Wimbo wa Kusifu | Natamani Ningekuwa na Mungu Kila Siku (Music Video)

22/03/2020

Siku ile Uliyotuacha, Ulikuwa na tabasamu usoni Mwako.

Ulitupungia mkono kwaheri. Na kwa huzuni tulikutazama Ukienda.

Nilijua kwamba makanisa yalikuhitaji, hivyo singekushikilia.

Niliutazama mgongo Wake alipokuwa Akitembea na kutokomea,

ningehifadhi Ulichoniaminia.

Kila ninapokuwa mnyonge, nafikiri kuhusu gharama Uliyolipa.

Upendo Wako wa kweli, maneno Yake yenye nguvu,

yanauchangamsha na kuupa joto moyo wangu,

nahisi mdeni sana Kwako.

Najichukia kwa kuujali mwili wangu kupita kiasi,

nikihisi asiyestahili kuja mbele Yako.

Kila ninapoufikiria upendo wa Mungu, moyo wangu unatiwa moyo mara dufu.

Nataka kuwa ubavuni mwa Mungu na kufanya wajibu wangu,

na nahisi kuwa kimo changu ni kidogo sana.

Nitakua lini niwe mtu anayeweza kuwa ubavuni mwa Mungu na kumtumikia?

Nimeazimia kutenda neno la Mungu ili maisha yangu yakue haraka.

Mungu, nataka kuwa upande Wako na kukuambia siri zangu zote.

Nakumbuka tulipokuwa pamoja, na inaufanya moyo wangu kufurahi.

Unaishi kwa unyenyekevu mbele ya wanadamu,

na kututolea ukweli na uzima.

Tunakutazamia Wewe na tunataka kuwa na Wewe.

Mungu, nataka kuwa upande Wako na kukuambia siri zangu zote.

Nakumbuka tulipokuwa pamoja, na inaufanya moyo wangu kufurahi.

Unaishi kwa unyenyekevu mbele ya wanadamu,

na kututolea ukweli na uzima.

Tunakutazamia Wewe na tunataka kuwa na Wewe.

Tunakutazamia Wewe na tunataka kuwa na Wewe.

kutoka katika Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp