Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 335

01/09/2020

Hatima yenu na majaliwa yenu ni muhimu sana kwenu—ni za matatizo makubwa. Mnaamini kuwa msipofanya mambo kwa uangalifu sana, itakuwa sawa na kutokuwa na hatima, na uharibifu wa majaliwa yenu. Lakini mmewahi kufikiri kwamba kama juhudi mtu hutumia ni kwa ajili ya hatima zao tu, hizo ni kazi tu zisizo na matunda? Juhudi za aina hiyo si halisi—ni bandia na danganyifu. Kama ni hivyo, wale ambao wanafanya kazi kwa ajili ya hatima yao watapokea maangamizo yao ya mwisho, kwa sababu kushindwa katika imani ya watu katika Mungu hutendeka kwa sababu ya udanganyifu. Hapo awali Nilisema kuwa Mimi Sipendi kusifiwa mno au kupendekezwa, au kuchukuliwa kwa shauku. Ninapenda watu waaminifu kukubali hali ilivyo kuhusu ukweli na matarajio Yangu. Hata zaidi, Ninapenda wakati watu wanaweza kuonyesha uangalifu mkubwa na kufikiria kwa ajili ya moyo Wangu, na wakati wanaweza hata salimisha kila kitu kwa ajili Yangu. Ni kwa njia hii tu ndipo Moyo wangu unaweza kuliwazwa. Sasa hivi, ni mambo mangapi yapo yanayowahusu ambayo Mimi Nachukia? Ni mambo mangapi yapo yanayowahusu ambayo Napenda? Je, hakuna kati yenu ambaye ametambua ubaya wote ambao mmeonyesha kwa ajili ya hatima zenu?

Katika moyo Wangu, Sitaki kuwa Mwenye kudhuru moyo wowote ambao ni chanya na wa motisha, na Mimi hasa Sitaki kupunguza bidii ya mtu yeyote ambaye anafanya wajibu wake kwa uaminifu; hata hivyo, ni lazima Niwakumbushe kila mmoja wenu juu ya upungufu wenu na roho chafu sana ndani ya mioyo yenu. Azma ya kufanya hivyo ni kutarajia kwamba mtaweza kutoa mioyo yenu ya kweli katika kukabiliana na maneno Yangu, kwa sababu kile Nachukia zaidi ni udanganyifu wa watu kuelekezwa Kwangu. Natarajia tu kuwa katika hatua ya mwisho ya kazi Yangu, mnaweza kutekeleza kwa kujitokeza, kujitoa kikamilifu, na wala sio shingo upande tena. Bila shaka, Natarajia pia kuwa nyote muwe na hatima nzuri. Hata hivyo, bado Nina mahitaji Yangu ambayo ni kwenu nyinyi mfanye uamuzi bora kabisa katika kujitoa Kwangu pekee na moyo wa ibada ya mwisho. Kama mtu hana moyo huo wa ibada pekee, mtu huyo hakika atakwenda kuwa thamani ya Shetani, na Mimi Sitaendelea kumtumia. Nitamtuma nyumbani akatunzwe na wazazi wake. Kazi yangu imekuwa ya msaada sana kwa ajili yenu; kile Natarajia kupata kutoka kwenu ni moyo ulio mwaminifu na unaotia msukumo kwenda juu, lakini hadi sasa mikono Yangu bado ni tupu. Fikiria kulihusu: Wakati siku moja bado Nitakuwa na kukwazika kusikoelezeka, mtazamo Wangu kuwaelekea utakuwa upi? Je, Mimi bado Nitakuwa mwema? Je, Moyo wangu utakuwa bado mtulivu? Je, mnaelewa hisia za mtu ambaye kwa kujitahidi amelima lakini hakuvuna hata nafaka moja? Je, mnaelewa ukubwa wa jeraha la mtu ambaye amepigwa kipigo kikubwa? Je, mnaweza kuonja uchungu wa mtu aliyejawa na matumaini ambaye anafaa kuachana na mtu kwa uhusiano mbaya? Je, mmeona hasira ya mtu ambaye amekasirishwa? Je, mnaweza kujua hisia ya kulipiza kisasi kwa haraka ya mtu ambaye amekuwa akichukuliwa kwa uadui na udanganyifu? Kama mnaelewa fikira za watu hawa, Nadhani haipaswi kuwa vigumu kwenu kuwaza mtazamo Mungu Atakuwa nao wakati ule wa adhabu Yake. Hatimaye, Natarajia nyote mnaweka jitihada kali kwa ajili ya hatima yenu wenyewe; hata hivyo, ni bora msitumie njia za udanganyifu katika juhudi zenu, au bado Nitasikitishwa nanyi katika moyo Wangu. Je, kusikitishwa kwa aina hii huelekea wapi? Je, hamjidanganyi wenyewe? Wale ambao hufikiria kuhusu hatima yao na bado wanaiharibu ni watu wenye uwezekano mdogo zaidi wa kuokolewa. Hata kama watu hawa watakerwa, ni nani atawahurumia? Kwa jumla, bado Niko tayari Kuwatakia muwe na hatima inayofaa na nzuri. Hata zaidi, Natarajia kwamba hakuna kati yenu atakayeanguka katika maafa.

Neno, Vol. 1. Kuonekana na Kazi ya Mungu. Juu ya Hatima

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp