Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 553

05/11/2020

Kazi hii miongoni mwenu inatekelezwa kwenu kulingana na ile kazi inayohitajika kufanywa. Baada ya ushindi wa watu hawa binafsi, kundi la watu litafanywa kuwa timilifu. Kwa hivyo, wingi wa kazi ya sasa umo katika matayarisho ya shabaha ya kuwafanya kuwa watimilifu, kwa sababu wapo wengi sana wanaohitaji kuupata ukweli na ambao wanaweza kufanywa kuwa watimilifu. Kama kazi ya ushindi itatekelezwa kwenu na baadaye hakuna kazi ya ziada itakayofanywa, basi si ni kweli kwamba baadhi ya wale wanaotamani ukweli hawataupata? Kazi ya sasa inalenga kufungua njia ya kuwafanya watu kuwa watimilifu baadaye. Ingawa kazi Yangu ni ya ushindi tu, njia ya maisha iliyotamkwa na Mimi bila shaka ni katika matayarisho ya kuwafanya watu kuwa watimilifu baadaye. Kazi inayokuja baada ya ushindi inatilia maanani kuwafanya watu kuwa watimilifu, na hivyo basi ushindi unafanywa ili kuweka msingi wa kule kufanywa kuwa watimilifu. Binadamu anaweza kufanywa kuwa mtimilifu tu baada ya kushindwa. Sasa hivi kazi kuu ni kushinda; baadaye wale wanaotafuta na kutamani ukweli watafanywa kuwa watimilifu. Kufanywa kuwa mtimilifu kunahusisha dhana nzuri za watu kuhusu maisha: Je, unao moyo unaopenda Mungu? Kina cha yale umepitia ulipotembea kwenye njia hii ni kipi? Upendo wako katika Mungu ni safi vipi? Mwenendo wako wa ukweli ni mpevu kiasi kipi? Ili kufanywa kuwa mtimilifu, lazima mtu awe na maarifa ya kimsingi ya dhana zote za ubinadamu. Hili ni hitaji la kimsingi. Wale wote wasioweza kufanywa kuwa watimilifu baada ya kushindwa hugeuka na kuwa vifaa vya kuhudumu na hatimaye bado watatupwa kwenye ziwa la moto na kibiriti na bado wataanguka kwenye lile shimo lisilokuwa na mwisho kwa sababu ya tabia yao ambayo haijabadilika na wangali watakuwa wa Shetani. Kama mtu atakosa sifa za kufuzu za kuwa mtimilifu, basi yeye ni bure bilashi—hana manufaa, ni chombo, kitu ambacho hakiwezi kustahimili majaribio ya moto! Upendo wako kwa Mungu sasa hivi ni mkubwa vipi? Chukizo lako kwa nafsi yako ni kubwa kiasi kipi? Unamjua Shetani kwa mapana yapi? Umelegeza uamuzi wenu? Maisha yenu katika ubinadamu yamethibitiwa vyema? Maisha yenu yamebadilika? Unayaishi maisha mapya? Mtazamo wenu wa maisha umebadilika? Kama mambo haya hayajabadilika, huwezi kufanywa kuwa mtimilifu hata kama hutabadilisha mwenendo; badala yake, wewe umeshindwa tu. Wakati ukifika wa kukujaribu, unakosa ukweli, ubinadamu wako si wa kawaida, na wewe ni wa kiwango cha chini kama mnyama. Umeshindwa tu, wewe ndiwe umeshindwa tu na Mimi. Kama vile tu, punde punda anapopitia mjeledi wa mmiliki wake, yeye huwa na woga na wasiwasi wa kufanya chochote kila wakati anapomwona bwana wake, ndivyo pia, wewe ulivyo kama punda huyo aliyeshindwa. Kama mtu atakosa vipengele hivyo vizuri na badala yake yeye ni wa kutoonyesha hisia na mwenye wasiwasi, mwepesi kutishwa na wa kusitasita katika mambo yote, asiyeweza kutambua chochote kwa njia iliyo wazi, asiyeweza kukubali ukweli, ambaye bado hana njia ya kuendeleza mwenendo wake, na hata zaidi asiye na moyo wa upendo wa Mungu—kama mtu hana uelewa wa namna ya kumpenda Mungu, namna ya kuishi maisha yenye maana, au namna ya kuwa mtu halisi—mtu kama huyu anawezaje kumshuhudia Mungu? Hii inaonyesha kwamba maisha yako yanayo thamani ndogo na wewe si kingine ila punda aliyeshindwa. Wewe umeshindwa, lakini hilo linamaanisha tu kwamba umelikataa lile joka kubwa jekundu na umekataa kunyenyekea katika uwanja wake; hiyo inamaanisha kwamba wewe unaamini kuwa kunaye Mungu, unataka kutii mipango yote ya Mungu na huna malalamiko yoyote. Lakini je, dhana zile ni nzuri? Uwezo wa maisha ya kudhihirisha neno la Mungu, uwezo wa kumdhihirisha Mungu—huna vyote hivi, kumaanisha bado hujamilikiwa na Mungu, na kwamba wewe si mwengine ila punda aliyeshindwa. Hakuna chochote cha kutamanika ndani yako, na Roho Mtakatifu hayumo kazini ndani yako. Ubinadamu wako unakosa mengi na haiwezekani Mungu kukutumia. Lazima uidhinishwe na Mungu na kuwa mara mia moja bora zaidi kuliko wanyama wale wasioamini na kuliko wale wanaotembea wakiwa wamekufa—wale tu wanaofikia kiwango hiki ndio wanaofuzu kufanywa kuwa watimilifu. Pale tu ambapo mtu anao wema na utu na dhamiri ndipo anapofaa kutumiwa na Mungu. Pale ambapo tu mnafanywa kuwa watimilifu ndipo mtakapochukuliwa kuwa binadamu. Wale waliofanywa kuwa watimilifu tu ndio wale wanaoishi maisha yenye maana. Watu kama hawa tu ndio wanaoweza kushuhudia hata vizuri zaidi kuhusu Mungu.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Wale Waliokamilishwa Pekee Ndio Wanaoweza Kuishi Maisha Yenye Maana

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp