Maneno ya Mungu ya Kila Siku: Kujua Kazi ya Mungu | Dondoo 212

18/09/2020

Katika siku za mwisho, Mungu alipata mwili ili kufanya kazi Aliyopaswa kufanya na kutekeleza huduma Yake ya maneno. Alikuja yeye mwenyewe ili kufanya kazi kati ya wanadamu kwa lengo la kuwakamilisha wale watu ambao wanaipendeza nafsi Yake. Kutoka wakati wa uumbaji hadi leo Yeye hufanya tu hiyo kazi wakati wa siku za mwisho. Ni wakati wa siku za mwisho tu ambapo Mungu alipata mwili ili kufanya kazi kwa kiwango kikubwa. Ingawa Yeye huvumilia shida ambazo watu wanaweza kupata ugumu kuvumilia, ingawa Yeye kama Mungu mkuu ana unyenyekevu wa kuwa mtu wa kawaida, hakuna kipengele cha kazi Yake kimecheleweshwa, na mpango Wake haujatupwa katika mchafuko hata kidogo. Anafanya kazi kulingana na mpango Wake wa awali. Mojawapo ya madhumuni ya kupata mwili huku ni kuwashinda watu. Mengine ni kuwakamilisha watu Anaowapenda. Yeye hutamani kuwaona kwa macho Yake mwenyewe watu Anaowakamilisha, na Yeye hutaka kujionea Mwenyewe jinsi watu Anaowakamilisha humshuhudia. Sio mtu mmoja ambaye hukamilishwa, na sio wawili. Hata hivyo, ni kikundi cha watu wachache sana. Kikundi hiki cha watu huja kutoka nchi mbalimbali za dunia, na kutoka kwa makabila mbalimbali ya ulimwengu. Kusudi la kufanya kazi hii nyingi ni kukipata kikundi hiki cha watu, kupata ushuhuda ambao kikundi hiki cha watu humtolea, na kupata utukufu ambao Yeye hupata kupitia kwa kikundi hiki cha watu. Yeye hafanyi kazi ambayo haina umuhimu, wala hafanyi kazi ambayo haina thamani. Inaweza kusemwa kuwa, kwa kufanya kazi nyingi sana, lengo la Mungu ni kuwakamilisha watu wote ambao Yeye anataka kuwakamilisha. Katika wakati wowote wa ziada Alio nao nje ya hili, Atawaondosha wale walio waovu. Jua kwamba Haifanyi kazi hii kubwa kwa sababu ya wale walio waovu; kwa kinyume, Yeye hufanya kadri Awezavyo kwa sababu ya idadi hiyo ndogo ya watu ambao hawana budi kukamilishwa na Yeye. Kazi ambayo Yeye hufanya, maneno ambayo Yeye hunena, siri ambayo Yeye hufichua, na hukumu Yake na adhabu zote ni kwa ajili ya idadi hiyo ndogo ya watu. Yeye hakupata mwili kwa sababu ya wale walio waovu, sembuse wao kuchochea ghadhabu kubwa ndani Yake. Yeye husema ukweli, na huzungumzia kuingia, kwa sababu ya wale watakaokamilishwa, Alipata mwili kwa sababu yao, na ni kwa sababu yao Yeye hutoa ahadi na baraka Zake. Ukweli, kuingia, na maisha katika ubinadamu ambayo Yeye huzungumzia si kwa ajili ya wale walio waovu. Yeye hutaka kuepuka kuzungumza na wale walio waovu, na hutaka kuwapa wale ambao watakamilishwa ukweli wote. Lakini kazi Yake inahitaji kwamba, kwa sasa, wale walio waovu waruhusiwe kufurahia baadhi ya utajiri Wake. Wale ambao hawatekelezi ukweli, ambao hawamridhishi Mungu, na ambao hukatiza kazi Yake wote ni waovu. Hawawezi kukamilishwa, na wanachukiwa kabisa na kukataliwa na Mungu. Kwa kinyume, watu ambao hutia ukweli katika vitendo na wanaweza kumridhisha Mungu na ambao hujitolea wenyewe kabisa katika kazi ya Mungu ndio watu ambao watakamilishwa na Mungu. Wale ambao Mungu hutaka kuwakamilisha sio wengine bali ni kikundi hiki cha watu, na kazi ambayo Mungu hufanya ni kwa ajili ya watu hawa. Ukweli ambao Yeye huzungumzia unaelekezwa kwa watu ambao wako tayari kuutia katika vitendo. Yeye huwa hazungumzi na watu ambao hawatii ukweli katika vitendo. Ongezeko la umaizi na ukuaji wa utambuzi ambao Yeye huzungumzia umelengwa kwa watu ambao wanaweza kutekeleza ukweli. Anapozungumza juu ya wale ambao watakamilishwa Yeye anazungumzia watu hawa. Kazi ya Roho Mtakatifu inaelekezwa kwa watu ambao wanaweza kutenda ukweli. Mambo kama kumiliki hekima na kuwa na ubinadamu yanaelekezwa kwa watu ambao wako tayari kutia ukweli katika vitendo. Wale ambao hawatekelezi ukweli wanaweza kusikia maneno mengi, lakini kwa sababu wao ni waovu sana kiasili na hawavutiwi na ukweli, kile wanachoelewa is mafundisho ya dini na maneno tu, na nadharia tupu, bila kujali hata kidogo kuingia kwao katika maisha. Hakuna hata mmoja wao aliye mwaminifu kwa Mungu; wao wote ni watu wanaomwona Mungu lakini hawawezi kumpata; wote wamehukumiwa na Mungu.

Kimetoholewa kutoka katika Neno Laonekana katika Mwili

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp