungu. Baadaye, utatupwa nje. Wale ambao hawatafuti kuingia katika neno la Mungu hawana uwezo wa kusimama kama shahidi Wake. Watu ambao wanaweza kutoa ushahidi kwa Mungu na kuridhisha mapenzi Yake wote wanategemea kikamilifu bidii yao kufuatilia maneno ya Mungu. Kazi ambayo Mungu Anaitekeleza katika watu ni kimsingi kuwawezesha kuupata ukweli; Kukufanya wewe kufuatilia maisha ni kwa ajili ya kukukamilisha, na yote ni ya kukufanya ufae kutumika na Mungu. Yote unayofuata sasa ni kusikia siri, kusikiliza maneno ya Mungu, kulisha macho yako, kuona kitu kipya ama kuona ni mwenendo upi, na kuridhisha udadisi wako. Kama hii ndio nia ya moyo wako, hakuna vile utafikia mahitaji ya Mungu. Wale ambao hawafuati ukweli hawezi kufuata mpaka mwisho kabisa. Wakati huu, si kwamba Mungu hafanyi kitu—ni kwamba watu hawashirikiani, kwa sababu wamechoka na kazi Yake. Wanataka tu kusikia maneno ya baraka Yake, na hawataki kusikia maneno ya hukumu Yake na kuadibiwa. Sababu ya hii ni nini? Ni kwa sababu tamaa ya watu kupata baraka haijatimizwa, na wako hasi na wanyonge. Si kwamba Mungu kimakusudi hakubali watu kumfuata, na si kwamba anapeana mapigo kimakusudi kwa wanadamu. Watu wako hasi na wanyonge kwa sababu nia zao hazifai. Mungu ni Mungu Ambaye Anampa mwanadamu maisha, naye hawezi kumleta mwanadamu katika kifo. Uhasi wa watu, unyonge na kurudi nyuma yote yanasababishwa na wao wenyewe.

Kazi ya Mungu ya sasa inawaletea watu usafishaji kiasi, na wale tu ambao wanaweza kusimama imara katika usafishaji huu watapata kibali cha Mungu. Haijalishi ni jinsi gani Anajificha, bila kuongea, ama kufanya kazi, bado unaweza kufuata kwa bidii. Hata kama Mungu Alisema angekukataa, bado ungemfuata Yeye. Hii ni kusimama kama shahidi kwa Mungu. Mungu Akijificha kutoka kwako nawe ukome kumfuata, hii ni kusimama shahidi kwa Mungu? Watu wasipoingia ndani kwa kweli, hawana kimo cha kweli, na wanapokabiliana na jaribio kubwa hasa, wanaanguka. Mungu haneni kwa sasa, ama kile Afanyacho hakilingani na dhana zako, kwa hivyo hauko sawa. Kama Mungu angekuwa sasa anatenda kulingana na dhana zako kwa sasa, kama Angekuwa anayakidhi matakwa yako na ukawa na uwezo wa kusimama na kufuatilia kwa nguvu, basi ni nini ambacho kweli ungekuwa unatumia kuendelea kuishi? Nasema kuwa kuna watu wengi ambao wanaishi wakitegemea kabisa udadisi wa binadamu. Hawana kabisa moyo wa kweli wa kufuata. Wale wote wasiofuata kuingia katika ukweli lakini wanategemea udadisi wao katika maisha ni watu wenye kustahili dharau walio hatarini! Kazi za Mungu tofauti yote ni ya kuwakamilisha wanadamu. Hata hivyo, watu daima ni wadadisi, wanapenda kuuliza kuhusu tetesi, wana wasiwasi kuhusu kinacho endelea nje ya nchi—ni nini kinaendelea Israeli, kama kuna mtetemeko wa ardhi Misri—kila wakati wanatafuta kitu mpya, kitu kisicho cha kawaida kuridhisha tamaa zao za kibinafsi. Hawafuati maisha, wala kufuata kukamilishwa. Wanatafuta tu siku ya Mungu kufika haraka ili ndoto yao nzuri ijulikane na tamaa zao badhirifu zitimie. Mtu kama huyo si wa kweli—ni mtu aliye na mtazamo usio sawa. Kuufuata ukweli ni msingi wa imani ya wanadamu katika Mungu. Watu wasipofuata kuingia katika maisha, wasipotafuta kumridhisha Mungu, basi watatiishwa chini ya adhabu. Wale watakaoadhibiwa ni wale ambao hawajakuwa na kazi ya Roho Mtakatifu katika wakati wa kazi ya Mungu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp