Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kuingia Katika Uzima | Dondoo 521

09/09/2020

Kulikuwepo na kilele katika yale yote Petro alipitia, wakati mwili wake ulinyenyekea zaidi, lakini Yesu akampa himizo ndani kwa ndani. Na akajitokeza kwake mara moja. Wakati Petro alikuwa katika mateso makuu na moyo wake ulikuwa taabani, Yesu alimwelekeza: “Ulikuwa na Mimi ulimwenguni, na Nilikuwa na wewe hapa. Na Ingawa awali tulikuwa pamoja mbinguni, kwa hakika, huko ni, ulimwenguni kwa kiroho. Sasa Nimerudi kwenye ulimwengu wa kiroho, na wewe umo ulimwenguni. Kwani Mimi si wa ulimwengu, na Ingawa wewe pia si wa ulimwengu, lazima utimize kazi yako hapa ulimwenguni. Kwani wewe ni mtumishi, lazima uwajibike kwa njia bora zaidi uwezayo.” Petro alipata tulizo, kwa kusikia kwamba angeweza kurudi kwa upande wa Mungu. Wakati Petro alipokuwa katika masumbuko hayo karibu hali yake iwe mahututi kitandani, alisikitika kiasi cha kusema hivi: “Nimepotoka kwelikweli, siwezi kumtosheleza Mungu.” Yesu alijitokeza kwake na kusema: “Petro, huenda ikawa umesahau azimio ulilowahi kunitamkia Mimi? Je, kwa kweli umesahau kila kitu Nilichosema? Umesahau azimio ulilonitajia?” Petro aliona kwamba alikuwa Yesu na akainuka kutoka kitandani, naye Yesu akamkabili na kusema: “Mimi si wa ulimwengu, tayari Nimekuambia wewe—hili lazima uelewe, lakini umesahau kitu kingine Nilichokuambia? ‘Wewe pia si wa ulimwengu, si wa dunia.’ Sasa hivi kunayo kazi unayohitaji kufanya, huwezi kuhuzunika namna hivi, huwezi kuteseka hivi. Ingawa binadamu na Mungu hawawezi kuishi pamoja kwenye ulimwengu mmoja, Ninayo kazi Yangu na wewe unayo yako, na siku moja wakati kazi yako imekamilika, tutakuwa pamoja katika himaya moja, nami Nitakuongoza wewe kuwa pamoja Nami milele na milele.” Petro alipata tulizo na hakikisho baada ya kuyasikia maneno hayo. Alijua kuteseka huku kulikuwa ni jambo ambalo lazima angevumilia na kupitia, na akapata mhemko kuanzia hapo. Yesu alijitokeza haswa kwake katika ule muda muhimu, akimpa fahamisho na mwongozo maalum, na akifanya kazi nyingi ndani yake. Na ni nini ambacho Petro alijutia zaidi? Yesu alimwuliza Petro swali jingine (Ingawa haijarekodiwa kwenye Biblia kwa njia hii) si kipindi kirefu baadaye Petro alikuwa amesema “Wewe ndiwe Mtoto wa Mungu aliye hai,” nalo swali lenyewe lilikuwa: “Petro! Umewahi kunipenda?” Petro alielewa kile alichomaanisha, na kusema: “Bwana! Niliwahi kumpenda Baba wa mbinguni, lakini nakubali sijawahi kukupenda Wewe.” Yesu naye akasema: “Kama watu hawampendi Baba wa mbinguni, watawezaje kumpenda Mtoto hapa ulimwenguni? Na kama watu hawampendi Mtoto aliyetumwa na Mungu, Baba, wanawezaje kumpenda Baba aliye mbinguni? Kama kweli watu wanampenda Mtoto aliye ulimwenguni, basi kwa kweli wanampenda Baba aliye mbinguni.” Wakati Petro alipoyasikia maneno haya aligundua upungufu wake. Siku zote alihisi huzuni hadi kiwango cha kulengwalengwa na machozi machoni kutokana na maneno yake “niliwahi kumpenda Baba wa mbinguni, lakini sikuwahi kukupenda Wewe.” Baada ya ufufuo na kupaa angani kwa Yesu alihuzunika na kuwa na simanzi zaidi kwa yale yote yaliyokuwa yamefanyika. Huku akikumbuka kazi yake iliyopita na kimo chake cha sasa, mara nyingi angekuja mbele ya Yesu kwa maombi, siku zote akiwa na hisia za majuto na masikitiko kwa kutoweza kutosheleza tamanio la Mungu, na kutoweza kufikia viwango vya Mungu. Masuala haya yakawa ndiyo mzigo wake mkubwa. Alisema: “Siku moja nitatoa kila kitu changu nilichonacho na kila kitu kinachonifanya mimi kuwa mimi kwa ajili Yako, nitakupa kile chenye thamani zaidi.” Alisema: “Mungu! Ninayo imani moja tu na upendo mmoja tu. Maisha yangu hayana thamani ya chochote, na mwili wangu hauna thamani ya chochote. Ninayo imani moja tu na upendo mmoja tu. Ninayo imani kwako Wewe katika akili yangu na upendo Kwako wewe katika moyo wangu; mambo haya mawili tu ndiyo niliyonayo kukupatia Wewe, na wala sina kingine chochote.” Petro alihimizwa pakubwa na maneno yake Yesu, kwa sababu kabla ya Yesu kusulubishwa alikuwa amemwambia: “Mimi si wa ulimwengu huu, na wewe pia si wa ulimwengu huu.” Baadaye, wakati Petro alipofikia hali ya maumivu makali, Yesu alimkumbusha: “Petro, je, umesahau? Mimi si wa ulimwengu huu, na ni kwa ajili tu ya kazi Yangu ndipo Niliondoka mapema. Wewe pia si wa ulimwengu huu, umesahau? Nimekuambia mara mbili, kwani hukumbuki?” Petro alimsikia na kumwambia: “Sijasahau!” Yesu naye akasema: “Uliwahi kuwa na wakati mzuri ukiwa umekusanyika pamoja na Mimi kule mbinguni na kwa kipindi fulani kando Yangu mimi. Unanidata Mimi, na Mimi ninakudata. Ingawa viumbe hivi havistahili kutajwa katika macho Yangu, ninawezaje kukosa kupenda yule ambaye hana hatia na anapendeka? Je, umesahau ahadi Yangu? Lazima ulikubali agizo Langu hapa ulimwenguni, lazima utimize kazi Niliyokuaminia. Bila shaka siku moja Nitakuongoza kuwa kando Yangu.” Baada ya kuyasikia haya, Petro akahimizwa zaidi, na kupata mhemko mkubwa zaidi, kiasi cha kwamba alipokuwa msalabani, aliweza kusema hivi: “Mungu! Siwezi kukupenda vya kutosha! Hata ukiniomba kufa, siwezi bado kukupenda vya kutosha! Popote Utakapotuma nafsi yangu, utimize au ukose kutimiza ahadi Zako, chochote ufanyacho baadaye, ninakupenda na ninakuamini.” Kile alichoshikilia kilikuwa imani yake, na upendo wa kweli.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp