Tenzi ya Rohoni | Nimeuona uzuri wa Mungu (Music Video)

09/08/2017

I

Nasikia sauti ijulikanayo ikiniita mara kwa mara.

Nikaamka na kuangalia kuona, ni nani aliye pale akizungumza.

Sauti yake ni nyororo lakini kali, picha Yake nzuri!

Nateseka kupigwa na kuvumilia maumivu makubwa, nikipapaswa na mkono Wake wenye upendo.

Halafu natambua ni Mwenyezi ambaye nilipigana naye.

Najichukia mwenyewe, kwa majuto makubwa, fikiria niliyoyafanya.

Nimepotoka kwa kina, hakuna wanadamu, sasa nauona ukweli.

Pamoja na mwanzo mpya, kujiingiza katika maisha halisi, kutimiza wajibu wangu.

Kwa hali, kushindana na Mungu, mimi siheshimiki.

Mungu bado Mungu, mtu ni mtu—mimi ni mjinga sana.

Mjinga na mwenye kiburi kiasi cha kutoijua nafsi yangu halisi.

Nilikosa aibu na kutahayarika; moyo wangu umejaa majuto.

Najichukia mwenyewe, bila kujua kile ninachoishia.

Shetani alinikanyaga kwa miaka mingi sana, nikawa mdharauliwa.

Wakishapewa sumu na yule Mwovu, wanadamu wamepotea.

Kama sitabadilishwa na kuzaliwa upya, sina maisha ya kweli.

II

Tabia yangu potovu hunisumbua, huduma yangu bado i bure.

Ni mjinga wa kumjua Mungu, na kujawa na dhana; jinsi gani mimi singepinga?

Mungu hunihukumu, kwa uasi wangu, na ukosefu wa uadilifu.

Nimeuona upendo wa kweli wa kuadibu na kuhukumu.

Mungu ni mwenye haki, mimi nina hakika kabisa.Niko ana kwa ana naye.

Wokovu wa vitendo wa Mungu umenisaidia kufika uambali huu.

Uhalisi wa Mungu na uweza wake, vimefichuliwa kikamilifu kwa mtu.

Kwa kuishi katika mwanga, namjua Mungu na kuuona uzuri wake.

Nikiwa na nia ya kutimiza wajibu, Nitamtosheleza Mungu na kumpenda.

kutoka kwa Mfuateni Mwanakondoo na Kuimba Nyimbo Mpya

Tazama zaidi

Ulimwengu umezongwa na maangamizi katika siku za mwisho. Je, hili linatupa onyo lipi? Na tunawezaje kulindwa na Mungu katikati ya majanga?

Leave a Reply

Shiriki

Ghairi

Wasiliana nasi kupitia WhatsApp