Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kufunua Upotovu wa Wanadamu | Dondoo 363

02/09/2020

Nyote mnapaswa sasa kujichunguza haraka iwezekanavyo, ili muone ni kiasi gani cha kunisaliti kimebaki ndani yenu. Ninangojea jibu lenu kwa pupa. Msiwe wazembe katika kunishughulikia. Kamwe Mimi huwa sichezi michezo na watu. Nikisema Nitatenda jambo basi hakika Nitalitenda. Natumai kila mmoja wenu atakuwa mtu anayeyachukulia maneno Yangu kwa uzito, na asifikirie kana kwamba maneno hayo ni ubuni wa sayansi. Ninachotaka ni kitendo thabiti kutoka kwenu, siyo mawazo yenu. Baadaye, lazima mjibu maswali Yangu, ambayo ni kama ifuatavyo: 1. Ikiwa kwa kweli wewe ni mtendaji huduma, je, unaweza kutoa huduma Kwangu kwa uaminifu, bila dalili yoyote ya uzembe au mtazamo hasi? 2. Je, ukigundua kuwa Sijawahi kukuthamini, bado utaweza kusalia na kunitolea huduma ya maisha yote? 3. Ikiwa bado Ninakudharau sana licha ya wewe kutumia bidii nyingi, je, utaweza kuendelea kunifanyia kazi katika mashaka? 4. Ikiwa, baada ya wewe kufanya matumizi kwa ajili Yangu, Siyaridhishi mahitaji yako madogo, je, utavunjika moyo na kusikitishwa na Mimi, au hata ukasirike na kunitukana kwa sauti kubwa? 5. Ikiwa daima umekuwa mwaminifu sana, ukinipenda sana, ilhali unateseka na ugonjwa, umaskini, na kutengwa na marafiki na jamaa zako, au ikiwa unavumilia taabu nyingine zozote maishani, bado uaminifu na upendo wako Kwangu utaendelea? 6. Ikiwa hakuna lolote kati ya yale ambayo umefikiria moyoni mwako linalingana na kile ambacho Nimefanya, je, utaitembea njia yako ya baadaye kwa namna gani? 7. Ikiwa hupokei lolote kati ya mambo ambayo ulitarajia kupokea, je, unaweza kuendelea kuwa mfuasi Wangu? 8. Ikiwa hujawahi kuelewa kusudi na umuhimu wa kazi Yangu, je, unaweza kuwa mtu mtiifu ambaye hatoi hukumu kiholela na kufanya maamuzi? 9. Je, unaweza kuthamini maneno yote ambayo Nimeyanena na kazi yote ambayo Nimeifanya wakati Nimekuwa pamoja na wanadamu? 10. Je, unaweza kuwa mfuasi Wangu mwaminifu, aliye tayari kuvumilia mateso ya maisha kwa ajili Yangu, ingawa hupokei chochote? 11. Je, unaweza kuachilia kuzingatia, kupanga, au kuandaa njia yako ya kuendelea kuishi ya siku za baadaye kwa ajili Yangu? Maswali haya yanawakilisha mahitaji Yangu ya mwisho ninayotaka kutoka kwenu, nami Natumai kuwa ninyi nyote mnaweza kunipa majibu. Ikiwa umetimiza jambo moja au mawili ambayo maswali haya yanataka ufanye, basi lazima uendelee kujitahidi. Ikiwa huwezi kutimiza hata moja kati ya mahitaji haya, hakika wewe ni aina ya mtu ambaye atatupwa kuzimu. Sihitaji kusema chochote zaidi kwa watu kama hawa, kwa sababu hakika wao sio watu ambao wanaweza kukubaliana nami. Je, Ninawezaje kumweka nyumbani Kwangu mtu ambaye anaweza kunisaliti katika hali yoyote ile? Kwa wale ambao bado wanaweza kunisaliti katika hali nyingi, Nitazingatia utendaji wao kabla ya kufanya mipango mingine. Hata hivyo, wote wanaoweza kunisaliti, bila kujali ni chini ya hali gani, Sitawahi kusahau; Nitawakumbuka moyoni Mwangu, na kungojea fursa ya kulipiza matendo yao maovu. Mahitaji yote ambayo Nimeibua ni shida ambazo lazima nyote mzichunguze ndani yenu wenyewe. Natumai ninyi nyote mnaweza kuyazingatia kwa makini na kutonishughulika kwa uzembe. Hivi karibuni, Nitaangalia majibu ambayo mmenipa dhidi ya mahitaji Yangu. Kufikia wakati huo, Sitahitaji chochote zaidi kutoka kwenu na Sitawapa onyo lenye ari zaidi. Badala yake, Nitatumia mamlaka Yangu. Wale wanaopaswa kuhifadhiwa watahifadhiwa, wale wanaopaswa kupewa thawabu watapewa thawabu, wale wanaopaswa kukabidhiwa kwa Shetani watakabidhiwa kwa Shetani, wale wanaopaswa kuadhibiwa vikali wataadhibiwa vikali, na wale wanaopaswa kuangamia wataangamizwa. Kwa hiyo, hakutakuwa tena na mtu wa kunisumbua katika siku Zangu. Je, unaamini maneno Yangu? Je, unaamini kulipiza kisasi? Je, unaamini kuwa Nitawaadhibu wale waovu wote wanaonidanganya na kunisaliti? Je, unatarajia siku hiyo ije haraka au ije baadaye? Je, wewe ni mtu ambaye anaogopa adhabu, ama mtu ambaye angenipinga ingawa lazima avumilie adhabu? Siku hiyo itakapowadia, unaweza kukisia ikiwa utaishi katikati ya shangwe na kicheko, au ikiwa utalia na kusaga meno yako? Je, unatarajia kukumbana na mwisho wa aina gani? Je, umewahi kufikiria kwa uzito ikiwa unaniamini asilimia mia moja au una tashwishi nami asilimia mia moja? Je, umewahi kufikiria kwa uangalifu matendo na mwenendo wako vitakuletea matokeo ya aina gani? Je, unatumaini kwa kweli kuwa maneno Yangu yote yatatimizwa, ama unaogopa kuwa maneno Yangu yatatimizwa kama matokeo? Ikiwa unatumaini kuwa Nitaondoka hivi karibuni ili Niyatimize maneno Yangu, je, unapaswa kuyachukuliaje maneno na matendo yako mwenyewe? Ikiwa hutumainii kuondoka Kwangu na hutumaini maneno Yangu yote yatimizwe mara moja, kwa nini uniamini hata kidogo? Kwa kweli unajua mbona unanifuata? Ikiwa sababu yako ni kupanua upeo wako tu, hakuna haja ya kujisumbua kufanya hivyo. Ikiwa ni ili ubarikiwe na kuepukana na msiba unaokuja, mbona hujali kuhusu tabia yako mwenyewe? Mbona hujiulizi ikiwa unaweza kuyakidhi mahitaji Yangu? Mbona pia hujiulizi ikiwa unastahili kupokea baraka zitakazokuja?

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp