Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 461

22/09/2020

Siku hizi, watu wengi hawatilii maanani ni mafunzo yapi wanayopaswa kupata wakati wanaposhirikiana na wengine. Nimegundua kwamba wengi wenu hawawezi kupata mafunzo hata kidogo wakati wanaposhirikiana na wengine; wengi wenu huyashikilia maoni yenu wenyewe. Unapofanya kazi kanisani, unatoa maoni yako na mtu mwingine anatoa yake, na maoni hayo hayana uhusiano; kwa kweli hamshirikiani hata kidogo. Ninyi nyote mnajishughulisha sana na kuwasiliana tu kuhusu utambuzi wenu wenyewe ama kuachilia “mizigo” mliyoibeba ndani yenu, bila kutafuta uzima kwa namna yoyote ile. Unaonekana kufanya kazi kwa njia ya uzembe tu, daima ukiamini kwamba unapaswa kuitembea njia yako mwenyewe bila kujali kile ambacho mtu mwingine anasema ama kufanya; unafikiria kwamba unapaswa kushiriki jinsi Roho Mtakatifu anavyokuongoza, bila kujali hali za wengine zinaweza kuwa zipi. Hamwezi kugundua uwezo wa wengine, na wala hamwezi kujichunguza. Kukubali kwenu mambo kumepotoka na kuna makosa sana. Inaweza kusemwa kwamba hata sasa bado mnaonyesha unyoofu mwingi, kana kwamba mmerudia ugonjwa huo wa zamani. Kwa mfano, hamwasiliani kwa njia inayofanikisha uwazi kamili, kwa mfano, kuhusu aina ya matokeo ambayo mmepata kutoka kwa kazi katika makanisa fulani, ama kuhusu hali zako za ndani za siku hizi na kadhalika; kamwe hamwasiliani hata kidogo kuhusu mambo kama hayo. Hamshiriki hata kidogo katika vitendo kama kuyaacha mawazo yenu wenyewe ama kujikana. Viongozi na wafanyakazi wanafikiri tu kuhusu jinsi ya kuwazuia ndugu zao wasiwe hasi na jinsi ya kuwafanya waweze kufuata kwa juhudi. Hata hivyo, ninyi nyote mnafikiri kwamba kufuata kwa juhudi pekee kunatosha, na kimsingi, hamwelewi maana ya kujijua na kujikana, sembuse kuelewa maana ya kuhudumu kwa kushirikiana na wengine. Mnafikiri tu kuhusu ninyi wenyewe kuwa na nia ya kuulipiza upendo wa Mungu, kuhusu ninyi wenyewe kutaka kuishi kwa kudhihirisha mtindo wa Petro. Hamfikirii kuhusu kitu kingine isipokuwa mambo haya. Hata unasema kwamba bila kujali yale watu wengine wanayofanya, hutatii bila kufikiria, na kwamba bila kujali jinsi watu wengine walivyo, wewe mwenyewe utatafuta kukamilishwa na Mungu, na hiyo itatosha. Hata hivyo, ukweli ni kwamba kutaka kwako hakujapata maonyesho thabiti kwa kweli. Je, haya yote sio mwenendo ambao mnadhihirisha siku hizi? Kila mmoja wenu anashikilia utambuzi wake mwenyewe, na nyote mnatamani kukamilishwa. Naona kwamba mmehudumu kwa muda mrefu sana bila kufanya maendeleo mengi; hasa katika funzo hili la kufanya kazi pamoja kwa upatanifu, hamjafanikisha chochote hata kidogo! Unapokwenda katika makanisa unawasiliana kwa njia yako, na wengine wanawasiliana kwa njia zao. Ushirikiano wa upatanifu unafanyika mara chache sana, na hili ni kweli hata zaidi kwa wafuasi walio chini yako. Yaani, ni mara chache ambapo yeyote kati yenu anaelewa maana ya kumhudumia Mungu, ama jinsi mtu anavyopaswa kumhudumia Mungu. Mmekanganyikiwa na mnayachukulia mafunzo ya aina hii kama mambo madogo. Hata kuna watu wengi ambao hawakosi kutenda kipengele hiki cha ukweli tu, lakini ambao pia wanafanya makosa kwa makusudi. Hata wale ambao wamehudumu kwa miaka mingi wanapigana na kupangiana njama nao ni wenye wivu na wenye kupenda kushindana; ni kila mtu na wake, na hawashirikiani hata kidogo. Je, mambo haya yote hayawakilishi kimo chenu cha kweli? Ninyi watu mnaohudumu pamoja kila siku ni kama Waisraeli, ambao kila siku walimhudumia Mungu Mwenyewe moja kwa moja hekaluni. Inawezekanaje kwamba ninyi watu, mnaomhudumia Mungu, hamjui jinsi ya kushirikiana ama jinsi ya kuhudumu?

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Hudumu Jinsi Waisraeli Walivyohudumu

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp