Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 225

22/09/2020

Licha ya ukweli kwamba ujenzi wa ufalme umeanza rasmi, maamkuzi kwa ufalme bado hayajatangazwa rasmi—sasa ni unabii tu wa kile kitakachokuja. Wakati ambapo watu wote watakuwa wamefanywa kamili na mataifa yote ya dunia kugeuka kuwa ufalme wa Kristo, basi huo utakuwa wakati ambapo radi saba zitanguruma. Siku ya sasa ni hatua ndefu ya kwenda mbele katika mwelekeo wa hatua hiyo, shambulio limeachiliwa huru kwa muda ujao. Huu ni mpango wa Mungu—hivi karibuni utafanikishwa. Hata hivyo, Mungu tayari amefanikisha yote ambayo Amesema. Hivyo, ni dhahiri kwamba mataifa ya dunia ni makasri tu yaliyo mchangani yanayotetemeka bamvua linapokaribia: Siku ya mwisho iko karibu sana na joka kubwa jekundu litaanguka chini ya neno la Mungu. Ili kuhakikisha kwamba mpango wa Mungu unatekelezwa kwa ufanisi, malaika wa mbinguni wameshuka juu ya dunia, wakifanya kila wanaloweza kumridhisha Mungu. Mungu Mwenyewe mwenye mwili Amejipanga katika uwanja wa vita kupigana na adui. Po pote ambapo Aliyepata mwili huonekana, adui anaangamiziwa mahali hapo. Uchina ni ya kwanza kuangamizwa, kuharibiwa kabisa kwa mkono wa Mungu. Mungu haipi Uchina upande wowote kabisa. Thibitisho la kuendelea kuanguka kwa joka kubwa jekundu linaweza kuonekana katika ukomavu wa watu unaoendelea. Hili linaweza kuonekana wazi na mtu yeyote. Ukomavu wa watu ni ishara ya kifo cha adui. Huu ni ufafanuzi kidogo wa kile kinachomaanishwa na “kufanya vita.” Hivyo, Mungu aliwakumbusha watu wakati mwingi watoe ushuhuda mzuri kwa Mungu kutangua hali ya fikira, ubaya wa joka kubwa jekundu ndani ya mioyo ya wanadamu. Mungu hutumia kumbusho kama hizo kuchangamsha imani ya mwanadamu na, kwa kufanya hivyo, Hutimiza ujuzi katika kazi Yake. Hili ni kwa sababu Mungu amesema, “Binadamu ana uwezo wa kufanya nini? Si ni afadhali Nifanye hivyo Mwenyewe?” Wanadamu wote wako hivyo. Si kwamba wao hawawezi tu, bali pia huvunjika moyo na husikitishwa kwa urahisi. Kwa sababu hii, hawawezi kumjua Mungu. Mungu hafufui tu imani ya mwanadamu, kwa siri Yeye humjaza mwanadamu nguvu siku zote.

Linalofuata, Mungu alianza kunena kwa ulimwengu wote. Mungu hakuanzisha tu kazi Yake mpya Uchina, Kotekote ulimwenguni Alianza kufanya kazi mpya ya leo. Katika hatua hii ya kazi, kwa vile Mungu anataka kufichua matendo Yake yote kotekote katika dunia ili wanadamu wote ambao wamemsaliti watakuja tena kuinama kwa utiifu mbele ya kiti Chake cha enzi, hivi ndani ya hukumu ya Mungu bado kuna huruma na upendo wa Mungu. Mungu hutumia matukio ya sasa kotekote ulimwenguni kutetemesha mioyo ya wanadamu, Akiiamsha kumtafuta Mungu ili waweze kumiminika kwenda Kwake. Hivyo Mungu asema, “Hii ni mojawapo ya njia ambazo Nafanya kazi, na bila shaka ni kitendo cha ukombozi kwa ajili ya mwanadamu, na kile Ninachompa bado ni aina ya upendo.”

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp