Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kumjua Mungu | Dondoo 16

Mwelekeo wa Mungu kwa Wale Wanaotoroka Wakati Kazi Yake Inaendelea

Utampata mtu wa aina hii kila pahali: Baada ya kuwa na hakika kuhusu njia ya Mungu, kwa sababu mbalimbali, wanaondoka kimyakimya bila ya neno la kwaheri na kufanya chochote kile ambacho moyo wao unatamani. Huku haya yakiendelea, hatutaingilia kwa nini mtu huyu anaondoka. Kwanza tutaangalia mwelekeo wa Mungu ni upi kwa mtu wa aina hii. Iko wazi sana! Tangu muda ule ambao mtu huyu huondoka, machoni mwa Mungu, kile kipindi cha imani yao kimekwisha. Si mtu huyu aliyekimaliza, bali ni Mungu. Kwamba mtu huyu alimwacha Mungu inamaanisha kwamba tayari amemkataa Mungu, kwamba tayari hamtaki Mungu. Inamaanisha kwamba tayari hakubali wokovu wa Mungu. Kwa sababu mtu huyu hamtaki Mungu, Mungu naye anaweza bado kumtaka? Aidha wakati mtu huyu anao mwelekeo huu, mtazamo huu, na anayo azma ya kumwacha Mungu, tayari ameikera tabia ya Mungu. Hata ingawa hawakujipata wakiwa na hasira na wakalaani Mungu, hata ingawa hawakujihusisha katika uovu wowote au tabia au utovu wa nidhamu, na hata ingawa mtu huyu hafikirii: Kama kutawahi kuwepo na siku nitakapokuwa nimeshiba anasa zangu kwa nje, au nitakapokuwa bado nahitaji kitu kutoka kwa Mungu, nitarudi. Au kama Mungu ataniita, nitarudi. Au wanasema: Kama nitajeruhiwa kwa nje, nikiuona ulimwengu wa nje una giza sana na una maovu sana na sitaki tena kujishirikisha nao, nitarudi kwa Mungu. Hata ingawa mtu huyu amepiga hesabu katika akili zake ni wakati gani anarudi, hata ingawa wanauacha mlango ukiwa wazi wa kurudi kwao, hawatambui kwamba bila kujali ni namna gani wanavyofikiria na namna gani wanavyopanga, hii ni ndoto tu. Kosa lao kubwa zaidi ni kutokuwa wazi kuhusu namna ambavyo Mungu anahisi wakati wanapotaka kuondoka. Kuanzia muda ule ambao mtu huyu anaamua kumwacha Mungu, Mungu amemwacha kabisa; tayari Mungu ameanzisha matokeo katika moyo Wake. Matokeo hayo ni yapi? Kwamba mtu huyu ni mmoja wa buku, na ataangamia pamoja nao. Hivyo basi, watu mara nyingi huona aina hii ya hali: Mtu anamwacha Mungu, lakini hapokei adhabu yoyote. Mungu hufanya kazi kulingana na kanuni Zake binafsi. Watu wanaweza kuona baadhi ya mambo, na baadhi ya mambo yanahitimishwa tu katika moyo wa Mungu, kwa hivyo watu hawawezi kuyaona matokeo. Kile ambacho watu huona si lazima kiwe ndio upande wa ukweli wa mambo; lakini upande ule mwingine, ule upande usiouona—hizi ndizo fikira na hitimisho la kweli kuhusu moyo wa Mungu.

Watu Wanaotoroka Wakati wa Kazi ya Mungu ni Wale Wanaoiacha Njia ya Kweli

Hivyo basi kwa nini Mungu ampe mtu wa aina hii adhabu kali kama hiyo? Kwa nini Mungu anakuwa na hasira kali kwao? Kwanza kabisa tunajua kwamba tabia ya Mungu ni adhama, ni hasira. Yeye si kondoo ili achinjwe na yeyote; na hata zaidi Yeye si kikaragosi ili adhibitiwe na watu vyovyote vile wanavyotaka. Yeye pia si hewa tupu ili kuamrishwa huku na kule na watu. Kama kweli unasadiki kwamba Mungu yupo, unafaa kuwa na moyo unaomcha Mungu, na unafaa kujua kwamba kiini halisi cha Mungu hakifai kughadhabishwa. Ghadhabu hii inaweza kusababishwa na neno; pengine fikira; pengine aina fulani ya tabia bovu; pengine tabia ya upole tabia inayoweza kuruhusiwa kwenye macho na maadili ya binadamu; au pengine inasababishwa na falsafa, nadharia. Hata hivyo, punde unapomghadhabisha Mungu, fursa yako inapotea na siku zako za mwisho zinakuwa zimewasili. Hili ni jambo baya! Kama huelewi kwamba Mungu hawezi kukosewa, basi pengine humchi Mungu, na pengine unamkosea Yeye kila wakati. Kama hujui namna ya kumcha Mungu, basi huwezi kumcha Mungu, na hujui namna ya kujiweka kwenye njia ya kutembelea kwa njia ya Mungu—kumcha Mungu na kujiepusha na maovu. Punde unapokuwa na habari, unaweza kuwa na ufahamu kwamba Mungu hawezi kukosewa, kisha utajua ni nini maana ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu.

Kutembea katika njia ya kumcha Mungu na kujiepusha na maovu si lazima kuumaanishe ni kiwango kipi cha ukweli unachojua, ni majaribio mangapi ambayo umepitia, au ni mitihani mingapi ambayo umepitia na kutiwa adabu. Badala yake, kunategemea na kiini halisi cha moyo wako kumhusu Mungu, na mwelekeo wako kwa Mungu pia. Kiini halisi cha watu na mielekeo yao ya kibinafsi—mambo haya ni muhimu sana, muhimu kabisa. Kuhusiana na wale watu ambao wamemkana na kumwacha Mungu, mwelekeo wao wa dharau kwa Mungu na mioyo yao inayodharau ukweli ulikera tabia ya Mungu, hivyo basi kulingana na Mungu hawatawahi kusamehewa. Wamejua kuhusu uwepo wa Mungu, wamekuwa na taarifa kwamba Mungu tayari amewasili, wameweza hata kupitia kazi mpya ya Mungu. Kuondoka kwao si kutokana na kudanganywa, wala si suala kwamba wao wamechanganyikiwa kulihusu. Hata si suala hata kidogo la wao kulazimishwa kuondoka. Lakini kwa nadhari yao, na kwa akili iliyo wazi, wamechagua kumwacha Mungu. Kuondoka kwao si kupotea kwao; si hata kutupwa kwao nje. Hivyo basi, katika macho ya Mungu, wao si kondoo aliyepotea njia kutoka kwenye kondoo wale wengine, sikuambii hata mtoto wa kiume mbadhirifu aliyepotea njia yake. Waliondoka bila hofu ya kuadhibiwa, na hali kama hiyo, mfano kama huo unaikera tabia ya Mungu na ni kutokana na kero hili ambapo Yeye huwapa matokeo yasiyo na matumaini. Je, huoni kwamba matokeo kama haya yanatisha? Hivyo basi kama watu hawamjui Mungu, wanaweza kumkosea Mungu. Hilo ni suala dogo! Kama mtu hatachukulia mwelekeo wa Mungu kwa umakinifu, na bado anasadiki kwamba Mungu angali anatarajia kurudi kwake—kwa sababu wao ni mojawapo wa kondoo wa Mungu waliopotea na kwamba Mungu angali anawasubiria kubadilisha moyo wao—basi mtu huyu hayupo mbali sana na kuweza kuondolewa kwenye siku yake ya adhabu. Mungu hatakataa tu kumkaribisha. Hii ndiyo mara yake ya pili ya kuikera tabia ya Mungu; hivyo basi suala hili ni baya zaidi! Mwelekeo wa mtu huyu usioheshimu vitu vitakatifu tayari umekosea agizo la kiutawala la Mungu. Bado Mungu atawakaribisha? Kanuni za Mungu kuhusiana na suala hili ni: Kama mtu amekuwa na hakika kuhusu njia ya kweli ilhali anaweza bado kwa nadhari yake na kwa akili wazi kumkataa Mungu, na kuwa mbali na Mungu, basi Mungu atazuia kabisa barabara iendayo katika wokovu wake, na hata lango la kuingia kwenye ufalme watafungiwa. Wakati mtu huyu atakapokuja kubisha kwa mara nyingine, Mungu hatamfungulia lango. Mtu huyu atafungiwa milele. Pengine baadhi yenu mmeisoma hadithi hii ya Musa kwenye Biblia. Baada ya Musa kupakwa mafuta na Mungu, viongozi 250 hawakutosheka na Musa kwa sababu ya hatua zake na sababu zingine mbalimbali. Ni nani waliyekataa kumtii? Hakuwa Musa. Walikataa kutii mipango ya Mungu; walikataa kutii kazi ya Mungu katika suala hili. Walisema yafuatayo: “Ninyi mnachukua mengi kwenu, kwa sababu mkusanyiko wote ni mtakatifu, kila mmoja wao, naye Yehova yuko miongoni mwao….” Katika macho yenu, maneno haya ni mazito? Si mazito! Angaa maana ya moja kwa moja ya maneno haya si mazito. Katika mkondo wa kisheria, hawavunji sheria zozote, kwa sababu kwenye sehemu ya juu kabisa si lugha katili, au msamiati, isitoshe, hayana maana yoyote ya kukufuru. Sentensi ya kawaida ndiyo iliyo hapo, hamna cha ziada. Ilhali inakuwaje kwamba maneno haya yanaweza kuanzisha hasira kali kama hiyo kutoka kwa Mungu? Ni kwa sababu hayasemwi kwa watu, mbali kwa Mungu. Mwelekeo na tabia iliyoelezewa na wao ndicho hasa kinachoikera tabia ya Mungu, hasa ile tabia ya Mungu ambayo haiwezi kukosewa. Sote tunajua matokeo yao hatimaye yalikuwa yapi. Kuhusiana na wale waliomwacha Mungu, mtazamo wao ni upi? Mwelekeo wao ni upi? Na ni kwa nini mtazamo na mwelekeo wao unasababisha Mungu kuwashughulikia kwa njia hiyo? Sababu ni kwamba wanajua waziwazi Yeye ni Mungu ilhali bado wanachagua kumsaliti Yeye. Na ndiyo maana wanaondolewa kabisa fursa yao ya wokovu. Kama vile Biblia inavyosema: “Kwa sababu tukitenda dhambi makusudi baada ya sisi kupokea maarifa ya ukweli, hakuna tena dhabihu ya dhambi.” Je, mmelielewa suala hili sasa?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Maudhui Yanayohusiana

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp