Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 470

21/10/2020

Kwa kila hatua ya kazi ya Mungu, kunayo njia ambayo watu wanapaswa washirikiane. Mungu Anawasafisha watu ili wawe na imani katikati ya usafishaji. Mungu Anawakamilisha watu ili wawe na imani ya kukamilishwa na Mungu na wako tayari kuukubali usafishaji Wake na kushughulikiwa na kupogolewa na Mungu. Roho wa Mungu Anafanya kazi ndani ya watu ili kuwaletea nuru na mwangaza, na kuwafanya washirikiane Naye na kutenda. Mungu Haneni wakati wa usafishaji. Hatoi sauti Yake, lakini bado kuna kazi ambayo watu wanapaswa kuifanya. Unapaswa kushikilia kile ambacho unacho tayari, unapaswa bado kuwa na uwezo wa kumwomba Mungu, kuwa karibu na Mungu, na kusimama shahidi mbele ya Mungu; hivi utatimiza wajibu wako mwenyewe. Nyinyi wote mnapaswa muone kwa dhahiri kutoka kwa kazi ya Mungu kuwa majaribu Yake ya imani ya watu na upendo inahitaji kuwa waombe zaidi kwa Mungu, na kwamba waonje maneno ya Mungu mbele Zake mara kwa mara. Mungu Akikupa nuru na kukufanya kuelewa mapenzi Yake lakini huyaweki katika matendo hata kidogo, hutapata chochote. Unapoyaweka maneno ya Mungu katika matendo, unapaswa bado kuwa na uwezo wa kumwomba, na unapoyaonja maneno Yake unapaswa utafute kila wakati mbele Zake na uwe umejaa imani Kwake bila kuvunjika moyo ama kuwa baridi. Wale wasioweka maneno ya Mungu katika matendo wamejawa na nguvu katika mikusanyiko, lakini wanaanguka katika giza wanaporudi nyumbani. Kuna wengine ambao hawataki hata kukusanyika pamoja. Kwa hivyo lazima uone kwa wazi ni wajibu gani ambao watu wanapaswa kutimiza. Unaweza kukosa kujua mapenzi ya Mungu ni nini hasa, lakini unaweza kutekeleza wajibu wako, unaweza kuomba inapopaswa, unaweza kuuweka ukweli katika matendo unapopaswa, na unaweza kufanya kile watu wanapaswa kufanya. Unaweza kushikilia maono yako asili. Hivi, utaweza kukubali zaidi hatua ya Mungu inayofuata. Ni shida ukikosa kutafuta wakati ambapo Mungu anafanya kazi katika njia iliyofichika. Anaponena na kuhubiri katika mabaraza, unasikiza kwa shauku, lakini Asiponena unakosa nguvu na kurudi nyuma. Mtu wa aina gani anafanya hivi? Huyu ni mtu ambaye tu anaenda na mkondo. Hana msimamo, hawana ushuhuda, na hawana maono! Watu wengi wako hivyo. Ukiendelea katika njia hiyo, siku moja utakapopitia jaribio kuu, utateremka katika adhabu. Kuwa na msimamo ni muhimu sana katika kukamilishwa kwa watu na Mungu. Kama huna shaka na hatua yoyote ya kazi ya Mungu, unatimiza wajibu ya mwanadamu, unashikilia kwa uaminifu kile Mungu Amekufanya ukiweke katika matendo, hiyo ni, unakumbuka mawaidha ya Mungu, na haijalishi Anachokifanya sasa husahau mawaidha Yake, huna shaka kuhusu kazi Yake, unadumisha msimamo wako, kushikilia ushahidi wako, na una ushindi katika kila hatua ya njia, mwishowe utakamilishwa kuwa mshindi na Mungu. Kama unaweza kusimama imara katika kila hatua ya majaribu ya Mungu, na bado unaweza kusimama imara hadi mwisho kabisa, wewe ni mshindi, na wewe ni mtu ambaye amekamilishwa na Mungu. Kama huwezi kusimama imara katika majaribu yako ya sasa, baadaye itakuwa hata vigumu zaidi. Ukipitia mateso kidogo yasiyo ya muhimu na usiufuate ukweli, hutapata chochote mwishowe. Utakuwa mkono mtupu. Kuna watu wengine ambao wanaacha kufuata wanapoona kuwa Mungu Haneni, na moyo wao unatawanyika. Je, si huyo ni mjinga? Watu wa aina hii hawana ukweli. Mungu Anenapo, wanakimbia huku na kule kila wakati, wakiwa na shughuli nyingi na kuwa na shauku kwa nje, lakini sasa Haneni, hawatafuti tena. Mtu kama huyu hana maisha ya usoni. Katika usafishaji, lazima uingie ndani kutoka kwa mtazamo halisi na usome masomo unayostahili kusoma; unapomwomba Mungu na kusoma neno Lake, unapaswa kulinganisha hali yako mwenyewe nayo, utambue pungufu zako, na ujue kuwa una somo mengi sana unayofaa kusoma. Unapotafuta kwa uaminifu katikati ya usafishaji, ndipo utakapojipata kuwa una pungufu. Unapokuwa unapitia usafishaji kunayo masuala mengi ambayo unapitia; hautayaona kwa wazi, unalalamika, unatambulisha mwili wako wenyewe—ni kwa njia hii pekee ndiyo unaweza kugundua kwamba una tabia nyingi sana potovu ndani yako.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp