Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 359

18/09/2020

Tabia ambayo haiwezi kunitii kabisa ni usaliti. Mwenendo ambao hauwezi kuwa mwaminifu Kwangu ni usaliti. Kunidanganya na kutumia uongo kunilaghai ni usaliti. Kujawa na dhana na kuzieneza kila mahali ni usaliti. Kutozilinda shuhuda na maslahi Yangu ni usaliti. Kubuni tabasamu wakati mtu ameniacha moyoni mwake ni usaliti. Tabia hizi ni mambo yote ambayo daima mna uwezo wa kuyafanya, na pia ni za kawaida kati yenu. Hakuna mmoja wenu anayeweza kufikiri kwamba hilo ni tatizo, lakini Mimi sifikirii hivyo. Siwezi kuchukulia kunisaliti kama jambo dogo, na zaidi ya hayo siwezi kulipuuza. Nafanya kazi miongoni mwenu sasa lakini bado mko hivi. Kama siku moja hakutakuwa na mtu wa kuwalinda na kuwaangalia, si nyote mtakuwa wafalme wa kilima? Kwa wakati huo, nani atavisafisha vitu tena na kuondoa uchafu mnaposababisha janga kubwa? Mnaweza kufikiri kwamba baadhi ya vitendo vya usaliti ni kitu cha mara moja tu badala ya tabia ya kuendelea, na hakipaswi kutajwa kwa uzito hivi, kikiwasababisha kuadhirika. Kama kweli mnaamini hivyo, basi mnakosa wepesi wa kuhisi. Kadiri mtu anavyofikiri hivi, ndivyo anavyokuwa kielelezo na umboasili wa uasi. Asili ya mtu ni maisha yake, ni kanuni ambayo anaitegemea ili kuendelea kuishi, na anashindwa kuibadilisha. Jinsi ilivyo hali ya usaliti—kama unaweza kufanya kitu ili kumsaliti ndugu au rafiki, hii inathibitisha kwamba ni sehemu ya maisha yako na hali ambayo ulizaliwa nayo. Hiki ni kitu ambacho hakuna mtu anaweza kukikana. Kwa mfano, kama mtu anapenda kuiba vitu vya watu wengine, basi hii “kupenda kuiba” ni sehemu ya maisha yake. Ni kwamba tu wakati mwingine anaiba, na wakati mwingine haibi. Bila kujali kama anaiba au la, haiwezi kuthibitisha kwamba kuiba kwake ni aina ya tabia. Badala yake, inathibitisha kwamba kuiba kwake ni sehemu ya maisha yake, yaani, asili yake. Baadhi ya watu watauliza: Kwa kuwa ni asili yake, basi kwa nini wakati mwingine anaona vitu vizuri lakini haviibi? Jibu ni rahisi sana. Kuna sababu nyingi kwa nini haibi, kama vile kama bidhaa ni kubwa mno kwake kuinyakua akitazamwa na watu, au hakuna wakati mzuri wa kutenda, au bidhaa ni ghali sana, imelindwa vikali, au hana nia hasa ya kitu kizuri kama hicho, au bado hajafikiria matumizi ya kitu hicho, na mengineyo. Sababu hizi zote zinawezekana. Lakini haidhuru, akikiiba au la, hii haiwezi kuthibitisha kuwa hiyo dhana humjia akilini kwa muda tu. Kinyume chake, hii ni sehemu ya asili yake ambayo ni ngumu kuirudia tena. Mtu kama huyo haridhiki na kuiba mara moja tu, lakini mawazo ya kudai vitu vya wengine kama vyake huamshwa wakati wowote anapokutana na kitu kizuri au hali inayofaa. Hii ndiyo sababu Nasema kwamba wazo hili haliinuki kila mara, lakini linatokana na asili ya mtu huyu mwenyewe.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp