Korean Christian Song | Upendo wa Kweli wa Mungu | Haleluya! Msifuni Mungu! (Music Video)

12/05/2018

Leo naja mbele ya Mungu tena,

naona uso Wake wa kupendeza.

Leo naja mbele ya Mungu tena,

nimeacha siku zangu za zamani za kuzurura nyuma yangu.

Leo naja mbele ya Mungu tena,

kufurahia neno Lake kunanijaza na furaha.

Leo naja mbele ya Mungu tena,

moyo wangu una mengi ya kusema.

Ni maneno Yake mororo yanayoninyunyizia

na kunirutubisha ili nikue.

Ni maneno Yake makali yanayonitia moyo ili nisimame tena.

Ee Mungu! Tunaweza kukusifu kwa kuwa Umetuinua!

Tunaweza kukuimbia leo yote

kwa sababu ya baraka na neema Yako.

Ee Mungu, Unatupenda sana kweli!

Unatufanya tufurahie maneno Yako kila siku!

Ee Mungu, Unatupenda sana kweli! Unatupa nuru kila siku!

Ee Mungu, Unatupenda sana kweli!

Unawanyunyizia na kuwastawisha watu Wako.

Unatuepusha na ushawishi wa Shetani.

Ndugu, fanyeni upesi na muinuke! Tumsifu Mungu wetu!

Hebu tufurahie jinsi ambavyo Ametukusanya hapa leo.

Tuwe huru kabisa kutokana na mizigo ya mwili!

Sifa kwa Mwenyezi Mungu kwa bidii!

Tutimize wajibu wetu kwa moyo wetu wote na nguvu zote,

tuonyeshe upendo wetu kwa Mungu kwa matendo.

Tutakupenda milele, Mwenyezi Mungu wa Kweli!

kutoka kwa Mfuate Mwanakondoo na Imba Nyimbo Mpya

Umeme wa Mashariki, Kanisa la Mwenyezi Mungu lilianzishwa kwa sababu ya kuonekana na kazi ya Mwenyezi Mungu, ujio wa pili wa Bwana Yesu, Kristo wa siku za mwisho. Linashirikisha wale wote ambao wanaikubali kazi ya Mwenyezi Mungu katika siku za mwisho na ambao wameshindwa na kuokolewa kwa maneno Yake. Liliasisiwa kikamilifu na Mwenyezi Mungu mwenyewe na linaongozwa naye kama Mchungaji. Kwa hakika halikuanzishwa na mtu. Kristo ni ukweli, njia, na uzima. Kondoo wa Mungu husikia sauti ya Mungu. Mradi unasoma maneno ya Mwenyezi Mungu, utaona kuwa Mungu ameonekana.

Kauli Maalum: Uzalishaji huu wa video ulitengenezwa kama mradi usio wa faida na Kanisa la Mwenyezi Mungu. Wahusika wanaoonekana katika uzalishaji huu wanafanya kwa msingi wa kutotafuta faida, na hawajalipwa kwa njia yoyote. Video hii isisambazwe kwa mtu mwingine kwa minajili ya faida, na ni matumaini yetu kwamba kila mtu atashiriki kuigawa na kuisambaza hadharani. Wakati unapoisambaza, tafadhali sisitiza chanzo chake. Bila ridhaa ya Kanisa la Mwenyezi Mungu, hakuna shirika, kundi la kijamii, au mtu binafsi anayeweza kubadilisha au kuhudhurisha visivyo maudhui ya video hii.

Baadhi ya taarifa katika video hii zinatoka kwa:

FG LUT(https://filtergrade.com/free-cinematic-luts-video-editing/) By Filtergrade/CC BY 3.0(https://creativecommons.org/licenses/by/3.0/)

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp